Hawa jamaa wana mbinu nyingi za kutaka kuvuruga mipango ya UN, yaani wanafanya mambo ya kitoto kuhadaa DUNIA kwamba suala la DRC si rahisi kupatiwa ufumbuzi!! Kwa nini nalisema hili - leo Museveni kaja na mpya, anasema waasi wa Al Shabaab wamevamia mji mdogo wa Kongo uliopo mpakani na Uganda eti waliuteka kwa muda na kuwafanya RAIA wa Kongo kukimbilia nchini Uganda. Hivi Al Shaabab wana interest gani ndani ya DRC, kwa nini wajitokeze wakati M23 wamepewa masaa 48 kusalimisha silaha zao - kwa mawazo yangu naona huu ni mchezo wa kuhigiza uliochongwa na M7 na PK wakiwa na lengo la kushtua nchi za magharibi specifically Merikani ambayo imewakalia kooni, wala siwezi kushangaa kama wanaohitwa ni Al Shabaab ni kikosi kidogo cha majeshi ya M7 au PK kilifanya operation hii kutaka ku-draw attention za International Community oh yes publicity STUNT. Ukiangalia kwa makini utagundua siku hiyo hiyo au kesho yake Balozi wa Rwanda ndani ya UN alipokuwa anaulizwa maswali/ufafanuzi na wandishi wa habari alikuwa anajibu kimkato mkato kwa jeuri na kiburi kabisa mtu unashangaa hawa watu wamelelewa VIPI - jamaa hawa wako mahili sana katika harakati zao za kudanganya DUNIA, wanacho tafuta hapa ni kutaka kuonyesha kwamba saula la DRC ni gumu kutatuliwa, madai ya kusema kwamba kundi la AL Shabaab wamekwisha jipenyeza ndani ya DRC(uongo mtupu) lina lengo la kuvuruga mipango ya UN, yaani UN ipunguze kasi ya kuwashughulikia M23 na kuanza kufikilia Al Shaabab wa kuchongwa na jamaa hawa. Nataka niwakumbushe kwamba dunia imekwisha washtukai mbinu zao, wasipo jirudi watasjilahumu sana siku za usoni.