JK awashangaa viongozi CCM kupenda anasa

Angalia alivyo na Mishituko akatangaza AZIMIO LA ARUSHA upya kudai watu wanapenda Anasa na kukumbuka TANU

Uongozi Umemshinda inabaki kukopa kopa Masuala Magumu yaliyopita ya Mwl. Nyerere

Haoni Chochote bora cha Mzee Ruksa zaidi ya kuvika Dhahabu wakeze
 
hana jipya mbaya zaidi kasema ngeleja na mhando hawana kosa tatizo ni maji, anyway mi nilisikia kwenye nukuu za magazeti ya jana, mwenye full story anijuze.

Huyo ndiye rais wetu, kiongozi na mtawala. Siku zote yeye ni kushangaa tu kila jambo sawa sawa na dereva aliyekaa kiti cha dereva na kushika usukani halafu anawauliza abiria jamani mbona hatuondoki?? Ni ajabu sana. Kama ngeleja na mhando hawana kosa basi hata maji ya kuendeshea mitambo ya umeme hayana kosa kwa vile yapo mengi tu. Kilichotakiwa ni ubunifu wa kuyapata hayo maji na kuyatumia yanapotakiwa. Kuna njia nyingi sana za kufanya ili sehemu ile yenye mitambo ambayo inahitaji maji isikaukiwe. Kinachotakiwa ni ubunifu tu. Kama anawasafisha hao ni dhahiri kwamba mwenye shida ni yeye mwenyewe na kwa ajili hiyo awajibike pamoja na serikali yake. Tumechoka kusikia pumba pumba pumba kila kukicha pumba pumba tu.
 
Kaa Nchini acha safari za Nje... Umesikia Mwai Kibaki akisafiri safiri kama wewe?
Kama tulikuwa pamoja Mkuu,hata mie nilitaka nihoji Safari zakwenda Kubembea Nje Ya Nchi(Majuu)zenyewe tuziiteje?
 
Mara TANU imekumbukwa tunasubiri ujamaa na Tanganyika sasa, Mtikila kaa mkao wa kula.
 
Kwa kuwa wameamua kuikumbuka TANU kwa mbwembwe,ni vema pia wakalikumbuka na kulirudisha azimio la Arusha!
 
Juzi, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilisheherekea miaka 57 ya kuzaliwa kwa TANU kwa mbwembwe na chereko. TANU ilimaliza muda wake wa kuishi baada ya kuungana na ASP mwaka 1977.

Hii inafanana na kufanya birthday ya marehemu mzazi wako! Kuna kituko kimoja kilifanyika Moshi cha mtu kufanya jubilei ya ndoa yake wakati mwenzi wake alishakufa miaka kumi iliyopita.

Ukitazama kwa makini inaonyesha kuwa CCM wameshaona kuwa hawana ushawishi wala haiba kwa wananchi na ikapelekea kukumbuka marehemu mzazi wake na kumfanyia birthday party ili walau kupata mapokeo mazuri ya wananchi.

Kulikuwa na ulazima gani wa kufanya sherehe hiyo? Kwa kizazi cha sasa ambacho kina muamko tofauti (rejea matokeo halisi ya uchaguzi mkuu uliopita), wala hawajui TANU ni nini! Labda wale wenye udadisi wa historia. Na hata wakiijua, haina mantiki yeyote kwao.

Nasubiri kwa hamu kufanywa kwa birthday party ya ASP. Tena basi mwakani ifanyike sherehe za kuzaliwa kwa TAA maana bila hiyo, TANU isingezaliwa! Halafu tena na sherehe ya kuzaliwa HIZBU. Ushanifahamu?

Nadhani hii comment imemaliza yote...
 
Hivi yeye alivyoenda kubembea kule Jamaica kwa gharama kubwa za pesa za walipa kodi na safari zake chungu nzima zisizo na tija kwa Taifa huku akifuatana na kundi kubwa la wapenda masurufu, huwa safari zile siyo anasa!?
 
Huyu bwana, hala lolote ni sharobaro tuu, anapenda kuonekana na kuongea sana kwamba yy ndio
mzee wa busara, but anaishi kwa majungu sana. Kamsingizia Lowasa bila sababu leo hii wameshindwa
ku prove if he is guilt. JK ndio anajua kila kitu kuhusu Dowans, ameamua kuuza ushahidi kwa
wamarekani mitambo ile ile mibovu juzi kakiri ni mipya.
 
