John Tendwa Live on ITV katika 'Kipima Joto' cha Masako!

Mzee Markusi anaweka wazi kuwa hapa inaonekana wazi kuwa ccm inatumia polisi kuwadhibiti wapinzani, lakini je leo chama kama chadema kikiingia madarakani pia kitawatumia polisi hawahawa kuwangamiza ccm
 
Tendwa kabanwa vibaya anajiumauma tu....jamaa mwenye shati jeupe anambana sana anamwamba sio kwamba polisi wanapambana na vyama polisi wanapambana na chama tena jamaa kataja ni chadema kasema polisi wanapambana na chama ambacho kinakinyemelea chama tawala Tendwa analo leo lol.....
 
Kunajamaa anasema c c m inatumia polisi kuidhibiti chadema mmapa msajili wa vyamaanatoka jasho mashavuni kwenye vipele
 
Bwana Sungusia anatoa mfano anasema fikiria refa anachezesha mpira halafu baada ya mechi refa anaenda kujiunga na moja wapo ya timu alizokuwa akizichezesha, je watu (mashabiki) watamuamini vp huyo refa kuwa alikuwa neutral? coz hawa mapolisi baadhi ndio wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa pia...
 
Lazima 2we na jeshi la polisi ambalo ni sawa haliegemie pande yoyote jamaa anasema
 
Kwa ujumla huyu Tendwa ana wakati mgumu ktk nafasi aliyonayo na asipojiuzulu hakika siku moja anaweza akaanguka kwa presha!
Tukaeni na tutaona!
 
Hivi Tendwa kwa kweli uwa simuelewa kwanza anajifanya kiswahili kinampa shida halafu ana tabia za kibabe ambazo zinamfanya awe anropoka hovyo.

Ritz huyu mzee ni zaidi ya matatizo hivi kumbe kuwa mzee ni matatizo hivi, au ni huyu tu??
 
Ukimuwaza na kumfikiria sana Mzee Tendwa utagundua vitu kadhaa kwake.

1. Unaweza kusema kuwa ni mnafiki na mchonganishi. Ukimfikiria hivi, unajijazia uzito wa hoja yako kwa kukumbuka kauli alizozitoa kule Arumeru kuhusu Glema wakati wa uchaguzi ulio mpa Nassari ubunge, alisema "Wazee wa kimila (washiri) wamesema hawataki kumuona Lema Arumeru na wakimuona wana wata mdhuru" ilikuwa kauli yake haikuwa kauli ya wazee, yeye msimamazi wa vyama vya siasa akachagua upande! _Unafiki.

2. Ukisema kuwa ni kibaraka anae panga mipango ovu na ccm kwa kivuli cha usajili na u- refarii wa vyama vya siasa pia huwezi kukosea! Jijazie hoja yako kwa kurejea kwenye kauli yake ya kufuta vyama vitakavyo sababisha mauwaji! Hapa alimaanisha cdm. Kumbuka maneno ya kina Nape, shigella na Nchimbi halafu kauli za polisi kuhusu mauwaji. Kama una akili timamu huhitaji kuwa na shahada ya chuo kikuu kujua kuwa kulikuwa na mpango mkubwa ulioshindwa nyuma yake! Mpango umeshindwa kwa kuwa Mungu alipanga kuwaumbua. Kusinge patikana picha za muuwaji wa Mwangosi ndio tunge ona rangi halisi za Tendwa kupitia kauli za Nape, Shigella, Nchimbi na jeshi la polisi.

3. Unaweza kusema pia kuwa mzee wetu Tendwa hajui analolifanya bali anaendeshwa kwa remote control! Kwa kuwa hakuna viongozi wa serikali wanao ikemea ccm na yeye hakemei matendo yao! Kwa kuwa wapo. Viongozi wa serikali wano ikemea cdm kwa kuwa wana ihofu na inawapa tumbo joto nae anungwana nao hata panapo kuwa na upendeleo wa wazi! Anailamu chadema kwa kuandamana anaifumbia macho ccm ikiandamana maana niya chama tawala na wao ndio wamempa ulaji.

Tendwa ni mzee wetu lakini naweza kuthubutu kusema kuwa mzee wetu anajivua heshima yake kwa kuwa kipofu mbele ya ccm na kuvaa darubini mbele ya cdm.

Sent from BlackBerry 8520 authorized by JamiiForums.
 
Kwa hiyo ni lazima tufanye kama nchi zingine wanavyo fanya?

TENDWA anasema inapotokea barua ya polisi ikachelewa kukufikia katika kuahirisha mkutanonwako, anasema busara inapaswa kutumika, anasema swala la mauaji ya polisi kwa raia hayatokei hapa kwetu tu anasema yanatokea nchi zoote duniani... naona Uzee si kitu kizuri
 
Sasa si mseme anachoongea badala ya kuanza kuponda tu kama mazumbukuku. Ooh Tendwa ana manundu, mara ana virusi, mara ana wadogo zake wanaitwa Tendeana. Hayo ndiyo mambo ya kuchangia watu wenye akili zenu? Watu wengine bwana.

Mfano wa upuuzii anaoongea ni kwamba 'mauaji ni swala la kawaida'.... Itakuwa virus wameshaanza kutafuna ubongo, sijui kama ana ela za ku change blood kama muajiri wake afanyavyo... Mizee kama hii ni bora ipumzishwe, inakera...
 
Kumbe mabadiliko yanawezekana wajamen????

Haya ndio majibu ya Ritz kweli??

Hivi Tendwa kwa kweli uwa simuelewa kwanza anajifanya kiswahili kinampa shida halafu ana tabia za kibabe ambazo zinamfanya awe anropoka hovyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom