JK atakiwa kuomba radhi

Waislam wapewe hiyo mahakama ya kadhi,ila lisiwe suala la kikatiba na wala isifanye kazi kwa pesa za serikali.Vinginevyo wapewe,ni haki yao ya msingi.
 
Mwanabodi,
Nimejaribu kwa muda mrefu kuvumilia haya nayoyasoma hapa lakini imefikia wakati inabidi nizitoe hizi pamba masikioni kuyapokea yote kisha kusema yangu machache kwa haki hiyo hiyo mnayoitangaza wengine.
Ni lazima katiba iwe na vifungu vinavyoruhusu baadhi ya sheria kutambua uhuru wa watu fulani ili kutimiza haki mnayozungumzia. Mnaposema Fedha na kodi za Watanzania wote mna maana gani?.... maanake hili swala sasa hivi linaanza kujenga hoja za Udini zaidi na watu mnajibu mengi kwa kutazama rangi zenu za dini.
Sasa ikiwa serikali haitambui mafundisho ya Kikristu inawezaje jenga kinga ya dini hii kuweza kuendesha shughuli zake nchini?..Kila sheria nchini inajengwa kwa kutazama vipengele vyote (Objective) ktk kujenga na sio ktk kubomoa (Negative) manner. Katiba inajengwa kulingana na mazingira yetu, watu wake na mambo yote yanayohusu jamii nzima kwa mtazamo wa kujenga na kuimarisha jamii hiyo. Hata mikataba inayotiwa sahihi ina sheria zake ktk Katiba kwa kuwatazama wawekeshaji, miradi na kadhalika kwa manufaa yetu sote hata kama ni kundi dogo la hawa watu wanaopewa sheria hiyo. Kuna sheria za Kikatiba zinazowapa nguvu na haki wanawake, watoto na hata wageni tofauti na kundi la watu wengine kwa sababu hizi Sheria zipo kwa ajili ya kuweka usawa ama kuleta maendeleo kwa jamii nzima.
Wanabodi, rais wetu alitoa ahadi ya kuwepo kwa korti ya Kadhi na zipo sababu ambazo zilifanya yeye kuafiki ama kutoa ahadi swala ambalo sisi kama raia wake inabidi tujenge hoja zinazolinda maslahi ya Taifa na sio kubomoa. Tatizo kubwa linalojitokeza hapa yaonyesha wazi sio korti hizi ila ni hofu yenu kwa Uislaam. Hofu ambayo Mtikila kama kiongozi wenu wa dini kainjenga ktk mioyo yenu na sasa mnaanza kuamini kabisa kuwa korti za kadhi ni mbinu ya waislaam kuutokomeza Ukristu. Hoja zenu zinajieleza wazi kabisa na hata hizo kodi mnazozungumzia ni sababu finyu zilizotanguliwa na hofu yenu kuhusu Uislaam.
Kitu cha maana hapa ni kutoa mapendekezo yetu ktk swala hili kisha tujenge hoja inayolingana na kuprotect maslahi ya nchi na sio kuzungumzia maswala ya fedha na kodi wakati ni fedha na kodi hizo hizo zinazoendesha serikali yetu ktk kila taasisi. Ni sawa na mtu kusema sheria za Uhalifu kuwepo kwa Polisi ama Jela ni upotozaji wa kodi za wananchi kwani mimi sio mhalifu na wala sintakuwa. Ukitazama kujitenga wewe na hao wahalifu kisha ukajenga hoja. Ikiwa kriti za kadhi ni too much kwenu jengeni hoja inayohusu korti hizi na waislaam sio kutazama nje ya waislaam kama tunavyozitazama korti zetu, Polisi na jela zetu tukitazama na kuzingatia Uhalifu (crime).
As a Muslim sioni sababu ya muhimu kwa Kikwete kwenda Vatican na naweza jenga hoja za kipuuzi lakini kama naelewa nini mahusiano ya jamiii ktk mawasiliano siwezi kuweka visingizio na kudai kwa nini kodi za waislaam zimelipia ziara hiyo ya rais huko Vatican!. Huu ni ufinyu wa kutazama swala zima linalohusiana na ziara za rais na kama nita raise swali kwa njia hiyo nitakuwa nachekesha. Zipo sababu nyingi za kuhoji ziara za rais lakini sio kwa mtazamo wa dini.

Rais Mwinyi alitoa ahadi ya kurudisha shule na mahospital kwa madhehebu ya dini hasa wakatoliki mbona hamkupiga makelele na kuuliza kulikoni kwa mtazamo huu mnaoutumia hapa. Naelewa kwa uhakika kuna walimu waislaam kibao walifukuzwa kazi zao kwa sababu tu ni waislaam lakini sijasikia mkisema yote haya isipokuwa leo Mtikila mshenzi mmoja kajenga mioyo yetu kuamini kuwa Waislaam ni Magaidi basi nanyi mnadakia na kuanza kumwita rais wenu GAIDI just because ni Muislaam aliyetoa ahadi kwa waislaam. Mbona Nyerere alitoa ahadi nyingi tu kwa Vatican na hakuna muislaam aliyejenga hoja za kipuuzi kuulizia kodi za waislaam.. ahadi ambazo alikuja zitimiza lakini bila kuathiri maisha ya waislaam.
Guys sisi tumesoma ktk shule za katoliki na tumelazimika kutumia majina ya kikristu kuweza kupata nafasi ya kusoma. Tazama huko Tanga kuna watu kibao wenye majina mchanganyiko utasikia mtu akiitwa Gregory Hamid, wote hawa wamebadilisha majina yao kwa sababu ya kutafuta elimu chini ya himaya ya kikristu leo sheria zinabadilika kidogo mnaanza kutazama ni kwa faida ya waislaam.
Pleeease kluna tatizo na korti ya kadhi toeni hoja zenu zikizungumzia korti hiyo na sio waislaam kuwa heading ya mada kwani wapo waislaam wasiokubaliana na korti hizo.

KUWAITA WAISLAAM MAGAIDI ni ushenzi, Upumbavu na Ufisadi mkubwa unaotokana na utumwa wa imani ya dini..

Mkandara hongera kwa article na majibu yako mazuri sana.
Kilichopolelea uandike ni uchungu uliokuwa nao juu ya kutukanwa kwa uislamu na vinara hawa wachache wenye moyo wa chuki dhidi ya imani ya kiislamu.
Kuhusu Fedhuli Mtikila nani asiye mjuwa juu ya vita vyake vya muda mrefu dhidi ya uislamu. Wakati wa vuguvugu la vyama vingi mwanzoni mwa miaka ya 90 ailkuwa hachoki kuushambulia na kuudhihaki uislamu..akiwaita waislamu washenzi na watu wasio wastaarabu ktk jamii.
Anachokifanya leo ni kilele cha vita yake dhidi ya uislamu na mbaya zaidi mi jitu mi-jahili ina zungumza utumbo mtupu humu ndani ya JF.
Mimi naona ukomo wa stahamala unaweza kufika tamati ikiwa hoja za kizembe za aina ya Mtikila na wachangiaji humu hazita kwisha. Nani asiyejuwa kama nchi yetu ina balozi wa Vatican nchini lakini imekuwa mstari wa mbele eti kupinga Tanzania kujiunga na OIC. Visingizio vya chuki vinatolewa eti kwa kuingia OIC nchi itakuwa ni ya kiislamu. Huu ni uzandiki mkubwa. Uganda imeingia mbona hai itwi ni nchi ya Kiislamu?
 
Kingwele sijui kama unasoma yaliyoandikwa au la, mbona Tanzania ina Ubalozi Uarabuni (Saudi) na hilo siyo tatizo kwako?
 
Wachangiaji wengi hawapingi kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi,ila tunachosema ni kwamba waanzishe tu ktk taratibu zao ktk misikiti yao bila kuingilia utendaji wa kila siku wa shughuli za serikali kwa maana ya kuziendesha kwa kodi za watanzania.
Wakristo wana baraza yao ktk kila kanisa lilipo na wahumini wa mahali hapo upeleka matatizo yao yanayoweza kutatuliwa na kanisa.lakini hakatazwi mtu kwenda mahakamani kama anaona inafaa.
 
