hiram
JF-Expert Member
- Aug 1, 2013
- 266
- 393
Mwaka 1968 Yanga walichukua Ubingwa wa Ligi na kuiwakilisha nchi kwenye klabu bingwa barani afrika 1969.
Yanga walienda nchini Romania kufanya pre season ya mwezi mzima kitu kilichowafanya kufanya vizuri sana kwenye mashindano
Hatua ya awali.
Yanga wakakutana na fitarikandro ya Madagascar Yanga walishinda 4-0 na marudiano yanga wakafungwa 2-0 kuendelea
Raundi ya kwanza.
Yanga walikutana na Saint George ya Ethiopia wakatoka 0-0 mechi ya kwanza na mechi ya pili wakaipiga bila huruma saint george 5-0 na kuingia robo fainali moja kwa moja.
Hapa Yanga ikawa timu ya kwanza nchini Tanzania kuingia Robo fainali
Robo fainali
Yanga walikutana na Asante Kotoko na wakatoka sare 1-1 mechi zote mbili hatimaye ikaamuliwa irushwe shilingi ili iamue nani aende nusu fainali.
Makapteni wote wawili wakishuhudia shilingi ikarushwa hata hivyo kapteni wa Asante kotoko alifanya udanganyifu kwani kabla shilingi haijatua alijifanya kushangilia na kumfanya kapteni wa Yanga Abdulrahaman kuamini kuwa shilingi imeangukia upande wake.
Ndipo Yanga ikadhulumiwa nafasi ya kuwa timu ya kwanza kuingia nusu fainali, rekodi iliyokuja kuwekwa na watani zao Simba mwaka 1974.
kitwana Manara akaingia kwenye orordha ya wafungaji bora akiwa mfungaji bora namba tisa mwenye magoli mawili.
i
Yanga walienda nchini Romania kufanya pre season ya mwezi mzima kitu kilichowafanya kufanya vizuri sana kwenye mashindano
Hatua ya awali.
Yanga wakakutana na fitarikandro ya Madagascar Yanga walishinda 4-0 na marudiano yanga wakafungwa 2-0 kuendelea
Raundi ya kwanza.
Yanga walikutana na Saint George ya Ethiopia wakatoka 0-0 mechi ya kwanza na mechi ya pili wakaipiga bila huruma saint george 5-0 na kuingia robo fainali moja kwa moja.
Hapa Yanga ikawa timu ya kwanza nchini Tanzania kuingia Robo fainali
Robo fainali
Yanga walikutana na Asante Kotoko na wakatoka sare 1-1 mechi zote mbili hatimaye ikaamuliwa irushwe shilingi ili iamue nani aende nusu fainali.
Makapteni wote wawili wakishuhudia shilingi ikarushwa hata hivyo kapteni wa Asante kotoko alifanya udanganyifu kwani kabla shilingi haijatua alijifanya kushangilia na kumfanya kapteni wa Yanga Abdulrahaman kuamini kuwa shilingi imeangukia upande wake.
Ndipo Yanga ikadhulumiwa nafasi ya kuwa timu ya kwanza kuingia nusu fainali, rekodi iliyokuja kuwekwa na watani zao Simba mwaka 1974.
kitwana Manara akaingia kwenye orordha ya wafungaji bora akiwa mfungaji bora namba tisa mwenye magoli mawili.
i