Kikwete atua Dodoma na kupokelewa na Hamad Rashid

Status
Not open for further replies.
Labda kile chama kipya atakacholile la anzisha kitakuwa nyumba ndogo ya CCM!

nasikitika sana kuona bado watanzania tunakuwa na mawazo mgando kama wewe, vp kuhusu cdm kwenda ikulu na soon after that wakapoa na lile la kung'ang'ania katiba mpya ghafla likapoa, unadhani ni kwa nini? only reason ni kwa sababu lile walilokuwa wanapigia kelele lishasikilizwa kama walivyokuwa wanahitaji sasa hawana sababu ya kuendelea kulishikia bango......wote ni upinzani sasa haya mambo ya uccmfsdi smol haus unatokea wapi? hebu tafakari siasa za chuki huu si muda wake......mpinzani wa kweli ahitaji kuandamana tu yale mazuri lazima tuyasapoti.....jipange
 
Mwacheni yakhe ! Awasemee walomtenda akina maalim seif kinyume na walivokubaliana na ccm !

Muulizeni alipokwenda pemba peke yake na ndege ya atc nani alilipa gharama za kukodi ndege hiyo ? Si tunavojua atc haiendi pemba ati !

Samaki walana vao kwa vao !
Kwani hakai Wawi mpaka aende na akitokea Dar,au ni mbunge wa Wawi kwa remotesi ajabu tutasikia hata nyumba hana huko Wawi,bali ana bungalow Dar
 
Hakika kwa mwendo huu CCM wanakimbiza JET kwa miguu...very technical, au ndio waziri mkuu mstaafu WA ZNZ?vyeo vingine ni vya milele
 
Mbona unatoa habari za uongo Wewe, Haya hebu tuhabarishe hao Wamarekani wamepigwa lini hiyo pi na kwa sababu zipi na lini hasa waliondoka hapa nchini, mwisho Je? Hiyo kampuni ya Cmu ipo AMA haipo?

Usipoteze maboya bw.hassan124. Hamad aliwapeleka bungeni kuwatambulisha wawekezaji wa talktell tena wakati huo akiwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, lakini hiyo kampuni ilikuja kugundulika ni ya kitapeli na ililiza watu wengi sana akiwemo yusuph manji. Hamad hana maana wala muamana woowte!!!
 
Usipoteze maboya bw.hassan124. Hamad aliwapeleka bungeni kuwatambulisha wawekezaji wa talktell tena wakati huo akiwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, lakini hiyo kampuni ilikuja kugundulika ni ya kitapeli na ililiza watu wengi sana akiwemo yusuph manji. Hamad hana maana wala muamana woowte!!!

Usilojua usiku wa kiza.....nimeuliza hiyo kampuni ipo AMA la! Unatakiwa useme imekufa, ipo AMA cjui....basi kwa kukuibia Ni kwamba leseni ipo mkononi sasa utapeli upi tena huo?! Acha kuandika NON SENSE kwa dhamira ya kumchafua mtu tu Wewe, wanaokutumia waambie umebugi step.....kuna watu hawachafuliki Wewe!! ESPECIALLY Honorable Hamad Rashid Mohamed, jitahidi uwe msafi kwny nafasi Yako utaishi kwa Amani, chama chenu cha Chuki Ubinafsi na Fitna naona kinakufa vibaya mno.....na kosa lenu kubwa Ni kuabudu mtu....Yule Ni mwanadamu tu Kama Wewe na mimi elewa hata yeye hukosea na kukosolewa Ni muhimu kwani kuteleza si kuanguka....sawa sawa?!!
 
mimi nawashangaa hawa binadam,viongozi wa chadema,cuf nk walienda ikulu nakunywa juice ya ccm,ajabu kila m2 anamshangaa mh hr:acheni senge yenu
 
Bila shaka anaenda kutoa shule kwa Wabunge wake kuwapa shule ya kwa nini ameridhia mapendekezo yaliyowasilishwa na vyama na asasi za kijamii. Cha kushangaza ama sielewi Hamadi Rashid kaongoza mapokezi. Ama kakabidhiwa na Makinda kwa muda ama ni harakari za kuhamia CHAMA TAWALA.

