JK, Shein waula

JK, Shein waula

Kama waliingia madarakani kwa katiba ya zamani,bc watatoka kwa kufuata katiba hiyo ya zamani ambayo inasema kuwa uchaguzi utafanyika kila baada ya miaka mitano (5).Lazima watoke 2015,
Hoja yako ni kweli! Lakini kumbuka kuwa tutakuwa na kura ya maoni mwakani na kama rasimu hii ya katiba itakubaliwa, katika uchaguzi mkuu ujao tutahitajika kuchagua rais wa muungano na rais wa Tanganyika!

Bahati mbaya hatuna katiba ya Tanganyika hivyo tutalazimika kuanza mchakato wa katiba hiyo! Kutokana na uzoefu wa kuandaa rasimu hii ya katiba ya muungano ni wazi muda wa kuandaa katiba ya Tanganyika hautapungua miaka miwili! Na katika muda huo na ili kufanikisha kuandikwa kwa katiba ya Tanganyika, Bunge litalazimika kutunga sheria ya kuongeza muda wa uongozi wa serikali iliyopo madarakani!
 
Sasa ni dhahiri endapo rasimu ya katiba mpya itapitishwa katika kura za maoni basi ni wazi kuwa JK na Shein wataendelea kukalia viti vyao si chini ya miaka miwili zaidi ili kuwezesha Watanganyika kuandaa katiba yao na Wazanzibari kurekebisha katiba yao ili iendane na katiba mpya!

Hivyo nawashauri Watanzania wenzangu tujiandae kisaikolojia kukabiliana na hali hiyo!

Mungu ibariki Tanzania!
Mungu ibariki Tanganyika!
Mungu ibariki Zanzibar!
...hili umefikiri awewe au limetoka ndani ya rasimu ya katiba???maana hata mi najiuliza sioni time frame na mechanism ya kufanyia kazi uwepo wa katiba ya TZ bara..pia bunge na serikali....sioni rasimu inasemaje kuhusu muda wa kuyafanya haya mambo kabla kabla ya uchaguzi mkuu....
 
Sasa ni dhahiri endapo rasimu ya katiba mpya itapitishwa katika kura za maoni basi ni wazi kuwa JK na Shein wataendelea kukalia viti vyao si chini ya miaka miwili zaidi ili kuwezesha Watanganyika kuandaa katiba yao na Wazanzibari kurekebisha katiba yao ili iendane na katiba mpya!

Hivyo nawashauri Watanzania wenzangu tujiandae kisaikolojia kukabiliana na hali hiyo!

Mungu ibariki Tanzania!
Mungu ibariki Tanganyika!
Mungu ibariki Zanzibar!

Muda wa Jakaya ufikia mwisho he will just have to leave the office and relinguish the presidency at least to Madam Speaker. We can not afford further his expensive and useless trips abroad.
 
Hizi kauli za 'Kuula' 'Waula' ni kauli zinazochochea wizi na matumizi mabaya ya public office.Tubadili mentality hii...!

kuna watu hawafikirii sawasawa humu, wanashindwa kuelewa kuwa kupewa madaraka ni jukumu zito wanakuwa na mawazo mepesi eti flani aula, hii haikubaliki
 
Muda wa Jakaya ufikia mwisho he will just have to leave the office and relinguish the presidency at least to Madam Speaker. We can not afford further his expensive and useless trips abroad.

umeenda opp, hapa tunajadili katiba ya nchi na uongozi wa muda, sio safari za rais.
 
Itabidi iwe katiba moja yenye sehemu tatu, moja kwa kila serikali. Kwa hivyo basi, akina Warioba watapashwa kupendekeza katiba yenye sehemu zote tatu. Maoni waliyokusanya yatatosheleza kwa kazi hiyo.

Ni kosa kudhani kutahitajika kusubiri kutengeneza katiba ya serikali ya Tanganyika.

Nchi moja haiwezi kuendeshwa kwa katiba tatu ambazo hazitegemeani. Inaweza kuendeshwa kwa katiba moja yenye sehemu tatu.

Warioba na kamati yake waje na utatu wa katiba, na si vinginevyo. Katiba moja, serikali tatu. Sasa.
 
Jk ataendelea kuwa ruru na anayeumwa ni kumwacha aumwe tu wala hatachafua sifa ya jk,twende jk tunaimani na wewe.

Wewe acha hizo,hapa inabid iundwe serikal ya mpito,yaani JK anavyotuburuza namna hiyo bado mnataman aendelee kututawala! Heeeh!
 
Sasa ni dhahiri endapo rasimu ya katiba mpya itapitishwa katika kura za maoni basi ni wazi kuwa JK na Shein wataendelea kukalia viti vyao si chini ya miaka miwili zaidi ili kuwezesha Watanganyika kuandaa katiba yao na Wazanzibari kurekebisha katiba yao ili iendane na katiba mpya!

Hivyo nawashauri Watanzania wenzangu tujiandae kisaikolojia kukabiliana na hali hiyo!

Mungu ibariki Tanzania!
Mungu ibariki Tanganyika!
Mungu ibariki Zanzibar!

Hivi Tanganyika AKA Tanzania bara haina katiba sio! Maana hapa tunatoa muda kwa katiba ya JMT na ZNZ tu! Kweli Tanganyika wana TANGA TANGA NA NYIKA!
 
Katiba ya muungano lazima iseme kila serikali kwenye huo muungano itakuwaje.

Katiba ya nchi itakuwa na vipengele vya serikali zote, kuanzia za mitaa, hadi za Tanganyika na Zanzibar, na kuainisha jinsi serikali zote hizo zitakavyokuwa sehemu ya serikali ya muungano.
 
Sio wao peke yao!ni wao na serikali yao sio?!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Hivi Tanganyika AKA Tanzania bara haina katiba sio! Maana hapa tunatoa muda kwa katiba ya JMT na ZNZ tu! Kweli Tanganyika wana TANGA TANGA NA NYIKA!
​Chikawe amesema inawezekana tukawa na katiba ya Tanganyika kabla ya 2015! Lakini kwa utaratibu huu wa kusuasua I doubt!
 
Ila mbona Watanzania twapenda kulalamika sasa? Tulitaka katiba mpya sasa inaelekea kupatikana bado tuna lalamikia hili. Nyie mnadhani kuswitch toka katiba moja kwenda katiba nyingine ni kitu rahisi? Chukulieni mfano hata Kenya ambapo raisi Kibaki aliishia kubaki madarakani miezi kadhaa ya ziada. Tulitaka katiba mpya let's make the sacrifices.
 
Jk ataendelea kuwa ruru na anayeumwa ni kumwacha aumwe tu wala hatachafua sifa ya jk,twende jk tunaimani na wewe.
Hahaha kule kwetu hilo jina lako nimtu ambaye hajawahi kutoa wazo lolote la maana, au mvivu wakazi na hata kufikiri, nimeliona nikacheka sana.
 
Back
Top Bottom