Mbunge wa Ubungo John Mnyika anajenga hoja Bungeni kuwa idadi ya wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka nje ya wabunge/wawakilishi iongezwe kufikia 290 kwa kuwa wale wabunge/wawakilishi wa vyama waliopo sasa wanatokana na vyama vya siasa. Tumjulishe tu mbunge kuwa wabunge wanagombea ubunge kwa tiketi za vyama lakini hawachaguliwi na wanachama wa vyama vya siasa pekee, wanachaguliwa na wanachama na wasio wanachama wa vyama vya siasa! Of course, finally lengo la upande wako linafahamika kuwa ni kutafuta namna ya kuiwezesha hoja ya serikali tatu kwa njia ya ujanja-ujanja. Wasiwasi wangu ni kuwa hata katika hao 290 anaowapigia debe yawezekana wengi wao wakawa na msimamo tofauti na ule anaodhani Mnyika na upande wake!! Eventually, wingi wa wajumbe wa Bunge la Katiba wasiotokana na vyama vya siasa inaweza kukosa mashiko na ikawa ni ufujaji wa fedha za walipa kodi tu!!!