Jinsi ya kuondoa madoa na mabaka mwilini

Jinsi ya kuondoa madoa na mabaka mwilini

Habari wapendwa!

Naomba kuuliza aina ya dawa au mafuta yakutoa mabaka baka ya cream kwa mwanamke kama ikimkata, asante na dada anatatizo hilo.

Tumia Zikuuzoka cream (kama ni mweupe atumie ile iliyoandikwa lightening akiwa Maji ya kunde atumie iliyoandikwa cream tu. Pia kama unaweza nitafute kesho nikiwa dukani kwa kuni quoite tu maana taona kiurahisi zaidi nikuonyeshe nyingine. NB: mabaka hayo kama amezaliwa nayo hayatatoka ila kama yamekuja kwa sababu mbalimbali yatatoka.
 
pimples.jpg


Jamani ndugu zangu, dada yenu ninakuja kwa heshima kubwa kuomba msaada wenu, japo wa mawazo tu nimetokewa na mabaka meusi usoni (katika mashavu) mabaka hayo yamechanganyika na chunusi mwaka wa tatu sasa.

Nimejaribu kutumia dawa na vipodozi mbalimbali lakini sijaona mafanikio yoyote miongoni mwa madawa/vipodozi nilivyotumia ni sonaderm cream, Safi cream, epiderm cream, bidhaa za Forever Living, bidhaa za Oriflame, bidhaa za Grace (Zoazoa), asali na mayai na nyingi nyingi nyingi.

Pamoja na kutumia madawa na vipodozi hivyo, bado tatizo lipo pale pale ninaleta kwenu tatizo langu, nisaidieni. Maana ninaanza kuichukia sura yangu nitumie dawa gani nipo tayari kwa bajeti yoyote
 
Picha hazifunguki lakini ikijiangalia una ngozi ya aina gani dry, normal combination au oily?
 
pole sana,nenda kamuone dr wa ngozi;TMJ HOSPITAL
Nashukuru sana. Nitaenda ila niliwahi kwenda kwa Kairuki nikapewa cream flani hivi ambayo nayo haikunisaidia.

Nikaelekezwa kwa wakongo fulani kuwa wao wanatengeneza dawa ya asili nikatumia dawa zao, pia hazikunisaidia
 
Nashukuru sana. Nitaenda. Ila niliwahi kwenda kwa Kairuki nikapewa cream flani hivi ambayo nayo haikunisaidia.

Nikaelekezwa kwa wakongo fulani kuwa wao wanatengeneza dawa ya asili. Nikatumia dawa zao, pia hazikunisaidia

Au umri shosti maana kuna stage ukifikia unanawiri kidogo mafuta yanajaa mwilini.
 
Pole.....vizuri ukamuone dr wa ngozi.....
Ila pia kuna mahali unakosea......hivyo vyote ulivyopaka kujitibu ni kwa ajili ya oily skin.....?.....
Kweli eeeh!! Kwa hiyo nilitakiwa nipake vya dry skin? Au combination ya oily na dry!!!?
 
Mimi niliwahi kuwa na chunus nyingi sana kipindi nipo advance nilikuwa natumia kila aina ya madude ili niwe kawaida ila sikuwah kupata matokeo yoyote mazuri.

Baada ya hapo nilibadili life style tu nilaacha kuogea sabun yoyote ya kunukia nukia( Sijui kiurembo zinaitwaje) .

Nikaanza kuogea sabun ya magadi au jamaa kila siku asubuh na jion na kabla ya kulala nilikuwa naosha sura kwa sabun hyo halafu napata tube nija inaitwa spot remover.

Mafuta yangu ya uson mpaka sasa n vesselin napaka asubuh na jion kama nipo dar kwenye joto ila kama n kwenyw barid huwa nayachanganya na hyo spot remover kila asubuh na usiku nikioga.

Hakika sura yangu imebadilika sina tena hayo mapele ninaeweza kukutumia picha kwa ushahd wa hilo ila ni vizuri pia ukawaona wataalamu wa afya ya ngozi

NB. MPANGO HUU NI USON TU ...
 
Au umri shosti.......?.....maana kuna stage ukifikia......unanawiri kidogo mafuta yanajaa mwilini......
Nina miaka 30 sasa hili tatizo lilinipata nikiwa na miaka 27 hadi sasa
 
Kutokana na kuapply a lot of chemicals hadi sasa,nadhani,u should give a break to your face kwa muda hivi nadhani huenda ikasaidia. Inaonesha inakukera sana uso huupumzishi,safisha uso kwa maji vuguvugu na sabuni zisizo na kemikali kisha upake mafuta ya nazi asubuhi na jioni.
 
Kweli eeeh!! Kwa hiyo nilitakiwa nipake vya dry skin? Au combination ya oily na dry!!!?

Unatakiwa upake vitu vya oily skin ukiongeza mafuta juu ya ngozi yenye mafuta inablock pores na ndio chunusi zinazidi tafuta cleanser toner (kwa ajili ya kutight hizo pores zisiingize uchafu) halafu cream ya oily skin usipake lotion au kunawia sabuni ya marashi usoni osha uso kwa maji baridi au vuguvugu lakini sio Moto usitumbue chunusi zinaacha mabaka tumia extractor kuzitoa.
 
Pole dada zingatia ushauri/maelekezo ya specialist wa ngozi ukipewa dawa ukatumia alafu haijakusaidia unaridi kwa aliekupa hizo. Too much trials is not healthy
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom