NAGAMAHONGA
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 12,322
- 10,914
Sawa sawa kabisa na ndani yake ilipatikana makala ya stanslaus katabalo ikihusu loliondo.akiita loliondo-gate.wapo wengi tu kuna emmanuely kibiki yo man.Namkumbuka George Mwakingili. Kama sijakosea alikuwa akimtumia mpelelezi aliyeitwa Jim Mtemvu ilikuwa ni kama Joram Kiango alivyotumiwa na Ben R. Mtobwa au Willy Gamba wa Elvis Musiba.
Gazeti la Motomoto pia nalikumbuka. Jina "Motomoto" lilikuwa na maandishi mekundu kama lilivyokuwa gazeti la Shaba.
Sawa sawa kabisa na ndani yake ilipatikana makala ya stanslaus katabalo ikihusu loliondo.akiita loliondo-gate.wapo wengi tu kuna emmanuely kibiki yo man.
hivi hadithi ya panga la shaba alichora nani? marco tibasima wapi b.mkora, mmenikumbusha mbali sana
Mkuu asante kwa taarifa!Mtuhumiwa kwangu mimi ni riwaya ya pili kwa ukali kutoka kwa Tuwa ikitanguliwa na Mkimbizi.
Nilicheki na Tuwa na kumueleza juu ya kuiweka Mtuhumiwa katika kitabu,kipindi hicho ndio alikua anaandaa riwaya yake ya UTATA lakini aliahidi ataifanyia kazi ishu.
Msachi tu kwenye facebook,chapa Husein Tuwa na mambo yataenda...you know wha i'm sayin'!!!?
Nadhani huyu ndo mchoraji wa ile hadithi ya "anga za wenyewe", mtanisaidia mnaokumbuka vizuri.
Hakuna kama John Kaduma. Hata waliomtangulia akina Philip Ndunguru (Mchoraji wa mwanzo kabisa wa Sani) hawakuwa na uwezo kama wake. Never. Akina madenge wa siku hizi wabaaaaya.
BTW, nafanyia kazi namna ya kurudisha nguvu za akina madenge, lodilofa etc kwa kizazi cha sasa na cha miaka ya 80 kwa njia inayosisimua zaidi. Likely kuanzia mwaka 2016 naweza kuwa katika hatua muafaka. "Niko kambini najifua." Tuombe uzima.
RIP John Kaduma.
Hivi huyu ndugu aliwahi kubadili jina na kuitwa "Mohammed Hussein"?
Kazi nyingine ninazozikumbuka za huyu gwiji john m kaduma ni ile ya MZUNGU WA UNGA (pablo zungu) ilikuwa inazungumzia masuala ya madawa ya kulevya katika jarida la KIU,
hata hivyo jarida hilo lilifutwa muda mfupi kwa sababu zisizojulikana.
Majarida mengine yaliyotamba enzi hizo ni pamoja na AMBHA na KINGO (james gayo wa kenya).
daah kaka ume nikumbusha hii kitu pablo zungu aisee!! ilikua kwenye jarida la Tabasamu toleo la kwanza na hadithi ikaanza!
r.i.p john kaduma he inspired me to be a good artist especially kwenye uchoraji maskini kipaji changu hakija nifikisha popote mfumo wa elimu ya bongo shida sana inaua vipaji sana,shuleni wame nitumia sana kuchora vitu mbali mbali.
Aisee niko serious sana. Kila siku, namaanisha kila siku, nawaza ama kufanya kitu fulani juu ya hili. Inawezekana ndani ya wiki moja na nusu ijayo nikawa na mazungumzo na wakubwa wa Sani. Implementation yake huenda ikachukua muda kidogo ila ningependa iwe nzuri kwa kadri ya uwezo wangu wote. Nachokusudia kufanya ni animation (3D). Kila siku ni lazima niwashe kompyuta yangu... kila siku. Asilimia 60 ya nayofanya katika kompyuta yanahusiana na haya. Hata hivyo animation nzuri ni extremely challenging ila nimeweka nguvu kubwa kwelikweli, amini hivyo. Najizuia nisiseme mengi.
Sina contacts za Tuwa ila naweza kufuatilia na nikizipata ntakucheki. Tuombeane uzima.
Namkumbuka George Mwakingili. Kama sijakosea alikuwa akimtumia mpelelezi aliyeitwa Jim Mtemvu ilikuwa ni kama Joram Kiango alivyotumiwa na Ben R. Mtobwa au Willy Gamba wa Elvis Musiba.
Gazeti la Motomoto pia nalikumbuka. Jina "Motomoto" lilikuwa na maandishi mekundu kama lilivyokuwa gazeti la Shaba.
Kuna mtu mwingine wa riwaya akiitwa george mwakingili na hadithi ya kinywa cha mauti gazeti motomoto.