John Pombe Magufuli unatuchefua

Kumbe shida ni upinzani tu? kaa ndio hamna ishu hapa..Ishu ni kwamba hii njemba ndio iliyosimamia uuzwaji wa nyumba za serikali.. yaani mafisi wanagawana mali za baba kabla hajafa, tena kwa bei ya kutupa (ya jioni )..Cha ajabu kuna wadanganyika wanadhani this kafiri inaweza kuvaa viatu vya urais..same goes to Mamvi..hii nchi imelaaniwa.
 

ishu hapa ni upinzani pamoja na utandaji wake. Aache kuhusisha maendeleo ya nchi hii na ilani ya chama chake. Maendeleo ya nchi yanatokana katiba nzuri pamoja na sera nzuri za kitaifa. Sera nzuri zinatengenezwa na raia wenye itikadi tofauti. Tatizo la ccm ni kuhodhi dhana ya maendeleo kupitia chama. Na watu kama magufuli ndio wanaokomalia hili. Hata cdm wakishika madaraka na wakaendeleza huu upuuzi wa chama kushika hatamu, tutawasema
 
2008 mita 22.5, 2010 mita 30, 2014 mita 37.5, 2017 mita ....... Hapo kuna nyumba itakayobaki? Magufuli jitahidi kwenda kistarabu sio kila ukijisikia tu unaongeza upana wa barabara unawapa presure wazee wetu wasio na ajira.
 
Ni kweli anachapa kazi lakini naye amezidi kuropoka na kupenda misifa.

Bora anayechapa kazi zikaonekana, anaropoka na kupenda sifa kuliko yule asiyefanya lolote. Hebu jiulizeni, Chenge na Kawambwa walifanya nini kwenye wizara hiyo? Ni wakati ule wa Chenge ndio kulitokea msongamano mkubwa wa magari yalipokwamna kule Singida. Waht did he do? Sasa sana aliwaponda Watanzania na ushamba wetu wa kushabikia vijisenti!

Au bora Bwana umeme/mafuta Ngereja asiyesema lolote lakini makali yake Watanzania wa ngazi zote tunaya feel? yeye sio mropokaji. This is true!

I am not sure if we are becoming fair to Dr. John Pombe Magufuli. Among the ministers, nani ni bora? nani mwenye nafuu? probably, mkiangalia sana, mtarudi kwa Magufuli.

Just thinking aloud.
 
2008 mita 22.5, 2010 mita 30, 2014 mita 37.5, 2017 mita ....... Hapo kuna nyumba itakayobaki? Magufuli jitahidi kwenda kistarabu sio kila ukijisikia tu unaongeza upana wa barabara unawapa presure wazee wetu wasio na ajira.

This is good observation and advise to him....
 

Very fair comment but people wil not want it!
 
Natamani angesome hizi comment zako kwa kweli.

Ni kweli ni mchapakazi nadhani angekazana kuhakikisha miundombinu iko safi badala ya kuanza kuponda. Atuachie wananchi tuamue

Kwani anachokisema magufuli ni uongo? Kwamba ili tuandamane, tunahitaji kuandamana katika bara bara nzuri on which we can andamana?
 
Magufuli ana mdomo mchafu sana na jimbo kwake hakubaliki
 

tatizo la magufuli ni masimango na kuropoka na kujikomba. Akibadili hayo hakuna mwenye shida nae. Anakuwa kama inzi!
 
Kweli Naamini mtendaji mkuu alikuwa Mkapa na si Vinginevyo mbona kwa sasa Maghufuli anahaha na hafanyi lolote. Barabara zinaendelea kuifirisi nchi kama samaki wake
 
Watu husemaga kuwa MAJINA YANA ROHO.

John POMBE Magufuli. Kama mtu mwenyewe anaitwa POMBE ni lazima awe na tabia za POMBE POMBE hivi! Kwa maana nyingine angeweza kuitwa hata Chapombe. Mtu akisha lewa pombe lazima afanye vitendo vya kilevi. Vurugu,kelele,matusi na kubwabwaja kwingi.

Hakika John Pombe Magufuli hana tofauti na MLEVI yeyote. Maneno yake,vitendo vyake na akili yake yote ni sawa tu na mlevi yeyote. CCM wanamtumia kama VUVUZELA kwa ajili ya kampeni zao za kibabe. Mfano mzuri ni ule wa kule Igunga ambapo wakti wa kampeni alienda kule kutoa ahadi ya kujenga daraja ambalo tangu Uhuru miaka 50 iliyopita halijawahi kujengwa.

Sina hakika kama ujenzi huo ulishaanza au ilikuwa ni gea ya kuchukua jimbo la Igunga kwa udanganyifu na rushwa.
 
Tatizo la wachangiaji wengi ni jazba isiyo kifani kiasi cha kukosa hoja. Magufuli ni CCM tusitegemee hata siku moja akasifia CDM. Akiponda CDM yuko sahihi maana ndio kazi yake kama mwanachama wa CCM. CDM msitake kupokea sifa tu, hizi ni dalili za udikteta. Inaelekea mkipewa madaraka makubwa rangi yenu itaonekana zaidi.
 

He is too much, which of course is harmful. Mwambie kwanza Magufuli aache jazba, mipasho na ubabe ndio uje kwingine. Newto's 3rd law of motion applies here
 
Nadhani kama ana Busara Bora watu wake wa karibu wamwambie asome hii topic ili aweze Kujirekebisha kwani anabwabwaja hata mambo yasiyomuhusu!! Kuhusu Hasara alizosababisha kwa Taifa ni Nyingi!! Kwanza ni ile ya samaki wa Magufuli!! Samaki Hawa walitunzwa pale Mwenge Kwenye Kiwanda cha Bahari sea foods Kwa Garama ya zaidi ya Bilioni 1.6, Hizi ni hela nyingi ambazo zingeweza kutukwamua kwenye Matatizo tuliyonayo kama Taifa!! Nyingine ni hasara iliyopatikana pale Mwanza baada ya kuvunja petrol station kwa Jazba!! Pale imelipwa fidia ya zaidi ya 3.2 billions!! Zipo hasara Nyingi ambazo hatuzioni Kabisa!! ila kasabisha huyu mweshimiwa!! Tunamuomba awe na ustaarabu zaidi!!
 

Read my signature..... kesho semeni tena mwakyembe na sita ni wazalendo... tatizo mnajua mno!!!
 
acheni ushabiki wa kijinga huo,mtu akiponda chadema tu mnamchukia na kumuundia zengwe....mbona ninyi huwa mnaponda magamba lakini hakuna mtu anayewaona kama ni hopeless

Unakameruniwa nini? kwa hiyo unaunga mkono siasa za maji taka sio?huo ndio unafiki wa sisiemu mwenzenu akikosea, mnampongeza badala ya kumkosoa,punguza unafiki wewe.
 
Read my signature..... kesho semeni tena mwakyembe na sita ni wazalendo... tatizo mnajua mno!!!

nimekusoma ndugu. Hakuna msafi mle. Mfumo umewaharibu sana. Katika siku za mwisho mwisho za uhai wake, Nyerere alikuwa akikiponda waziwazi hiki chama.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…