Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,866
Nimeyatazama haya maneno ya EL na ule ujumbe toka "msoga" kisha nimetambua kuwa JK anacheza mchezo wa hatari sana.
Mbali na kumuomba atangaze nia, masheikh hao pia walimsomea dua ya kumtakia heri katika harakati hizo.
Nyie ni special (maalum), mnatoka Bagamoyo na inajulikana kwa historia na ni nyumbani kwa Rais (Jakaya Kikwete). Namimi nimepata baraka zake na nyie mmemuwakilisha, alisema Lowassa.
Tumetoka naye mbali sana, lakini Mwenyezi Mungu akinijalia nitaanzia pale alikomalizia. Amefanya kazi kubwa na ya heshima kwa kweli. Kwa hiyo kitendo cha kutoka nyumbani kwenu kuja kuniona kwa kweli kimenipa nguvu kwamba wenzangu wa Bagamoyo wako pamoja na mimi.
Alisema anaheshimu sana maneno waliyomwambia masheikh hao na anayakubali.
Lowassa pia alimsifia Rais Kikwete kwa kufanya mambo makubwa nchini na kwamba kati ya maeneo aliyoshughulika nayo sana ni elimu.