nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,803
Imeandikwa tarehe 20 Oktoba 2013 By Theopista Nsanzugwanko
UMOJA wa Viongozi wa Dini ya Kiislamu na Kikristo kutoka madhehebu mbalimbali nchini, wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa busara aliyoitumia kukutana na viongozi wa juu wa vyama vya siasa vya upinzani na kushauriana na kusikilizana kuhusiana na mchakato unaendelea wa Katiba mpya.
Wamesema kitendo hicho ni mfano wa kuigwa kwa nchi za Afrika, kwani ameonesha uwezo mkubwa wa kisiasa na kwamba, kiongozi wa kweli ni yule anayekuwa muungwana, mvumilivu na msikivu kwa wale
anaowaongoza.
Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa Umoja huo, Sheikh Said Godigodi kwa niaba ya viongozi wa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC), Pentekoste, Lutheran, Wasabato na pia Waislamu.
Licha ya pongezi zao kwa Rais Kikwete, Umoja huo umewataka viongozi wa vyama vya upinzani na asasi za kiraia kuunga mkono juhudi za Rais huku wakionywa wasiwe chanzo cha kuiingiza nchi katika vurugu na machafuko.
Alisema wanasiasa na wanaharakati wanatakiwa kuwa na weledi wa kutosha kwani wapo Watanzania wanaoamini wanapotoa matamko yao lazima wawe makini na kuonesha uzalendo kwa Taifa kama anavyoonesha Rais Kikwete.
Pia tunapenda kuwatahadharisha Watanzania wote kuwa makini na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa na Asasi za kiraia kwa kuwa historia inaonesha kuwa sehemu mbalimbali katika bara la Afrika, Asia na kote
Ulimwenguni ndiyo chanzo cha vurugu na machafuko, alisema Shehe Godigodi.
Hivyo aliomba kuwa makini kama anavyofanya Rais Kikwete kwa kuwa na dhamira safi na kupuuza wenye nia wasiotaka Katiba mpya ipatikane nchini.
Katiba mpya ni muhimu kwa mustakabali wa Taifa, hivyo tunampongeza Rais Kikwete kwa kukubali kupatikana kwa Katiba mpya ambayo tumekuwa tukiililia kwa miaka mingi, alisema na kuongeza kuwa, kauli za vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa viongozi wa upinzani hazisaidii, na badala yake kuwataka kujenga hoja za msingi.
Katibu huyo alikumbusha kauli za vitisho za wapinzani walizozitoa Jangwani hazikuwa na sababu wakati walielewa wangeona na Rais Kikwete na kuzungumza naye kwa kina.
Sasa wameonana na Rais na kufikia mwafaka, sasa zile kauli za kuanza mazoezi na mengineyo zilikuwa za manufaa ya nani? Ni vema viongozi hao wasiyumbishe wananchi, kwani kama Rais asingekuwa na dhamira njema katika kupata Katiba mpya asingekubali kuanza kwa mchakato huo, alisema Shehe Godigodi.
Wiki iliyopita, Rais Kikwete alikutana na viongozi wa vyama vya upinzani vyenye wabunge na kuzungumzia changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa kupata Katiba mpya na kufikia mwafaka, baada ya awali vyama hivyo kuonesha wasiwasi wa mwenendo wake huku wakitishia kutokuwa tayari mchakato
ukiendelea.
Katika mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam vyama hivyo pinzani vilifanya mkutano wa hadhara na kutoa kauli za vitisho kwa Serikali.
UMOJA wa Viongozi wa Dini ya Kiislamu na Kikristo kutoka madhehebu mbalimbali nchini, wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa busara aliyoitumia kukutana na viongozi wa juu wa vyama vya siasa vya upinzani na kushauriana na kusikilizana kuhusiana na mchakato unaendelea wa Katiba mpya.
Wamesema kitendo hicho ni mfano wa kuigwa kwa nchi za Afrika, kwani ameonesha uwezo mkubwa wa kisiasa na kwamba, kiongozi wa kweli ni yule anayekuwa muungwana, mvumilivu na msikivu kwa wale
anaowaongoza.
Kauli hiyo imetolewa jana na Katibu wa Umoja huo, Sheikh Said Godigodi kwa niaba ya viongozi wa Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC), Pentekoste, Lutheran, Wasabato na pia Waislamu.
Licha ya pongezi zao kwa Rais Kikwete, Umoja huo umewataka viongozi wa vyama vya upinzani na asasi za kiraia kuunga mkono juhudi za Rais huku wakionywa wasiwe chanzo cha kuiingiza nchi katika vurugu na machafuko.
Alisema wanasiasa na wanaharakati wanatakiwa kuwa na weledi wa kutosha kwani wapo Watanzania wanaoamini wanapotoa matamko yao lazima wawe makini na kuonesha uzalendo kwa Taifa kama anavyoonesha Rais Kikwete.
Pia tunapenda kuwatahadharisha Watanzania wote kuwa makini na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa na Asasi za kiraia kwa kuwa historia inaonesha kuwa sehemu mbalimbali katika bara la Afrika, Asia na kote
Ulimwenguni ndiyo chanzo cha vurugu na machafuko, alisema Shehe Godigodi.
Hivyo aliomba kuwa makini kama anavyofanya Rais Kikwete kwa kuwa na dhamira safi na kupuuza wenye nia wasiotaka Katiba mpya ipatikane nchini.
Katiba mpya ni muhimu kwa mustakabali wa Taifa, hivyo tunampongeza Rais Kikwete kwa kukubali kupatikana kwa Katiba mpya ambayo tumekuwa tukiililia kwa miaka mingi, alisema na kuongeza kuwa, kauli za vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa viongozi wa upinzani hazisaidii, na badala yake kuwataka kujenga hoja za msingi.
Katibu huyo alikumbusha kauli za vitisho za wapinzani walizozitoa Jangwani hazikuwa na sababu wakati walielewa wangeona na Rais Kikwete na kuzungumza naye kwa kina.
Sasa wameonana na Rais na kufikia mwafaka, sasa zile kauli za kuanza mazoezi na mengineyo zilikuwa za manufaa ya nani? Ni vema viongozi hao wasiyumbishe wananchi, kwani kama Rais asingekuwa na dhamira njema katika kupata Katiba mpya asingekubali kuanza kwa mchakato huo, alisema Shehe Godigodi.
Wiki iliyopita, Rais Kikwete alikutana na viongozi wa vyama vya upinzani vyenye wabunge na kuzungumzia changamoto mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa kupata Katiba mpya na kufikia mwafaka, baada ya awali vyama hivyo kuonesha wasiwasi wa mwenendo wake huku wakitishia kutokuwa tayari mchakato
ukiendelea.
Katika mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam vyama hivyo pinzani vilifanya mkutano wa hadhara na kutoa kauli za vitisho kwa Serikali.