Jiwe la sumu ya nyoka

Mkuu hata mm ninalo jiwe la nyoka. Kuna secondary fulani nilisoma huko mbeya kuna nyoka wengi sana hivyo kwenye joining instructions wameagiza mawe mawili ya nyoka. Moja unaweka kwenye tranka na jingine unatembea nalo mfukoni. Ni msaada mkubwa sana hayo mawe. Hata ukilichemsha kwa maji moto kwa nusu saa hivi linatoka sumu yote thou maziwa ni recomended kwa ajili ya sumu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilishawahi kulitumia hilo jiwe miaka kadhaa iliyopita nyuma,hakika ukiambiwa huwezi amini jinsi linavyofanya kazi yake,kwa ufanisi
 
Pole sana kaka mshana,hapa mwili wote unanisisimka. Jamani hivo viumbe naviogopa balaa,yaani Leo nitaota vibaya mno. Nikiona picha au nikimuona live ninaota yaani nawaogopa hao
Usiogope bhana, ujue nyoka wa kuchoma watamu sana.
 
Pole sana kaka mshana,hapa mwili wote unanisisimka. Jamani hivo viumbe naviogopa balaa,yaani Leo nitaota vibaya mno. Nikiona picha au nikimuona live ninaota yaani nawaogopa hao
Kuna siku nilikuwa peke yangu kwenye chumba mara namuona nyoka kitandani halaf usiku!!! Nilipata ujasir sijui wapi tu nilimuua kesho yake nikahama nikaenda kupanga sehem nyingine.
 
Kuna siku nilikuwa peke yangu kwenye chumba mara namuona nyoka kitandani halaf usiku!!! Nilipata ujasir sijui wapi tu nilimuua kesho yake nikahama nikaenda kupanga sehem nyingine.
nacheka kama mazuri. Yaani mi nikiona hata picha itanitesa nitaota sana yaani duh.
 
mshana jr pole sana bingwa, kwanza huyo kiumbe hautakiwi kumpa RIP anastahili RIH (Rest In Hell). Pili, sayansi ya hilo jiwe hata mimi inanishangaza sana. Kwa sie wa kijijini mambo ya nge na nyoka kawaida sana. Niliwahi kung'atwa nve mguuni, unafungwa na kamba sehem ya juu kupunguza mzunguko wa damu, nikachanjwa na kuwekewa hicho kijiwe, kidogo tu cheusi. Kiliganda pale hadi hali ilipokua shwari kikadondoka.

Nimefurahi kuongeza elimu kutoka kwa jemedari MSAGA SUMU sijui kama alichoandika kina ukweli lakini kimenishawishi. Na kuanzia leo ataitwa Mkemia
 
nyie ndo mliokuwa mnafeli mitihani huku mkiwa mmesoma vitu vingi,hujikiti kwenye mada unajib hata usichoulizwa!
 
nyie ndo mliokuwa mnafeli mitihani huku mkiwa mmesoma vitu vingi,hujikiti kwenye mada unajib hata usichoulizwa!
Teh teh teh
Umenichekesha sana , nimejibu kwa upana na kutoa mifano Kwa faida ya wote ili kesho na keshokutwa tusije kujibu kitu icho icho kikiulizwa ktk angle nyengine.
In short ilo jiwe ni jeusi na sio la kutengeneza kama mdau mmoja alivyosema labda kama kulishepu na kulichonga hapo ni sawa.
Hilo jiwe ni carbonious rock na sifa yake kubwa ni kunyonya ions ( kumbuka kuwa damu ni ions ) iyo process ya kunyonya inaitwa adsorption na inafanyika kutokana na physical properties zake za kuwa na porous.
Nikatolea mfano ata maji yenye chumvi unaweza kuyachuja Kwa kutumia kaboni na chumvi ikanyonywa Kwa kiasi kikubwa, mtu atakayetumia activated carbon kwenye mgonjwa aliyegongwa na nyoka itakuwa more effectively treatment.
Pia hizi carbon utumika ata kwenye viwanda vya maji na soda for purification kuondoa madini fulani yaliyomo.
Kwa kuongezea pia utumika kufyonza gold ambayo ipo kwenye solution form.
Mazumuni ya kwenda mbali zaidi ili kuongeza uelewa Kwa watu wengine na kuitendea haki JF
 
ulichokifanya hapa ni kutafsiri notes!
na huu ndo udhaifu wa mfumo wa elimu tz
 


Pole sana. Jiwe unaweza tengeneza mwenyewe. Chukua mifupa migumu hasa wa mguuni au kichwani mwa mnyama kama Tembo, Ng'ombe au Nyati. Uchome kwenye moto mkali kwa Muda mrefu hadi uwe mweusi hapautapata hilo linaloitwa "Jiwe la nyoka" .

Huwa tunadanganywa ni jiwe toka Tabora blablah ...

NB: Sio kila nyoka ana sumu. Just animals like others, they are part of ecosystem. don't hurt them. Protect snakes!!
 
ulichokifanya hapa ni kutafsiri notes!
na huu ndo udhaifu wa mfumo wa elimu tz
Mkuu kwenye hili nafikiri % kubwa hatuchekani waTZ documents matters more than the know how practically ya jambo fulani na hapa ndiyo tunakwama sana.
Na tunaamini zaidi katika Newton's Laws kuliko mambo mengi yanayogusa jamii moja kwa moja.
Hili linathibitika katika kuvipa kipaumbele vitu vya nje zaidi ya vyetu, na hata mfumo wa elimu ukibadiliswa kama haujajengwa utamaduni wa kuthamini ubunifu na tafiti mbalimbali bado yatakuwa yaleyale.
HAITOSHI TU KUKOSOA ILA NINI MBADALA WA JAMBO HUSIKA AU UNGEPENDEKEZA kipi kilipaswa kuwa jibu sahihi au suluhisho?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmh am so sorry I will never protect a serpent

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…