Job Ndugai kuvuliwa Uspika wa Bunge?

Job Ndugai kuvuliwa Uspika wa Bunge?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
141,453
Reaction score
283,788
Kwa kipindi cha miaka zaidi ya mitano , kile kilichoitwa kipindi cha awamu ya 5, Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai aliuwa kinyama Mhimili wa Bunge na kuufanya sehemu ya Serikali ile, Ndugai alikuwa anahudhuria hata uzinduzi wa vyoo vya shule, stendi na masoko, tena vile vilivyofadhiliwa na wazungu baada ya serikali ya Tanzania kushindwa kuvijenga, hata hivyo hakuwahi kufungua mdomo wake kukemea mambo hayo, hii ni kwa sababu mzinduaji alikuwa boss wake.

Leo kwasababu zisizofahamika Ndugai yuleyule anajifanya ni mwenye huruma na Nchi kwa kumpiga Spana Kiongozi wake na kumtahadharisha kuhusu deni la Taifa !

Ni kweli kwamba ukopaji usio na tija ndio umetufikisha hadi mahali ambako Dunia imetuweka kwenye kundi la nchi vimeo ambazo soon zitakuwa hazikopesheki, bali msemaji wa Jambo hili hakupaswa kuwa Job Ndugai, huyu alishabikia kila uchafu wakati wa awamu ile ikiwemo ukopaji ambao matumizi ya hela hizo ilikuwa Mwiko kujadiliwa kwenye bunge lake, leo kuna nini hadi Ndugai awe upande wa Wananchi?

Je, kwa kauli zake hizo mpya tumuweke kwenye yale makundi ya mnyukano ndani ya CCM , na yeye yuko Team Mwendazake, na JE ATAENDELEA KUVUMILIWA KWENYE CHEO CHAKE?

62B393F2-8A7A-43B5-B107-B456A751062C.jpeg
 
Ni kweli kwamba ukopaji usio na tija ndio umetufikisha hadi mahali ambako Dunia imetuweka kwenye kundi la nchi vimeo ambazo soon zitakuwa hazikopesheki , Bali msemaji wa Jambo hili hakupaswa kuwa Job Ndugai, huyu alishabikia kila uchafu wakati wa awamu ile ikiwemo ukopaji ambao matumizi ya hela hizo ilikuwa Mwiko kujadiliwa kwenye bunge lake , leo kuna nini hadi Ndugai awe upande wa Wananchi
 
Ndugai hakumaanisha serikali isikope,alikua anatolea ufafanuzi kwanini tozo zilikubaliwa bungeni,na kwa jinsi ilivyo bila tozo na mikopo unadhani hali ingekuaje.
Tozo zinapunguza ukali wa mikopo,bila tozo kila kitu kingekua kinafanyika kwa mikopo
Kama alimaanisha hivyo ulivyoandika wewe, basi aitishe tena mkutano afafanue maana nadhani hakueleweka.
 
Ni kweli kwamba ukopaji usio na tija ndio umetufikisha hadi mahali ambako Dunia imetuweka kwenye kundi la nchi vimeo ambazo soon zitakuwa hazikopesheki , Bali msemaji wa Jambo hili hakupaswa kuwa Job Ndugai , huyu alishabikia kila uchafu wakati wa awamu ile ikiwemo ukopaji ambao matumizi ya hela hizo ilikuwa Mwiko kujadiliwa kwenye bunge lake , leo kuna nini hadi Ndugai awe upande wa Wananchi
Mliambiwa usipokuwa na upinzani wa nje, mtakuwa na upinzani wa ndani. Sasa mtaelewa
 
Ni kweli kwamba ukopaji usio na tija ndio umetufikisha hadi mahali ambako Dunia imetuweka kwenye kundi la nchi vimeo ambazo soon zitakuwa hazikopesheki , Bali msemaji wa Jambo hili hakupaswa kuwa Job Ndugai , huyu alishabikia kila uchafu wakati wa awamu ile ikiwemo ukopaji ambao matumizi ya hela hizo ilikuwa Mwiko kujadiliwa kwenye bunge lake , leo kuna nini hadi Ndugai awe upande wa Wananchi
Hivi matibabu yake kule ni kweli iligota b26
Au watu waliongeza chumvi

Ova
 
Kwa kipindi cha miaka zaidi ya mitano , kile kilichoitwa kipindi cha awamu ya 5 , Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai aliuwa kinyama Mhimili wa Bunge na kuufanya sehemu ya Serikali ile , Ndugai alikuwa anahudhuria hata uzinduzi wa vyoo vya shule , stendi na masoko , tena vile vilivyofadhiliwa na wazungu baada ya serikali ya Tanzania kushindwa kuvijenga , hata hivyo hakuwahi kufungua mdomo wake kukemea mambo hayo , hii ni kwa sababu mzinduaji alikuwa boss wake .

Leo kwasababu zisizofahamika Ndugai yuleyule anajifanya ni mwenye huruma na Nchi kwa kumpiga Spana Kiongozi wake na kumtahadharisha kuhusu deni la Taifa !

Ni kweli kwamba ukopaji usio na tija ndio umetufikisha hadi mahali ambako Dunia imetuweka kwenye kundi la nchi vimeo ambazo soon zitakuwa hazikopesheki , Bali msemaji wa Jambo hili hakupaswa kuwa Job Ndugai , huyu alishabikia kila uchafu wakati wa awamu ile ikiwemo ukopaji ambao matumizi ya hela hizo ilikuwa Mwiko kujadiliwa kwenye bunge lake , leo kuna nini hadi Ndugai awe upande wa Wananchi ?

Je kwa kauli zake hizo mpya tumuweke kwenye yale makundi ya mnyukano ndani ya ccm , na yeye yuko Team Mwendazake , na JE ATAENDELEA KUVUMILIWA KWENYE CHEO CHAKE ?

View attachment 2060532View attachment 2060533
Nchi imegawanyika Mihimili imekosana

Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Ndugai hakumaanisha serikali isikope,alikua anatolea ufafanuzi kwanini tozo zilikubaliwa bungeni,na kwa jinsi ilivyo bila tozo na mikopo unadhani hali ingekuaje.
Tozo zinapunguza ukali wa mikopo,bila tozo kila kitu kingekua kinafanyika kwa mikopo
Ndo nilivoelewa pia nilipoona video yake.
 
Tunajua wachawi wa Ndugai wako Chadema huko ndani ya BAWACHA.

Sasa mnahangaika kuzalisha mgogoro ndani ya CCM ili mnufaike.

Uzuri ni kwamba CCM wanawapotezea na vipost chonganishi vyenu toka vijiweni mnakouguza majeraha ya kukosa ubunge.
 
Samia kawa mkweli
Hapana mtetezi wa covid19 ndio mkweli.
Ndugai anaonyesha uchungu kwa nini mama maushungi alimuingiza kenge akubali kupitisha tozo za miamala ya simu ili zitumike kujenga madarasa na vituo vya afya.
Sasa anacholaumu subwoofer ni kwanini maushungi amekwenda kukopa fedha za kovid kwa ajili ya kujenga hayohayo madarasa? Mkopo ambao utalipwa na riba
Subwoofer anahisi amesnitchiwa kwa wananchi kwa kuwabebesha mzigo wa tozo.
Kama vipi basi tozo zifutwe si tunasikia majisisiem inavyojisifia kwamba haijawahi kutokea madarasa yamejengwa ya kutosha
 
Back
Top Bottom