JK na tripu za mkoa wa kilimani-njaro

WA MAMNDENII

JF-Expert Member
Jun 5, 2010
344
57
jamani kwa kipindi kisichozidi mwezi mmoja jk katembelea mkoa wa kilimani mara mbili, nahisi ni mkakati wa ccm kuhakikisha majimbo yote ya ubunge kilimani yanaporwa hasa la Ndesapesa na baada kusikia tena Mbowe anaenda kuchukua jimbo lake la Hai ccm wamedata kabsaa, CHADEMA inabidi ijipange sawasawa naamini jimbo la moshi mjini na hai watayahodhi
 
moshi sio kama dar, hawadanganyiki

hata aweke kambi huku wiki nzima

slaa mjengoni anarud
 
Mimi ninasubiri kwa shauku kubwa kuona Watanzania tukianza kuona umuhimu wa mwelemeo wa uwiano wa nguvu za kisiasa (tilt in the balance of political power) katika kuwafanya wanasiasa wetu na vyama vyao watuthamini sisi binafsi na mahitaji yetu badala ya dharau na kebehi wanayotuonyesha sasa. Kinachotakiwa, kwa kuanzia, ni CCM kupunguziwa viti vya uwakilishi Bungeni na kwenye Halmashauri. HILO NI LAZIMA LIFANYIKE KAMA KWELI TUNAJIJALI. Kuwaongezea ni kosa lisilo na msamaha kabisa na, likitokea, basi Watanzania tuwe radhi kuendelea kudhalilishwa na utawala wa kibazazi usio na soni. Na hapo tusisumbuke kumnyooshea kidole mtu mmoja mmoja au CCM kama chama. Hata ingekuwa CHADEMA mnawapa asilimia 90 na kuwahakikishia uhai wa kisiasa usio na ukomo, wataendelea kuwala tu. Surely they are not your uncles.
 
Back
Top Bottom