Abdulhalim
Platinum Member
- Jul 20, 2007
- 17,217
- 3,125
Kumbe shida ni upinzani tu? kaa ndio hamna ishu hapa..Ishu ni kwamba hii njemba ndio iliyosimamia uuzwaji wa nyumba za serikali.. yaani mafisi wanagawana mali za baba kabla hajafa, tena kwa bei ya kutupa (ya jioni )..Cha ajabu kuna wadanganyika wanadhani this kafiri inaweza kuvaa viatu vya urais..same goes to Mamvi..hii nchi imelaaniwa.
Ni kweli anachapa kazi lakini naye amezidi kuropoka na kupenda misifa.
2008 mita 22.5, 2010 mita 30, 2014 mita 37.5, 2017 mita ....... Hapo kuna nyumba itakayobaki? Magufuli jitahidi kwenda kistarabu sio kila ukijisikia tu unaongeza upana wa barabara unawapa presure wazee wetu wasio na ajira.
Bora anayechapa kazi zikaonekana, anaropoka na kupenda sifa kuliko yule asiyefanya lolote. Hebu jiulizeni, Chenge na Kawambwa walifanya nini kwenye wizara hiyo?
Ay bora ngereja asiyesema lolote lakini makali yake watanzania wa ngazi zote tunaya feel?
I am not sure if we are becoming fair to Dr. John Pombe Magufuli. Among the ministers, nani ni bora? nani mwenye nafuu? probably, mkiangalia sana, mtarudi kwa Magufuli.
Just thinking aloud.
Very fair comment but people wil not want it!
Natamani angesome hizi comment zako kwa kweli.
Ni kweli ni mchapakazi nadhani angekazana kuhakikisha miundombinu iko safi badala ya kuanza kuponda. Atuachie wananchi tuamue
Magufuli ana mdomo mchafu sana na jimbo kwake hakubaliki
Bora anayechapa kazi zikaonekana, anaropoka na kupenda sifa kuliko yule asiyefanya lolote. Hebu jiulizeni, Chenge na Kawambwa walifanya nini kwenye wizara hiyo? Ni wakati ule wa Chenge ndio kulitokea msongamano mkubwa wa magari yalipokwamna kule Singida. Waht did he do? Sasa sana aliwaponda Watanzania na ushamba wetu wa kushabikia vijisenti!
Au bora Bwana umeme/mafuta Ngereja asiyesema lolote lakini makali yake Watanzania wa ngazi zote tunaya feel? yeye sio mropokaji. This is true!
I am not sure if we are becoming fair to Dr. John Pombe Magufuli. Among the ministers, nani ni bora? nani mwenye nafuu? probably, mkiangalia sana, mtarudi kwa Magufuli.
Just thinking aloud.
Tatizo la wachangiaji wengi ni jazba isiyo kifani kiasi cha kukosa hoja. Magufuli ni CCM tusitegemee hata siku moja akasifia CDM. Akiponda CDM yuko sahihi maana ndio kazi yake kama mwanachama wa CCM. CDM msitake kupokea sifa tu, hizi ni dalili za udikteta. Inaelekea mkipewa madaraka makubwa rangi yenu itaonekana zaidi.
Mwanzoni tulijua kuwa wewe ni mtu makini kume tumekosea. Nadhani hata wanaokutumikisha wanajua kuwa wewe si makini na ndio maana wanakuwekea spidi gavana na kukuambia uache ubabe. Mwanzoni nilidhani wamekuonea kumbe walikuwa sahihi. Upo kama roboti. Nimegundua hili kutokana na matamshi na kauli zako. Barabara zote nchini unazijua wewe. Vifungu vyote vya sheria umevikariri wewe. Hizo sheria ni kwa ajili ya binadamu lakini wao/sisi sio programmed kama wewe.
Juzi hapa mkizindua barabara pale Dodoma, Pinda alikupiga dongo kuwa Rais alikupeleka uvuvi, na kule unajua idadi ya samaki nchini. Rais akaona bora akurudishe ujenzi. Tatizo lako mkuu unamtumikia kafiri kupitiliza, hadi unampa kero.
Wewe ni mchapakazi sawa, lakini yawezekana huna maadili ya kazi. Hakuna mtanzania anayekuwazia urais. Wanakuwazia uwaziri tu kwa kuwa watanzania wanajua unajua kutumika.
Achana kabisa na siasa zako za maji taka. Sio kila unapotoa neno hadharani usifie chama chako na kuponda upinzani. Kwa taarifa yako, unaowahutubia ni wapinzani. Sasa unapoponda viongozi wao na harakati za upinzani, wanakuchukia kweli. Wanakuoanisha na majina yako.
Tatizo lako mkuu unatupa mawe hovyo kiasi cha kuwatwanga na wazazi wako pia. Nakufananisha na Abunuwasi kukata tawi ulilokalia. Hilo tawi ni wananchi. Mpita njia akikuambia kuwa unafanya kosa kwani utaanguka, unamkejeli. Utakapoanguka utamkimbilia aliyekuambia ukweli kumwomba utabiri zaidi, angalia asijekwambia utakufa lini.
Achana na upinzani kwani ni jeshi kubwa kwa sasa. Una kashfa nyingi tu tunazozifahamu na nyingine zitafahamika. Una kashfa ya kuuza nyumba za serikali. Una kashfa za kumpa kimada wako nyumba ya serikali. Una kashfa ya kunyanyasa staff wako kwa kuletewa majungu na wapambe wako. Una kashfa ya ubabe, n.k, n.k. Fanya kazi, kiongozi kwani huijui kesho. Kazi ya kubwabwaja mwachue nape. Kaajiriwa kwa kazi hiyo. We kazi yako miundombinu. Usiwe kama mzazi anayewapa wanae mahitaji kwa masimango. Wenzako umeshwasikia wanabwabwaja hovyo? Time will tell
acheni ushabiki wa kijinga huo,mtu akiponda chadema tu mnamchukia na kumuundia zengwe....mbona ninyi huwa mnaponda magamba lakini hakuna mtu anayewaona kama ni hopeless
Read my signature..... kesho semeni tena mwakyembe na sita ni wazalendo... tatizo mnajua mno!!!