Jk: Njia panda

Anayo timu kubwa ya kumshauri pale Jengo jeupe Magogoni Waongeze kasi ya kumpa mwelekeo na mikakati ya haraka ya kurekebisha hali ya mambo. Bado anayo miaka mitatu iliyobaki TUVUKE SALAMA !!!!!
 
anao washauri wa kutosha pale white house magogoni. Waongeze kasi ya kumpa mwelekeo wa maamuzi ya haraka ili tuvuke salama. Bado ni rais wetu anayo miaka mitatu imebaki
 
Jamani tunafanya masihakhara wakati ngoma ya mdumange imeshaanza kupaswa huko. Serikali chode usikae kimya - labda JK aanze na hili la mgomo kwanza.
 
ana ugonjwa sugu aina ya swahibatism umemwathiri na nafikiri utammaliza muda si mwingi.
 
............kitu kimoja..lack of power from within'' hili ndilo tatizo la huyu jamaa.......na ndio maanakila kitu kimemshinda.........
Watu waliwahi kusema Obama yupo chini ya white power (kakikudi ka wamarekani weupe) hivo yeye kama rais hana la kuamua, hiv mtindo huu ndo unatumika na hapa nyumbani eee!
 
Kikwete aanze kipi? Chama, Serikali, Bunge ama Madaktari?

Vijana wa mtaani wanasema “ameshikwa bapaya”. Bunge wanataka ongezeko la pesa - naona hilo anajaribu kutia mkazo hakusaini, lakini hawezi kusema hadharani. Madaktari wamegoma lakini alichelewa kuona mgomo huu utafika hapa ulipo kwahiyo hawezi kuingilia sasa. Waziri Mkuu anashutumiwa anambadilisha vipi maana kambadilisha Lowasa majuzi tu - na swala amuweke nani? ili afanye nini? Eti afanye reshuffle kwa nini? Lakini unamfukuzaje Waziri na Naibu wake tu? Wabunge wa CCM wanamtishia juu ya katiba na labda kutoridhishwa na maamuzi yake ya posho.

Jamani haya mambo sio mepesi, na tusitizame kama jambo moja moja maana ikitokea tu haya mambo yakaunganika - basi tumekwisha.

Nadhani kikwete anahitaji ushauri hapa! Aanzie wapi? Unaanzaje na mgomo wakati ndani kwako ni vuruvaru?

Upuuzi wake ndio umemfikisha hapo alipo, Akionekana hadharani apigwe mawe kwa kuwa anaua wenzetu huko hospitali
 
Nahisi washauri wake si wazuri, au ni yeye mwenyewe hashauriki!
Si vibaya akimuomba ushauri kwa maraisi wengine kisha akapima ushauri unaowiana, akichanganya na mawazo yake, tutafika tu!
 
nduguzangu jiulizeni swali dogo tu hili, kwanini kila linapotokea tatizo la mafuta wanareact haraka sana, mara EWURA wameitisha place comference, mara vituo vimefungwa, WHY HILI LA MADAKTARI WANALIFANYA HIVI. SIMPLE ANSWER AS FOLLOWS
KWENYE MAFUTA-WANAMASLAHI BINAFSI
KWENYE AFYA HAWANA MASLAHI - WATAKWENDA HATA ST. THOMAS KUTIBIWA.

NDUGUZANGU DALILI YA MVUA SIKU ZOTEE NI MAWINGU, HUWEZI KUFIKA 10 KAMA 1, 2... 9 HUJAZIVUKA.
 
Vyote vitawezekana kama akianza kuvunja mikataba yoote ya migodi. Kushindwa kwake ni kwa ajili yeye mwenyewe anahusika sana.
YOU CAN FOOL SOME PEOPLE SOMETIME BUT YOU CANNOT FOOL ALL THE PEOPLE ALL THE TIME
 
Kikwete anabahati sana. Katika haya yote watu wanachotaka ni yeye kuwawajibisha tu watu wengine! Hilo ni jambo jema atumie nafasi hiyo kabla haijabadilika. Nadhani, Raisi kashauriwa hili la mgomo na posho ni mambo madogo sana hapaswi kuyaongealea, zaidi aachie vyombo vingine vifanye kazi yake. Nikujulishe tu Raisi wangu, washauri wako wamekosea hawasomi alama za nyakati. Ushauri wangu, longa tu nawananchi watakusikiliza - usisubiri watu wawe mbogo. Uongozi ni wako, wengine ni washauri tu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom