Jinsi ya kupika keki ya zabibu kavu

TIMING

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
24,593
10,893
JINSI YAKUPIKA KEKI YA ZABIBU KAVU




keki.jpg




Tengeneza keki ya zabibu kavu kisha ongezea ladha mbali mbali kutokana na upendavyo fata maelekezo hapo chini
Mahitaji:
= 240gram zabibu kavu
= 240garm maziwa ya maji
= 240garm siagi (butter)
= ½ chumvi kijiko kidogo cha chai
= 240gram sukari
= 240gram korosho au walnuts au karanga chochote ulichonacho
= 500gram unga wa ngano
= 1 kijiko kidogo cha chai baking soda (Baking powder)
= 2 mayai

JINSI YAKUTENGENEZA

1. Washa oveni yako katika joto 325 degree F (165 degree C) kisha kipake chombo chako siagi utakacho tumia kuokea keki yako.

2. Chukua bakuli changanya unga wa ngano, zabibu na baking soda kasha weka pembeni.

3. Chukua bakuli nyingine weka siagi na sukari ndani kisha piga mapaka ichanyanyike vizuri na kua laini kabisa kisha vunjia mayai ndani piga paka mchanganyiko wako uwe laini kabisa.

4. Kisha chukka mchanganyiko wa unga mimina kwenye mchanganyiko wa mayai changanya pole pole mpaka upate mchanganyiko mzito wa wastani kama itakua nzito sana ongeza maziwa kama itakua nyepesi sana ongeza unga.

5. Kwa kuongeza ladha unaweza kuongezea vitu hiyo hapo chini.
= ½ kijiko kidogo cha chai kungu manga ya unga (nutmeg)
= ½ kijiko kidogo cha chai Mdalasini ya unga (cinnamon)
= 1 kijiko kidogo cha chai vanilla ya maji

6. Kisha mimina mchanganyiko wako wa keki kwenye chombo utakachotumia kuokea na oka kwa dakika 40 hadi 45 kwa moto ule ulioelekezwa pale juu kama oven yako inamoto mkali zaidi unaweza choma kwa dakika 30 ila hatari ya kuunguza na keki isiive kati kati ni kubwa sana.

7. Baada ya dakika 40 chukua toothpick choma keki yako katikati toa angalia kama itakua kavu basi keki yako imeiva kama itakua na maji maji keki yaki bado haijaiva hivyo iache katika oven kwa muda kidogo kisha angalia tena.

8. Toa keki yako iache ipoe tayari kwa kuliwa.
 
Thanx ndg yng! Afadhal umeamua ku2letea maujuz yko! Tehe, tehe, tehe! Ubarikiwe sn!
 
keki.jpg


Mahitaji:

  • 40gram zabibu kavu
  • 240garm maziwa ya maji
  • 240garm siagi (butter)
  • ½ chumvi kijiko kidogo cha chai
  • 240gram sukari
  • 240gram korosho au walnuts au karanga chochote ulichonacho
  • 500gram unga wa ngano
  • 1 kijiko kidogo cha chai baking soda (Baking powder)
  • 2 mayai

Jinsi ya kutengeneza
Washa oveni yako katika joto 325 degree F (165 degree C) kisha kipake chombo chako siagi utakacho tumia kuokea keki yako.

Chukua bakuli changanya unga wa ngano, zabibu na baking soda kasha weka pembeni.

Chukua bakuli nyingine weka siagi na sukari ndani kisha piga mapaka ichanyanyike vizuri na kua laini kabisa kisha vunjia mayai ndani piga paka mchanganyiko wako uwe laini kabisa.

Kisha chukua mchanganyiko wa unga mimina kwenye mchanganyiko wa mayai changanya pole pole mpaka upate mchanganyiko mzito wa wastani kama itakua nzito sana ongeza maziwa kama itakua nyepesi sana ongeza unga.

Kwa kuongeza ladha unaweza kuongezea vitu hiyo hapo chini.

½ kijiko kidogo cha chai kungu manga ya unga (nutmeg)

½ kijiko kidogo cha chai Mdalasini ya unga (cinnamon)

1 kijiko kidogo cha chai vanilla ya maji

Kisha mimina mchanganyiko wako wa keki kwenye chombo utakachotumia kuokea na oka kwa dakika 40 hadi 45 kwa moto ule ulioelekezwa pale juu kama oven yako inamoto mkali zaidi unaweza choma kwa dakika 30 ila hatari ya kuunguza na keki isiive kati kati ni kubwa sana.

Baada ya dakika 40 chukua toothpick choma keki yako katikati toa angalia kama itakua kavu basi keki yako imeiva kama itakua na maji maji keki yaki bado haijaiva hivyo iache katika oven kwa muda kidogo kisha angalia tena.

Toa keki yako iache ipoe tayari kwa kuliwa.
 
nilikuomba recipe ya rockburns......ujue nakusubiria mwenzio nitakosa mshiko?

The uje na recipe ya nyama ya foil, nimpikie husband jumamosi.....
 
nilikuomba recipe ya rockburns......ujue nakusubiria mwenzio nitakosa mshiko?

The uje na recipe ya nyama ya foil, nimpikie husband jumamosi.....

Tatizo hunikumbushi badili tabia maana mwenzako nina mambo mengi kama kuku wa kizungu. Anyway nitajitahidi kukumbuka.
 
Kumbe wewe mpishi mzuri? Si ungepeleka food corner kabisa? Thanx for the. Recipe!

Yes maam. I love to cook very much. I would love to but tatizo kule food corner watu hawatembelei sana. Thread yangu ya itakaa huko hadi itaoza bila ya watu kuisoma.
 
Kweli tunahitaji jukwaa la mapishi. Ile thread ya food corner naitafutaga hadi nachoka! Thanks young master.
 
Aisee Arifu wewe kweli fulu Mavipaji,, hadi kupika umo!!
Hebu na mimi nifundishe namna ya kupika japo Pilau aisee..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom