John Shibuda: Tundu Lissu ni Interahamwe

John Shibuda: Tundu Lissu ni Interahamwe

MwanaDiwani

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2013
Posts
5,536
Reaction score
2,268
SIKU moja baada ya Mbunge wa Maswa Magharibi, mkoani Simiyu, Bw. John Shibuda kutangaza kuachia ngazi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mbunge huyo ameibuka tena na kusema aliahidiwa kupewa helikopta mbili na uongozi wa chama hicho aweze kuzitumia katika kampeni za Uchaguzi Mkuu 2010 lakini hakupewa.

Alisema uongozi wa chama hicho ukiongozwa na Katibu Mkuu, Dkt. Wilbrod Slaa, ulimwahidi kumpa helikopta hizo kwenye kampeni zake na kumpigia debe Katibu huyo aliyekuwa akiwania nafasi ya urais.

Bw. Shibuda aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Malampaka, wilayani Maswa na kuongeza kuwa, alijitolea kutumia pesa zake katika uchaguzi huo na kuahidiwa kurudishiwa lakini mpaka sasa bado kurudishwa.
"Katika kampeni za mwaka 2010, mbali ya kuahidiwa helikopta, pia nilikuwa chanzo kikubwa cha Dkt. Slaa kupata kura nyingi kwa mara ya kwanza na kuongoza kwenye Wilaya ya Maswa akimzidi mgombea mwenzake kutoka CCM, Rais Jakaya Kikwete.

"Helikopta nilizoahidiwa, hata wakati wa kampeni sikupewa, nilipouliza niliambiwa nitapewa...mimi ndiye chanzo kikubwa cha Rais Kikwete kupata kura ndogo katika jimbo langu, nilitumia gharama zangu kumfanyia kampeni Dkt. Slaa," alisema.
Wakati huo huo, Bw. Shibuda alisema msimamo wake ni Serikali mbili na kusisitiza hawezi kuwaunga mkono wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ambao msimamo wao ni Serikali tatu ambazo zitawaongezea mzigo wananchi wangu ambao ni wakulima na wafugaji.

Bw. Shibuda alisema wananchi wake hawataki kuongezewa mzigo wa Serikali; bali wanataka kutatuliwa kero walizonazo hasa zinazohusu kilimo cha pamba, migogoro ya wakulima na wafugaji.

"Siko tayari kuunga mkono muundo wa Serikali tatu kwa sababu wakulima wa pamba wana matatizo makubwa katika bei ya zao hili na pembejeo, pia katika wilaya yangu kuna migogoro mikubwa ya wakulima na wafugaji inayopaswa kutatuliwa kwa serikali hii tuliyonayo," alisema Bw. Shibuda.
Katika mkutano huo, Bw. Shibuda alikwenda mbali zaidi akimfananisha Mbunge wa Singida Mashariki ambaye pia ni Mwanasheria wa chama hicho, Bw. Tundu Lissu na kundi la Interahamwe lililochochea ubaguzi wa kikabila uliosababisha mauaji ya kimbari nchini Rwanda akidai mbunge huyo amekuwa mchochezi wa vita ndani na nje ya chama.

"Tundu Lissu ni Interahamwe kwani amekuwa mtu wa mchochezi mwenye tabia ya kuwatukana wenzake, hana tofauti na kundi hili kama wenzake walivyosababisha mauaji nchini Rwanda," alisema.

Alisisitiza kuwa amechoka kusikia hukumu dhidi yake kila siku kupitia vyombo vya habari kutoka kwa viongozi wake wa Chadema, huku akitoa mfano kuwa alipounga mkono nyongeza ya posho ya Bunge, aliitwa ‘Msaliti', lakini leo wabunge wote wakiwemo wa Chadema waliogomea wanachukua posho hiyo.

"Wazee wangu niliposema bungeni posho iongezwe, niliitwa mie ‘Msaliti' na wabunge wa Chadema lakini leo kila mmoja muulizeni hata huyu Kasulumbayi (Sylvester, Mbunge wa Maswa Mashariki, Chadema), ambaye tunaye hapa kwenye kikao kama hachukui posho hizo.

"Hata huyo Tundu Lissu anayeongea sana anachukua, hata Mbowe (Freeman, Mwenyekiti wa Chadema) alikataa gari la Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, lile la Serikali lakini hadi leo analitumia… mbona yeye haitwi ‘Msaliti'?" Alihoji Shibuda.

Chanzo: Habari leo
 
Kabla ya uchaguzi wa viongozi wakuu ndani ya CHADEMA tutaendelea kusikia mengi hasa ikichukuliwa kuwa tarehe ya Uchaguzi imebadilishwa mara tatu.

Haya ndiyo matokeo ya baadhi ya viongozi ndani ya chama kujijenga katika misingi ya kilaghai.

Kila uchaguzi wa ndani ukikaribia, lazima kuna baadhi ya viongozi watapata misukosuko ndani ya CHADEMA na hata kufukuzwa uongozi na uanachama.

Tutaona na kusikia mengi!
 
Kumjadili Tundu Lissu ni kupoteza muda huyo ni mgonjwa
 
[FONT=times
new roman]SIKU mbili baada ya Mbunge wa Maswa Magharibi, mkoani Simiyu,
Bw. John Shibuda kutangaza kuachia ngazi ndani ya Chama cha Demokrasia
na Maendeleo (CHADEMA), mbunge huyo ameibuka tena na kumfananisha Mbunge
wa Singida Mashariki ambaye pia ni Mwanasheria wa chama hicho, Bw.
Tundu Lissu na kundi la Interahamwe lililochochea ubaguzi wa kikabila
uliosababisha mauaji ya kimbari nchini Rwanda akidai mbunge huyo amekuwa
mchochezi wa vita ndani na nje ya chama.

"Tundu Lissu ni Interahamwe kwani amekuwa mtu mchochezi mwenye tabia ya
kuwatukana wenzake, hana tofauti na kundi hili kama wenzake
walivyosababisha mauaji nchini Rwanda," alisema.

Bw. Shibuda alikwenda mbali zaidi na kudai aliahidiwa kupewa helikopta
mbili na uongozi wa chama hicho aweze kuzitumia katika kampeni za
Uchaguzi Mkuu 2010 lakini hakupewa.
Alisema uongozi wa chama hicho ukiongozwa na Katibu Mkuu, Dkt. Wilbrod
Slaa, ulimwahidi kumpa helikopta hizo kwenye kampeni zake na kumpigia
debe Katibu huyo aliyekuwa akiwania nafasi ya urais.

Bw. Shibuda aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika
katika Kata ya Malampaka, wilayani Maswa na kuongeza kuwa, alijitolea
kutumia pesa zake katika uchaguzi huo na kuahidiwa kurudishiwa lakini
mpaka sasa bado kurudishwa.

"Katika kampeni za mwaka 2010, mbali ya kuahidiwa helikopta, pia
nilikuwa chanzo kikubwa cha Dkt. Slaa kupata kura nyingi kwa mara ya
kwanza na kuongoza kwenye Wilaya ya Maswa akimzidi mgombea mwenzake
kutoka CCM, Rais Jakaya Kikwete.

"Helikopta nilizoahidiwa, hata wakati wa kampeni sikupewa, nilipouliza
niliambiwa nitapewa...Mimi ndiye chanzo kikubwa cha Rais Kikwete kupata
kura ndogo katika jimbo langu, nilitumia gharama zangu kumfanyia kampeni
Dkt. Slaa," alisema.

Wakati huo huo, Bw. Shibuda alisema msimamo wake ni Serikali mbili na
kusisitiza hawezi kuwaunga mkono wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba
kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ambao msimamo wao ni Serikali
tatu ambazo zitawaongezea mzigo wananchi wangu ambao ni wakulima na
wafugaji.

Bw. Shibuda alisema wananchi wake hawataki kuongezewa mzigo wa Serikali;
bali wanataka kutatuliwa kero walizonazo hasa zinazohusu kilimo cha
pamba, migogoro ya wakulima na wafugaji.

"Siko tayari kuunga mkono muundo wa Serikali tatu kwa sababu wakulima wa
pamba wana matatizo makubwa katika bei ya zao hili na pembejeo, pia
katika wilaya yangu kuna migogoro mikubwa ya wakulima na wafugaji
inayopaswa kutatuliwa kwa serikali hii tuliyonayo," alisema Bw. Shibuda.
Chanzo: Majira[/FONT]

mfa maji haishi kutapatapa bwana, ulikutana na wajanja wenzio
 
Kumjadili Tundu Lissu ni kupoteza muda huyo ni mgonjwa
Ukiwa CCM kama wewe kweli kumjadili Tundu Lissu ni headache sababu anasema yale ambayo nyie hamtaki yasemwe.Sasa nyie CCM ole wenu mtupe katiba mdebwedo?
 
Huyu shibuda absolutely mwehu hiv kuna nchi inayoweza kuendelea bila uongoz makini ni lazms mjadili aina gani ya uongoz wanaihitaji ni lazma watu wajadili vipi wataongozwa na vp mgawanyo wa madaraka utakuwa :banghead: mgawanyo wa madaraka utKuwa
 
Nterahamwe wako bungeni kuchakachua rasimu ya katiba.Kwani na Lisu amerudi bungeni kuchakachua rasimu?.
 
Ukiwa CCM kama wewe kweli kumjadili Tundu Lissu ni headache sababu anasema yale ambayo nyie hamtaki yasemwe.Sasa nyie CCM ole wenu mtupe katiba mdebwedo?
Ndugu, CCM haitoi katiba katika stage zote nne za mchakato wa Katiba.

Katiba inatolewa na wananchi wenye haki kisheria kupiga kura ya maoni baada ya katiba mpya kutungwa na bunge la Maalum.
 
NENO itarahamwe sasa ndiyo limepatiwa mtu sahihi, siyo yale matusi ya LIPUMBA
 
Shibuda mbona anarudia yale yale??
kama ana hoaja za maana aziweke hapa sio story zile zile za kila siku.
Mchawi akiwa anakata roho huropoka hovyo yale yote yaliyomjaa.
 
Kabla ya uchaguzi wa viongozi wakuu ndani ya CHADEMA tutaendelea kusikia mengi hasa ikichukuliwa kuwa tarehe ya Uchaguzi imebadilishwa mara tatu.

Haya ndiyo matokeo ya baadhi ya viongozi ndani ya chama kujijenga katika misingi ya kilaghai.

Kila uchaguzi wa ndani ukikaribia, lazima kuna baadhi ya viongozi watapata misukosuko ndani ya CHADEMA na hata kufukuzwa uongozi na uanachama.

Tutaona na kusikia mengi!
YOTE haya yanasababishwa na madikteta wawili na siyo vinginevyo akila LISSU wanatekeleza tu kazi yao ya UKIBARAKA kwa mabwana wao.
 
Shibuda mbona anarudia yale yale??
kama ana hoaja za maana aziweke hapa sio story zile zile za kila siku.
Mchawi akiwa anakata roho huropoka hovyo yale yote yaliyomjaa.
msisitizo ni muhimu mkuu, sisi walimu tunaamini mwalimu hata uwe mzuri vipi darasani kama haukazii maarifa baada ya kipindi wanafunzi wako wataambulia patupu. SHIBUDA yuko sahihi kabisa.
 
Ndugu, CCM haitoi katiba katika stage zote nne za mchakato wa Katiba.

Katiba inatolewa na wananchi wenye haki kisheria kupiga kura ya maoni baada ya katiba mpya kutungwa na bunge la Maalum.

Bunge na Wananchi kila mmoja ana nafasi yake katika kupatikana Katiba mpya, hakuna wa kubezwa.
 
hiki chama bora kifutwe kabisa, hakipo kwa masilahi ya wananchi kila anayeonesha nia na akapingana na mawazo ya mwenyekiti huyo tayari anaitwa msaliti!
 
hiki chama bora kifutwe kabisa, hakipo kwa masilahi ya wananchi kila anayeonesha nia na akapingana na mawazo ya mwenyekiti huyo tayari anaitwa msaliti!

watu wa ajabu sana CHADEMA, hivi kwa nini hawataki kukubali kuwa MBOWE na SLAA ndiyo tatizo?
 
"Tundu Lissu ni Interahamwe kwani amekuwa mtu mchochezi mwenye tabia ya kuwatukana wenzake, hana tofauti na kundi hili kama wenzake walivyosababisha mauaji nchini Rwanda," alisema.

Hizi siasa za kibongo zinashangaza...

Yaani unalalamika kuwa mwenzako ni mchochezi na mwenye kutukana wenzake wakati huo huo nawe unatumia lugha ya kichochezi na matusi kumkosoa...
 
Ndugu, CCM haitoi katiba katika stage zote nne za mchakato wa Katiba.

Katiba inatolewa na wananchi wenye haki kisheria kupiga kura ya maoni baada ya katiba mpya kutungwa na bunge la Maalum.

Hiyo Kura ya Maoni inasimamiwa na Tume ipi? Hivi wewe ni mgeni hapa Tz hadi Uiamini hii tume ya Uchaguzi Ya CCM?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom