Jiwe kubwa(Asteroid) kupita karibu na Dunia April 13, 2029

sijui nini

JF-Expert Member
Sep 29, 2010
2,553
1,285
Jiwe kubwa (asteroid) lililopewa jina la Apobhis kupita karibu na dunia(flyby) mwaka 2029. Jiwe hilo liligundulika na Wanasayansi wa anga mwaka 2004 likiwa na takribani mita 340 za Kipenyo na litapita karibu na dunia kiasi cha umbali wa Km 31,000 kutoka duniani.

Ingawa Wanasayansi bado wanaamini jiwe hilo halitakuwa na madhara yoyote kwa dunia ila wanaamini ni moja ya nafasi chache zitakazowawezesha kujifunza zaidi juu ya mawe haya yanayopita karibu na dunia.

Kwa ukubwa wa jiwe hili inasemekana kuwa kiasi cha watu billion 2 wataweza kuliona kwa macho bila kutumia kiona mbali. Bado hakuna maelezo kamili juu ya muda na mahali gani haswa litaonekana ila wanasayansi bado wanajipanga namna ya kuweza kukusanya data na kujifunza zaidi juu ya jiwe hilo.

Pamoja na kuwa Wanasayansi wanaamini kuwa jiwe hilo halitakuwa na madhara yoyote ila bado wanaamini kuna uwezekano mkubwa miaka mingi ijayo dunia ikaja kugongwa na mawe ya angani kutokana na kuongezeka kwa idadi ya mawe haya yanayopita karibu na dunia.

Source :
 
Mkuu mita 340 kwa haya mawe ni jiwe kubwa sana.. Hilo likipiga dunia madhara yake si ya kawaida kama unavyodhani.. Linaweza likatumaliza
Mita 340 kiongozi ni kama viwanja vitatu na robo vya mpira tu hivyo hata eneo la uwanja wa taifa na uhuru lote halitajaa, Je kitakachotumaliza ni speed yake na kishindo chake litakapopiga?
 
Huwa yanatoka wapi wanasayansi bado hawaaamimi kuwa mungu yupo.
Mkuu universe ni kubwa mno.. Mfumo wetu wa sayari ni kama katone ka maji ndani ya bahari.. Humo kuna ma vitu ya kila aina.. Haya mawe yapo mengi kwenye mfumo wetu wa jua na kuna ambayo yanayotokea nje ya mfumo wetu wa jua.. Kuna mawe yanazunguka mzunguko wake ni mkubwa kiasi cha kutumia mamia hata million ya miaka kukamilisha mzunguko.. Yapo mawe ambayo wanasayansi wa zamani walishayaona yakipita duniani na kwa hesabu zao za zamani walijua yatarudi tena na kweli wanasayansi wa skuiz kwa vyombo vyao wamethibitisha ni kweli yanazunguka jua na yatarudi tena huko miakabya mbele
 
Mita 340 kiongozi ni kama viwanja vitatu na robo vya mpira tu hivyo hata eneo la uwanja wa taifa na uhuru lote halitajaa, Je kitakachotumaliza ni speed yake na kishindo chake litakapopiga?
Jaribu kufatilia habari za anga uone jiwe la saizi hiyo likigonga dunia madhara yake yatakuaje.. Ndo maana wanasayansi wanatumia ma billion ya hela kwenye mfumo ya ulinzi wa dunia ili kuweza kutambua mapema uwepo wa mawe haya.. Madhara ya jiwe kama hili ni kutokana na nguvu (force) inayotumia kugonga.. Mfano jiwe linalosemekana kupiga dunia na kuathiri uwepo wa dinosaurs lilikuwa na kiasi cha metre 12,000 hivi na madhara yake yalikaa karne na karne na ndo chanzo cha dinosaur kuisha kabisa

Kwa kuongezea soma hapa :

A potentially hazardous object (PHO) is a near-Earth object – either an asteroid or a comet – with an orbit that can make exceptionally close approaches to the Earth and large enough to cause significant regional damage in the event of impact.

An object is considered a PHO if its minimum orbit intersection distance (MOID) with respect to Earth is less than 0.05 AU(7,500,000 km; 4,600,000 mi) – approximately 19.5 lunar distances – and its absolute magnitude is brighter than 22, approximately corresponding to a diameter above 140 meters (460 ft).This is big enough to cause regional devastation to human settlements unprecedented in human history in the case of a land impact, or a major tsunami in the case of an ocean impact. Such impact events occur on average around once per 10,000 years. NEOWISE data estimates that there are 4,700 ± 1,500 potentially hazardous asteroids with a diameter greater than 100 meters.
 
Hilo.dude lingekuwa linakuja duniani wazungu wangelipiga na mabom likavunjika vipande.
Waafrika hatuna hofu mabro zetu wazungu wapo
WHILE THE
WORLD WORRIES ABOUT THE FUTURE...... 1 BILLION AFRICANS ARE
SHARING A COKE..
 
Back
Top Bottom