John Mnyika awaaga wana Kibamba

John Mnyika awaaga wana Kibamba

iron finger

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
358
Reaction score
221
Mgombea ubunge wa jimbo la Kibamba kupitia CHADEMA Mnyika Leo amewaaga wapiga kura wa jimbo la kibamba kutokana na ombi la mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe kuwataka wana kibamba wamruhusu mbunge wao mtarajiwa aende mikoani kwa ajili ya kuongeza nguvu katika majimbo yote ya ukawa na pia kujazia kura za urais.

Ombi hilo la Mbowe lilikubaliwa kwa sauti kubwa ya ndio na maelfu ya wapiga kura wa kibamba huku wakisema kwamba jimboni hapo mh Mnyika hana haja ya kupiga kampeni kwani tayari ni mbunge anayesubiri kuapishwa.

Kuanzia kesho Mnyika atajiunga na kundi lingine la wabunge machachari kina Lissu, Mdee,Lema, Kafulila na wengineo katika kampeni kali ya kutafuta kura za ukawa majimbo yote Tanzania

Amzungumzia Dr. Slaa

Mnyika alimfananisha mchumba wa aliyekuwa mke wa katibu mkuu wa Chadema Dr Slaa bi Josephine kuwa ni kama Delila aliyetumia ulaghai kumpotosha Samson.

Mnyika alisema kwamba adui wa Mabadiliko sio mtu toka ndani ya CCM ila ni mfumo wa CCM mzima na yeyote atakayesapoti mfumo wa CCM ni adui wa mabadiliko.
 
Hivi naweza kumpigia kura ,,, maana namkubali sn niko mkoani
 
Mnyika atajibu hoja za ufisadi hivi karibuni
 
safi sana Mnyika shambulieni kotekote tunataka ushindi wa saa5 asubuhi kura ziwe zimefika 14M
 
Mnyika SONGA MBELE, Mungu atakulipa kwa kazi kubwa unayoifanya kwa Taifa hili!
 
Mnyika ni mkombozi wa taifa,Be blessed brother tupo pamoja
 
Sasa sikilizeni mziki wa akina Mnyika Lissu, Kafulila! Aaaah! Ni shidaa!
 
Back
Top Bottom