Philipo Khan
Member
- May 14, 2016
- 37
- 44
Mbaya zaidi kituo cha Ukaguzi ni kimoja tuHili la kukagua Magari yanayotoka UK ni ulaji aliyopewa Lukosi wakishirikiana kula pesa bila jasho. Magari ya UK uwafanyiwa ukaguzi kila mwaka na huwezi kuliingiza gari lako barabarani kama halina cheti ya ukaguzi. Ukipatikana gari lako laweza kusagwa na wewe unachukuliwa point tatu au sita kwenye leseni yako pamoja na faini isiyozidi pound 500.
Ivyo siyo rahisi kwa mtanzania ambaye yupo UK akatuma gari ambayo haina MOT. Hili la ukaguzi ingewekwa uko nyumbani mfano unapoenda kulipia kodi zako wakati wa kutoa gari uonyeshe MOT yako. Siyo lazima MOT itoke kwa Lukosi kwani hapa UK sehemu pa kuangalia MOT ni karibu kila mtaa utawapata na wanatambulika kihali na serikali ya UK.
Usipoonyesha MOT wakati wa kutoa gari lako Dar ndio upigwe faini kali kwasababu itakuwa ni uzembe wako kuliko sasa unaambiwa ukitaka kutuma gari Tanzania lazima upeleke gari kwa Lukosi hata kama unakaa miles 100 ndio akupe MOT wakati yapo magarage kibao hadi mlangoni kwako.
Kwa kifupi MOT aliyopewa atoe Lukosi ni deal ya baadhi ya wakubwa uko Tanzania wanakula pesa pamoja. MOT hapa UK ni pound 30 hadi £45 lakini Lukosi na vibosile wake wanachaji pound 150. Inatuwia vigumu mfano unakaa Moshi inabidi uendeshe gari hadi Dar ndio ukapate MOT ya Lukosi Wakati hapo Moshi wa kuweza kukupatia MOT wapo zaidi ya 300.
Angalia tunavyonyanyaswa kwa ukiritimba za bongo bado wanaleta hadi huku. Hapa UK hakuna ujanja wa kusema kuwa utafanya kwenye MOT kwasababu gari lako likipata ajali ikaonekana ulicheza na MOT mwenye garage aliyetoa kibali inakula kwake pamoja na wewe.