Rais Kikwete amedhihirisha kuwa yeye ni mtu safi asiye na doa, lakini wanaomuangusha ni watendaji wake.
basi mwambie aache kulalamika,atumie mamlaka tuliyompa.Wananchi walalahoi 2nalalamika na rais wetu jamani nae hivyo hvyo!!!Yani panya kaingia ndani afu baba zima na midevu yake linaomba msaada tena kwa yowe,mke na watoto waende wapi sasa?
 
Kwa kweli hiyo ni comedy in the making. Yaani kwa kiongozi kusema "anashangazwa" na kutowajibika kwa viongozi ambao wako chini yake ni ushuhuda tosha kwamba kiongozi huyo is incapable, na mwoga wa kuwachukulia hatua ingawa anawafahamu fika kuwa hawawajibiki na wanatumia fedha za umma kwa anasa
 
Huyu ni mnafiki tu! Hana jipya. Analalamika lalamika tu na hana analofanya. Anatafuta huruma kwa wananchi wakati watu wameshamchoka! Poor Kikwete. Kuna siku atatoa na machozi kama Pinda.
 
hata hao waloambiwa kimoyo moyo walinena hayaa '' usitungie weweee we ndo taita wa anasa kila day uko hewani afu unajidai unatusemea kwa wananchi, kudadadeki''
 
WENYEKITI wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, amewashangaa baadhi ya viongozi wa chama hicho, akisema hawajituma, wamesahau wajibu wao na wanapenda anasa. Alisema tabia hiyo imejijenga kwa viongozi hao kiasi cha kusahau majukumu yao ambayo ni pamoja na kudumisha umoja na moyo wa kujituma. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Rais Kikwete alisema ni ajabu kuona viongozi hao wanashindwa kutekeleza majukumu yaliyoasisiwa na TANU, hata baada ya kuwezeshwa kwa rasilimali nyingi.

Kikwete alisema hayo wakati akizungumza na wanachama wa CCM katika maadhimisho ya kumbukumbu ya TANU na miaka 50 ya uhuru. Kwa mujibu wa Rais Kikwete, viongozi wa sasa wa CCM wamekosa moyo wa kujituma kiasi cha kusahau wajibu wao, licha ya kuwa na rasilimali nyingi ikilinganishwa na enzi za TANU.
“Sasa tumewapa magari, lakini hawaendi vijijini kuwatembelea wanachama. Wengine hata matawi hawayajui yanavyoendelea. Tusipokuwa na moyo wa kujituma, ndiyo utaona mambo yaliyopo sasa," alisema Rais Kikwete huku akishangiliwa na wanachama waliokuwa wamefurika katika Ukumbi wa Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam.
Rais Kikwete aliendelea: “Awali tuliwauliza, wana shida gani? Wakasema wanataka vipando (magari). Tukawapa Mahindra, wakaona hazitoshi. Siku hizi wana Land Cruiser. Lakini baadhi yao hawaonekani.

Kingunge alikuwa Katibu Mkuu wa TANU alifanya kazi kwa bidii bila gari. Leo wewe una shangingi unashindwa nini?” Akitoa mfano wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Rais Kikwete alisema msingi wa TANU, ni umoja na moyo wa kujituma. Alisema TANU ilishinda vikwazo vingi licha ya kutokuwa na rasilimali nyingi kama walizokuwanazo wakoloni, kwa kuwa walitegemea umoja wa wanachama waliokuwa masikini.

“TANU ilikuwa na uwezo mdogo wa rasilimali hivyo ilitegemea michango ya wanachama waliokuwa masikini. Siri ilikuwa ni umoja na mashikamano wa wanachama wake. Mwalimu Nyerere alisisitiza kitu hicho hadi anakufa, Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu,” alisema Kikwete Rais Kikwete alieleza kuwa kupitia umoja na moyo wa kujitolea, TANU ilishinda pia changamoto ya kuwaondoa wakoloni waliokuwa waking’ang’ania madarakani.

Kila mwenye akili timamu anaweza shangaa Kikwete anachozungumza. Anasema anasa zipi? Kwa sababu yeye anawauliza wanaomsaidia wanataka nini, wao wanamjibu mashangingi yeye anawapa wakati akijua wazi kuwa hiyo ni anasa lakini anawapa. Sasa anashangaa nini wao kupenda anasa wakati anawapa mwenyewe?
We have a serious leadership vacuum in this nation to the extent that even the president does not understand what he/she is talking, tumekwisha.
Yeye amekataa anasa zipi kusudi na wa chini yake waige mfano huo? hamna. Ati ukikaa mjini unasikia watu wanasema Lowasa anaandaliwa kuwa raisi Mungu tusaidie.
 
Nyani haoni kundule

2763766_017990ba91_m.jpeg
 
  • Thanks
Reactions: tz1
Back
Top Bottom