Katibu Tarafa,
Na mlipoifanya Jumapili kuwa siku ya mapumziko ili mwende kusali imemsaidia nini Muislaam ama Msabato?...Hata Bunge na IKULU husimama siku hiyo what's a big deal?..
Nitarudia kusema hivi, HIyo Korti ya kadhi haitufai, haitufai not because ni korti ya Waislaam bali Kile inachojaribu ku solve hakiwezekani ktk mazingira yetu.
kwa majibu yenu hayo itakuja fikia hata kupinga daraja kujengwa Mtwara tukiangalia nini faida yake kwa mkazi wa Mwanza! Ni hatari kubwa hasa tunapofikiria kuwa na madaraka mikoani. I mean sioni kabisa hoja nzito isiyokuwa na mtazamo wa kidini.
Mkuu Katibu tarafa,
Bila katiba hawa watu (wanyonge) hawawezi kupewa haki yao na msikiti hauwezi wala hauna nguvu ya kumlazimisha mtu kwani hawana sheria kikatiba, kubwa hapa ni Sheria. without Sheria everyone walks!.. huwezi kunilazimisha mimi kutomfukuza mke wa pili ktk nyumba yangu ikiwa hakuna sheria. Kwa nini tusiwatazame hawa wanyonge bila dini hiyo? yaani tukatae maamuzi yatakayo tokana na imani ya dini badala ya kukataa korti kwa kuweka dhana kuwa waislaam wanataka kuichukua nchi.
Tatizo kubwa la Korti hii ama sheria ktk Katiba kuongezwa kipengele ni pale swala linapochukuliwa kuwa ni haramu kidini. Mathlan, nimetaja watoto waliozaliwa nje ya ndoa. Korti ya kadhi haiwezi kuwasaidia watoto hawa ktk mirathi hasa kutokana na confussion iliyopo kati ya sheria za dini na hata ukitazama sheria zetu kitaifa - zinagongana. Mara nyingi watoto hawa wamekuwa na wakati mgumu sana ktk maisha yao sawa na wanawake walioolewa ktk ndoa za ukewenza, iwe kiasili ama Kiislaam.
Wakristu hawana tatizo la Kisheria kwani sheria zetu zimevutwa toka sheria za Mama Malkia - Ukristu. Mara nyingi huko kanisani kinachofanyika ni mapatanisho ktk relationship za watu, sio maswala yanayohitaji sheria.
Nadhani tukitaka kukata issue ni muhimu tuzungumze jinsi maswala kama haya yanavyoweza kusuluhishwa kwa mtazamo wa kati. yaani dini zote, tamaduni, mila na mazingira yetu kiasi kwamba sheria hiyo inaweza tumika kote.
nakumbuka mara nyingi sheria inapoandikwa huwa na vipengele vinavyosema:- Ikiwa Kipengele A kinahusika basi basi sheria inasema hivi, Kipengele B na C vitaendelea kutumia sheria kifungu Blaa blaa blaa.
Kama sheria inavyotazama swala la Custody ya watoto hutazama pande mbili kati ya Mume na Mke na zikizingatia Uraia wa wahusika ktk kutoa sheria. Hapa Uraia iwe sawa na dini ya mhusika na sio kusema siwezi kulipa kodi kwa ajili ya mtoto asiyekuwa wangu hizo custody wakazimalizie huko walikofunga ndoa!.. damn.
 
Mkandara,
serikali na mahakama zinatambua ndoa za kimila pamoja na zile za kidini. kunapotokea shauri la talaka, au mirathi, mahakama huwauliza wahusika ndoa yao ni ya aina gani, na wanataka shauri lau liamuliwe kwa kufuata taratibu za kimila au kidini.

Majuzi Zanzibar wameanzisha Ofisi ya Kadhi Mkuu ambayo inatambuliwa Kikatiba na iko chini ya waziri wao wa sheria. Mara baada ya kuanzishwa kwa Ofisi migogoro ikaanza.

Kwa mujibu wa katiba Kadhi Mkuu anapendekezwa na Waziri wa Sheria na kuidhinishwa na Raisi wa Zanzibar. Walitokea Waislamu waliokataa kumtambua Kadhi Mkuu wa ZNZ kwasababu alipendekezwa na Waziri wa sheria wa ZNZ wakati huo ADAM MWAKANJUKI--Mkristo!!

Mimi nafikiri badala ya Waislamu kudai Mahakama ya Kadhi, wangependekeza namna ya kuziboresha sheria zilizopo, na taratibu za mahakama zetu, ili waweze kupata huduma bora zaidi.
 
It's a 'dead horse' pple....let go!!. Tanzania hakutakuwa na KADHI COURTS fullstop, mjadala umefikwa na umauti. Nchi ni secular na kwasababu hiyo basi na nyinginezo mahakama zote pia zitabaki kuwa secular. Kuendelea kujadili suala hili ni upotezaji wa muda na resources uliokithiri!!.
 
Back
Top Bottom