Halafu TUCTA ambayo inakomba pesa nyingi kutoka kwenye mishahara yetu tena kwa lazima iko kimya. Ipo siku watu wataamua kutembeza bakora kama former DC Mnare!
Ni sahihi serikali yetu haijaongeza mshahara kwa asilimia iliyotamkwa na Mh.Rais wetu.
Lakini TUCTA hivi wanafanya nini katika kupigania maslahi ya watumishi? Mimi binafsi sijaona kama wanasaidia mana hata siku moja hawajawahi sema jambo wakalisimamia mpaka mwisho na likawa na mafanikio chanya.
Mimi naona vyama vya kisekta vina msaada kiliko vyama huru vya wafanyakazi mfano chama cha madaktari, chama cha walimu wanaodai malimbikizo ya walimu n.k.
Watumishi wa umma leo hii ni mwaka wa tatu hawajapandishwa vidato vya mshahara mwaka wa fedha unapoisha na mwingine kuanza, unadhani serikali imewaibia watumishi kiasi gani ktk hilo? TUCTA wapo na wahajaliona hili kama ni tatizo? Mtumishi anatakiwa mwaka unapoisha na mwingine kuanza apande kidato cha mshahara mfano kama mwaka 2011/2012 alikuwa TGTS D1 mwaka 2012/2013 aonekane TGTS D2, lakini setikali imekuwa haipandishi tena vidato ikikwepa gharama.
Je TUCTA kazi yenu ni nini kwa watumishi au ni kupokea hundi tu za makato ya mishahara pasipo kuwatetea maslahi yao? Ng'ombe mlishe ndo umkamue bwana!!
I submit