Jk azidi kuandika historia


Kwa kweli kwa hayo mekundu JK amefanya uthubutu. Kama si uthubutu angeweza kuzuia kuundwa kwa kamati ya Bunge iliyo mfanya EL ajiuzulu. Katika nchi kama zetu hizi kuruhusu Waziri Mkuu/Rafiki yako asulubiwe kiasi kile huku wewe ukiwa na uwezo wa kuzuia ni uthubutu mkubwa huo. Kama si uthubutu wa Rais si PCCB walikuwa wamemtakasa EL?
 
Ndo wameku2ma useme ivo? Nan kakuambia kua jk ndo anaruhus maandamano? Ningempongeza kama watakaofungwa gerezan ni yona,mramba,chenge na magamba mengne bt co hao
 

Kutangulia kuzaliwa haina maana una uwezo mkubwa wa kutoa hoja! Mawazo yako ni yako, mawazo yangu ni yangu. Sote tuwe na uhuru wa kutoa mawazo na kusikiliza wengine.
 
Kwa kweli jambo la msingi apongezwe JK kwa UTHUBUTU, sote twaelewa kuna viongozi wamepita walishindwa kutumia nafasi zao ingawa sheria na kanuni zilikuwepo
 
Hawa CDM wangempata mkapa ndio watajua nini maana heshima, Kikwete anawaachia wafanye wanacho taka, lakini siku yenu itafika tu. Wote nyie CDM mnatakiwa kumsujudia KIKWETE na kumtambua kama ndio kiongozi wenu.
 
Hawa CDM wangempata mkapa ndio watajua nini maana heshima, Kikwete anawaachia wafanye wanacho taka, lakini siku yenu itafika tu. Wote nyie CDM mnatakiwa kumsujudia KIKWETE na kumtambua kama ndio kiongozi wenu.

sio kwamba wamsujudie Mungu, ina maana kikwete wewe huwa unamsujudia?!
 
sisi CCM tunamkubali kwa moyo wote na hatuhitaji kumsujudia, CDM ndio wamsujudie kwa sababu yeye ni mwokozi wao.
 

Hivi Bangi ni halali????? kwanini iweke wazi namna hii??????????
 
Tujikumbushe baadhi ya hatua ambazo JK amethubutu kuchukua katika uongozi wake:-
1. Kuvunja Baraza la Mawaziri ikiwa ni kujiuzulu kwa Waziri Mkuu-JE ILIKUWA HIYARI YAKE AU NI KUTOKANA NA NGUVU YA UMMA?
2. Kuwafikisha mahakamani viongozi wandamizi wa serikali; Mramba, Yona na Mgonja-ALILIANZISHA YEYE HILI AU ALIFUATA MKUMBO TU? MBONA KESI HAIISHI? MBONA ALIENDA KUMPIGIA KAMPENI MRAMBA NA AKABWAGWA CHINI?
3. Kuwapeleka watuhumiwa wa EPA mahakamani-MBONA HAJAIPELEKA KAGODA(40BN) AMEWAFUNGA HAO WA 1BN
4. Kuwa na moyo wa uvumilivu kwa vyombo vya habari-MOYO UPI? KUYAFUNGIA MWANAHALISI NA KULIKONI KWA KUSEMA UKWELI?
5. Kutoa vibali vya maandamano kwa vyama vya siasa pasiipo ukomo-UKOMO WA NINI TENA? KUANDAMANA NI HAKI YA KIKATIBA NA HAIHITAJI UTASHI WA JK
 
Nyie semeni yote mwisho Mtamkubali tu.
 
Una uhuru wa kutumia demokrasia utakavyo, UKWELI unabaki pale pale JK kapaisha demokrasia TZ na vyombo vya dola amewapa uhuru wa kutekeleza majukumu
yake

****** mbona yuko huru wakati na yeye ni mhusika wa wizi huo?
 

Usaniii!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…