Jiondoe kwenye kifungo kisicho na ulazima

Jiondoe kwenye kifungo kisicho na ulazima

Tabu ni pale unaporuka majivu na kukanyaga moto! Namaanisha kuwa waweza kujiondoa leo lakini kesho ukajiingiza pabaya zaidi. Mapenzi .......
mkuu unapoondoka sehemu nadhani hutakiwi kuanza tena mahusiano, Bali unatakiwa kuujenga msingi bora kabla hujaanza tena KUPENDA
 
Watu hawa ni lazima tuwasaidie kutoka huku walipo na kuondokana na vifungo hivi. Je tutawasaidia kwa Vp
Mkuu njia pekee na inayo fanya kazi siku zote! Ni mhusika mwenyewe atambue tofaut ya hali aliyonayo (anayoyapitia) na aamue kuchukua hatua (bila other force )
 
mkuu unapoondoka sehemu nadhani hutakiwi kuanza tena mahusiano, Bali unatakiwa kuujenga msingi bora kabla hujaanza tena KUPENDA
Labda uamue kutopenda tena vinginevyo hata kama ungejipa miaka 10 waweza kujikuta umeangukia pabaya zaidi ya mwanzo. Kikubwa ni kujitahidi kuchukuliana na kuvumiliana,kujiondoa iwe last option!
 
Labda uamue kutopenda tena vinginevyo hata kama ungejipa miaka 10 waweza kujikuta umeangukia pabaya zaidi ya mwanzo. Kikubwa ni kujitahidi kuchukuliana na kuvumiliana,kujiondoa iwe last option!
naweza kubaliana na wewe
 
ukomavu wa kisaikolojia ni wa taratibu kama ulivyo ukuaji wa kimwili!utatambaa,uta simama dede,utatembea na mwishowe utakimbia na hata kuruka!ndivyo ilivyo ukuaji wa kisaikolojia,utaumizwa hapa,halafu nawe utamumwiza yule,utalia kutengwa na mpenzi,au kuchukiwa na umpendaye,na muda mwingi kwa utoto wa kiakili yanapo tokea matatizo ya kimapenzi unahisi we ndiye mkosefu,mwenye madhaifu na usiye faa...kumbe wakati mwingine mpenzio ndio mwenye shida...kukomaa kiakili na kisha kisaikolojia kunataka muda,jipe moyo utayashinda

Asante. Umedadavua vzr.
 
unapoondoka si kwamba unakwenda kutafuta mpenzi, bali kwenda kuanza peke yako huku ukiwa Huru na mwenye furaha. BORA NJAA KWENYE AMANI KULIKO CHAKULA KWENYE VITA NA MANYANYASO
Ndugu yangu hakuna ombwe baya kama huna anayeutuliza mtima. Na sijui matamanio ya nafsi utayakidhi vipi manake usije ukaishia kupiga p*nyeto au kutafuta ashki bandia Sasa uhuru na furaha bila mapenzi utajikuta unachanganyikiwa na kuanza kuweweseka ovyo.
 
Mapenzi yakikutesa mlilie Mungu ndie ANAYEJUA YOTE
 
Ndugu yangu hakuna ombwe baya kama huna anayeutuliza mtima. Na sijui matamanio ya nafsi utayakidhi vipi manake usije ukaishia kupiga p*nyeto au kutafuta ashki bandia Sasa uhuru na furaha bila mapenzi utajikuta unachanganyikiwa na kuanza kuweweseka ovyo.
Mkuu kabla hujaingia huko unaweza kupiga mechi za kirafiki huku ukiangalia na kujijenga kwa safari ya peke yako
 
Mkuu kabla hujaingia huko unaweza kupiga mechi za kirafiki huku ukiangalia na kujijenga kwa safari ya peke yako
Kwa hiyo suala ni kuwa free-lancer au hit and run, nako kuna shida zake. Haifanani na ile uliomilikishwa kihalali
 
Kwa hiyo suala ni kuwa free-lancer au hit and run, nako kuna shida zake. Haifanani na ile uliomilikishwa kihalali
mkuu maandalizi ya kumiliki chako huanza katika hilo... Huwezi kuingia huko bila kuwa na uhakika nako. Unapoujua mlango wa kuingilia huwezi kuwa mgeni
 
mkuu maandalizi ya kumiliki chako huanza katika hilo... Huwezi kuingia huko bila kuwa na uhakika nako. Unapoujua mlango wa kuingilia huwezi kuwa mgeni
Hio onja onja huwa haina mwisho na wala sio maandalizi ya kumiliki. Utaonja wangapi mpaka uipate yenyewe?
 
Niliwahi kuwa kifungoni nikatoka ila sasa mahusiano yangu yananipa furaha ajabu.
 
Hayo mengine ni majaribu ndugu yangu cha muhimu mvumiliane na mrekebeshane taratibu naomba ujue somo la uvumilivu
 
Back
Top Bottom