Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Ni usiku tena muda wa kupumzisha mwili na akili, wengine huita nusu kifo kwakuwa unapolala fofofo hujui kwa hakika nini kinaendelea, ni muda huu ambapo kila mmoja kwa imani yake huomba ulinzi kwa Mungu au kile anachokiamini na kukiabudu!Hata Mimi mshana jr sipo mbali na wao au na nyie au na wewe.!Lakini pamoja na sale na maombezi yetu yote ibilisi shetani haachi kutusumbua kupitia kwa mawakala wake wachawi na wanga.
Sasa haya ni mambo upaswayo kufanya kulingana na imani yako;
-Sala na maombezi kwa Mungu mkuu huku ukitumia maji ya baraka, Rosary iliyoombewa na Bible
-Au kidunia zaidi ukifanya kila kitu kwa kinyume Kama kugeuza ndani nje au nyuma mbele nguo unazolala nazo
-Au kugeuza ndala au makubazi unapotoka kwenda maliwatoni
-Au kutoka kinyumenyume mlangoni na kuingia mlango wa maliwatoni kinyumenyume
-Kulala Kichwa chini miguu juu nk nk
Wanga na wachawi ni watu wa kinyume, hutenda kinyume na hata matokeo yake huwa kinyume.Kwahiyo ukitaka kuwakomesha na kuwadhibiti nawe tenda kinyume ila fanya hivyo inapobidi
Hivi unajua ni kwanini wachawi na wanga wote waangukao safarini huwa uchi? Hii ni kwasababu ya kutenda kinyume na mazoea
Hivi unajua ndani ya ule ungo, wasafiri huangalia walikotoka na sio waendako? Kwenye kanuni za usafiri hili ni kinyume na mazoea
Hivi unajua kwanini wanga na wachawi wawapo angani safarini hawapigi story? Hii ni kinyume na mazoea Haiwezekani msafiri pamoja wengi Halafu mshindwe hata kusalimianaHivi unajua ni kwanini kwenye kusafiri ardhini hutumia fisi na angani hutumia ungo?
Bado ni mule mule. Katika hayawani wote wa Ulimwengu huu fisi anashika namba moja.Kumtumia Kama chombo cha usafiri ni kutenda tofauti na mazoea ungo kazi yake ni kupepeta nafaka unapotumika Kama chombo cha usafiri ni kukengeuka mazoea.
Lala ukijua kuna watu ni wakati wao kufanya yao wakifanya tofauti na kawaidaukisoma post hii na ukiona kuna dalili za kusumbuliwa dawa yake nawewe ni kutenda kinyume cha mazoea, kinyume cha kawaida kama wao Watakoma kukusumbua.
Sasa haya ni mambo upaswayo kufanya kulingana na imani yako;
-Sala na maombezi kwa Mungu mkuu huku ukitumia maji ya baraka, Rosary iliyoombewa na Bible
-Au kidunia zaidi ukifanya kila kitu kwa kinyume Kama kugeuza ndani nje au nyuma mbele nguo unazolala nazo
-Au kugeuza ndala au makubazi unapotoka kwenda maliwatoni
-Au kutoka kinyumenyume mlangoni na kuingia mlango wa maliwatoni kinyumenyume
-Kulala Kichwa chini miguu juu nk nk
Wanga na wachawi ni watu wa kinyume, hutenda kinyume na hata matokeo yake huwa kinyume.Kwahiyo ukitaka kuwakomesha na kuwadhibiti nawe tenda kinyume ila fanya hivyo inapobidi
Hivi unajua ni kwanini wachawi na wanga wote waangukao safarini huwa uchi? Hii ni kwasababu ya kutenda kinyume na mazoea
Hivi unajua ndani ya ule ungo, wasafiri huangalia walikotoka na sio waendako? Kwenye kanuni za usafiri hili ni kinyume na mazoea
Hivi unajua kwanini wanga na wachawi wawapo angani safarini hawapigi story? Hii ni kinyume na mazoea Haiwezekani msafiri pamoja wengi Halafu mshindwe hata kusalimianaHivi unajua ni kwanini kwenye kusafiri ardhini hutumia fisi na angani hutumia ungo?
Bado ni mule mule. Katika hayawani wote wa Ulimwengu huu fisi anashika namba moja.Kumtumia Kama chombo cha usafiri ni kutenda tofauti na mazoea ungo kazi yake ni kupepeta nafaka unapotumika Kama chombo cha usafiri ni kukengeuka mazoea.
Lala ukijua kuna watu ni wakati wao kufanya yao wakifanya tofauti na kawaidaukisoma post hii na ukiona kuna dalili za kusumbuliwa dawa yake nawewe ni kutenda kinyume cha mazoea, kinyume cha kawaida kama wao Watakoma kukusumbua.