RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa Serikali inakamilisha mipango ya kuanzisha upya utaratibu wa vijana kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria kama ilivyokuwa zamani.
Pia alisema kuwa Tanzania iko tayari kutoa uzoefu wake wa jinsi ya kuendesha Jeshi la Kujenga Taifa kwa Zimbabwe ambayo nayo inaangalia jinsi ya kuanzisha jeshi kama hilo kwa ajili ya vijana.
Rais Kikwete alisema hayo juzi Ikulu, Dar es Salaam alipofanya mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Zimbabwe, Jenerali Costantine G. Chiwenga ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi Tanzania.
Katika mazungumzo hayo, Jenerali Chiwenga alimweleza Rais Kikwete kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi ya Zimbabwe ikiwa ni pamoja na mchakato wa maandalizi ya katiba mpya ya nchi hiyo ambayo inafungua mlango wa kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwingine nchini humo.
Jenerali Chiwenga ambaye alifuatana na mwenyeji wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, pia alitumia mazungumzo hayo na Rais Kikwete kuishukuru tena Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika mapambano ya ukombozi wa Zimbabwe. Tuko nanyi.
Tanzania iko na wananchi wa Zimbabwe. Huu ni uhusiano wa kihistoria ulioanzia kwenye makambi ya wapigania Uhuru ya Kongwa na Nachingwea hadi kwenye misitu ya Mozambique mpaka ndani ya Zimbabwe yenyewe, alisema.
Pia alisema kuwa Tanzania iko tayari kutoa uzoefu wake wa jinsi ya kuendesha Jeshi la Kujenga Taifa kwa Zimbabwe ambayo nayo inaangalia jinsi ya kuanzisha jeshi kama hilo kwa ajili ya vijana.
Rais Kikwete alisema hayo juzi Ikulu, Dar es Salaam alipofanya mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Zimbabwe, Jenerali Costantine G. Chiwenga ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi Tanzania.
Katika mazungumzo hayo, Jenerali Chiwenga alimweleza Rais Kikwete kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi ya Zimbabwe ikiwa ni pamoja na mchakato wa maandalizi ya katiba mpya ya nchi hiyo ambayo inafungua mlango wa kufanyika kwa uchaguzi mkuu mwingine nchini humo.
Jenerali Chiwenga ambaye alifuatana na mwenyeji wake Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, pia alitumia mazungumzo hayo na Rais Kikwete kuishukuru tena Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika mapambano ya ukombozi wa Zimbabwe. Tuko nanyi.
Tanzania iko na wananchi wa Zimbabwe. Huu ni uhusiano wa kihistoria ulioanzia kwenye makambi ya wapigania Uhuru ya Kongwa na Nachingwea hadi kwenye misitu ya Mozambique mpaka ndani ya Zimbabwe yenyewe, alisema.