Kutokana na maruweruwe ninayo yaoni imefikia mahali ninajiuliza hivi JK alipokuwa ana bid for presidential post alijua na kudhamiria kuwatumikia watanzania au alitaka tu kuwa Celebrity ndani ya Ikulu?
Napata shida ninapoona rais anashindwa kufanya very simple decisions na kutatua mambo madogo madogo. Hv kweli huyu rais anayeelewa matarajio watanzania waliokuwa nayo kwake? Kwa nini ashindwe ku deliver kwa kiasi kikubwa namna hii?. Kukosekana kwa majibu ya maswali haya bado kunanifanya niamini JK alitafuta urais kwa sababu zake binafsi tofauti na tulivyokuwa tunatarajia. Yeye haswa alichukulia akiwa rais atakuwa Celebrity wa kupungiwa mikono, kukaribishwa kwenye ufunguzi na matukio mbalimbali n.k.
Mimi naona ana act kana kwamba siyo rais anayetakiwa kuwajibika bali watu wamfagilie tu kwa kusema mara he is presentable and handsome.Most of time uwe unaonyesha uso wa tabasamu hata kama mji mzima wa AR uko msibani.
Tabia hii ra rais ya kutaka aonekana mbele za watu kuwa ni ok wakati ndani ana maumivu ya kukosa majibu ya DOWANS, EPA, msiba Arusha, mgawanyiko ndani ya Chama, katiba mpya na kushindwa majukumu ndo yananifanya nimwone kama amekaa mkao wa Celebrity wa kuchonga zaidi
Nasikitika mno
Ukiacha wizi unaofanywa na chama na wapiga kuru tulaumiwe....Haiwezekani tumejaa kwenye mikutano cha ya chadema na kumshangilia kwa nguvu dakitaree Silaha kumbe shahada za kupigia kura tumeshauza... hapo ndipo macelebrity wanapopata fursa ya kuuza sura...Nani alaumiwe jk au waliompigia kura?
Mzee umekuwa PILATO?Mchukueni muukumuni kwa hiyo sheria yenu