Jinsi ya kutafuta hela

Jinsi ya kutafuta hela

laii

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2016
Posts
853
Reaction score
1,120
Tafuta hela kwa nguvu zako zote, sana sana ukiwa kijana, ukiajiriwa au ukijiajiri fanya kazi kwa bidii bila kusahau kumshukuru Muumba kwa sala na zaka.

Tafuta hela kama muuza machungwa anayeyamenya na hajui mteja atakuja saa ngapi?

Kama mkaanga chips, mihogo, samaki, maandazi na hajui wateja watatoka wapi?

Mtembea bure si sawa na mkaa bure, atafutae hachoki, haba na haba hujaza kibaba.

Bila kusahau kuwa na matumizi kiasi, usinunue kitu ambacho hukukipangia bajeti.

Bandu bandu humaliza gogo.

Wasalam
 
Tafuta hela kwa nguvu zako zote,sana sana ukiwa kijana,ukiajiriwa au ukijiajiri fanya kazi kwa bidii bila kusahau kumshukuru Muumba kwa sala na zaka.
Tafuta hela kama muuza machungwa anayeyamenya na hajui mteja atakuja saa ngapi?
Kama mkaanga chips,mihogo, samaki,maandazi na hajui wateja watatoka wapi?
Mtembea bure si sawa na mkaa bure,Atafutae hachoki,haba na haba hujaza kibaba.
Bila kusahau kuwa na matumizi kiasi,usinunue kitu ambacho hukukipangia bajeti. Bandu bandu humaliza gogo.
Wasalam
Jinsi ya kutafuta hela na kuzifanya zisikukimbie .....

Suggested heading
 
Tafuta hela maana hamna siku hela itakutafuta wewe..tafakari chukua hatua
IMG-20181022-WA0049.jpeg
 
Ha ha ha ha,ni biashara gani unaweza kuwekeza kidogo (input) ukapata kikubwa (output),mfano ukawekeza 50,000 ukapata 100,000?......utafutaji na uvumilivu ni silaha namba moja ya kupata fedha ikimaanisha unawekeza kingi lakini kinakuja kidogo.
 
Kilichomtambulisha Mo,baresa,mengi kwa watanzania karibia mamilioni,si haiba yake,si matendo na kazi zake tu kikubwa ni pesa aliye nayo. .so tufunge mkanda tutafute pesa kwa nguvu zetu,bila kusahau kumwomba Mungu
Screenshot_2018-09-26-15-29-47.jpeg
Screenshot_2018-10-19-20-47-01.jpeg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom