Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENTS OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumamosi, Julai 31, 2010, amemtumia salamu za pole Katibu Mkuu wa CHADEMA, Mheshimiwa Wilbroad Slaa, kufuatia habari kuwa kiongozi huyo amevunjika mkono.
Aidha, Rais Kikwete amemtakia Mheshimiwa Slaa aweze kupona haraka na kupata nafuu ya kuendelea na shughuli zake za kila siku katika kutumikia umma wa Watanzania.
Katika salamu hizo, Mheshimiwa Rais amemwambia Mheshimiwa Slaa: Nimepokea kwa masikitiko makubwa habari za kuumia kwako kwa kuvunjika mkono. Kwa dhati ya moyo wangu, nakutumia salamu nyingi za pole na kukuhakikishia kuwa niko pamoja nawe katika kipindi hiki kigumu cha maumivu.
Ameongeza Mheshimiwa Rais: Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akupe uwezo wa kupona haraka ili uweze kurejea katika shughuli zako za kutumikia umma wa Watanzania.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
31 Julai, 2009