Tazama hapa.
IMG_4218.JPG

Rais Jakaya Kikwete akiteta na Mbunge wa Wawi,Hamad Rashid baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma leo akitokea Mwanza.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.



IMG_4221.JPG

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege Dodoma akitokea Mwanza.

Dah! Kumbe baba liz nywele zinaanza kunyonyoka....Kipara nakiona kwa mbaliiiiiii...Tehe tehe tehe tehe....
 
binadam hamuishi mattizo;mbowe na silaa walipokwenda kunywa juice ya jk hamkuona kama ni noma:mtatiro na machano nao wakaenda kunywa kwa ck yao,hawakuitwa wasaliti;mh hr anaonyesha robo ya uwezo wake ktk kuwasaidia wabongo mnachoongaaa acheni muone mavituz huo ndo mwanzo wa shughuli yenyewe
 
Wawekezaji kutoka nchini Hispania waliokuja nchini kwa mualiko wa Mhe. Hamad Rashid Mohamed (CUF) mbunge wa WAWI, wametokea kuwa gumzo kubwa baada ya miradi yao kuivutia mno bunge na serikali kwa ujumla. Wawekezaji hao ambao walitambulishwa bungeni leo asubuhi na Naibu Spika Mhe. JOB Ndugai rasmi kama wageni waalikwa wa mhe. Hamad Rashid wamekuja na miradi mbalimbali ambayo kwa hakika ikitiliwa maanani na serikali na kuacha ukiritimba hakika itakuwa ni mkombozi kwa maisha ya Watanzania wengi.
Wawekezaji hao Professor Santiago (retired minister Spain) na Dr. Ruben wamekuja na:
1. Mradi wa nyumba za bei nafuu, ambapo wanaweza kujenga nyumba zaidi ya 300 kwa kipindi cha mwezi mmoja
2. Mradi wa kilimo cha kisasa(production of organic fertilizer) wenye uwezo wa kutoa mavuno tani 7-9 kwa hekari moja.
3. IT
Just to mention a few.
Baada ya serikali kuvutiwa mno na miradi hiyo, iliwalazimu kumjumuisha Mhe. Hamad katika orodha ya viongozi watakaompokea Rais aliyekuwa anawasili mjini Dodoma mchana huu kutoka Mwanza alipokuwa amehudhuria sherehe za kuzaliwa kwa CCM.
Rais Kikwete aliitisha kikao cha dharura na wageni hao katika kiwanja cha ndege mjini hapa. Ripoti zaidi zinasema Wageni hao walikuwa wamefanya vikao na viongozi mbalimbali wa serikali kama Waziri Mkuu, Waziri wa Uchukuzi, mama Mary Nagu, Ofisi ya Spika ambapo haikujulikana mara moja kama walionana na spika ama naibu wake.
Wafuatiliaji wa mambo wanasema kwa uwezo na jitihada anazozionyesha Mhe. Hamad Rashid licha ya kwamba hivi karibuni tu amepata matatizo ya kuvuliwa uanachama katika CUF, anaonyesha ni mfano wa kuigwa kwa viongozi wengi hapa nchini na hata nje ya nchi kwani hajaonyesha kutetereka licha ya kwamba amekuwa katika mgogoro mkubwa na viongozi wa chama chake hicho.
Mkuu, naomba source ya habari hii, tafadhali.
Mimi nina wasiwasi na hawa wawekezaji wanaojipachika vyeo na elimu na elimu hewa kwani nimetafuta orodha ya mawaziri wa Uhispania tnagu mwaka 1982 -2012 (miaka 20) hakuna ex-minister mwenye jina hilo. Huyu Professor Santiago katokea wapi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom