Jinsi ya kumuweka mume wako kiganjani

Jinsi ya kumuweka mume wako kiganjani

Mkunde Original

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2013
Posts
807
Reaction score
647
Habari zenu wamama, wadada aka wenye P.O.BOX zao mjini (refer lara1)

Nilikuwa likizo wiki mbili zilizopita (nilikuwa mkoa mmoja hivi mpakani mwa Tanzania) nikakutana na hiki kisa katika gathering na wenyeji wangu, sasa nimeona nije niwashirikishe wadada wenzangu.
Habari yenyewe ilikuwa hivi,
Mmmoja wa watu waliokuwa katika hiyo gathering alinyanyuka na kusema hivi:

Jamani ngojeni niwape habari ya kuboresha mapenzi kwa waume zenu hata mkawa mmewaweka kwenye viganja na unamshika utakavyo bila mwanamke yeyeote kumsumbua na kumrubuni mumeo.
1. Mume kama mume anachoka kitu kimoja au hikohiko kila siku hivyo anataka mabadiliko, sio tu kwenye chakula kwenye kila kitu kinachohusu nyumba hivyo ni jukumu lako mama/mke kuwa na mabadiliko hayo.

2. Mke kama ulizoea kuvaa suruali mara kwa mara hebu uwe unabadilisha mara moja moja na kuvaa sketi fupi usawa wa magoti iwe ya kubana kidogo (hakikisha mumeo anaona mabadiliko hayo). Kama ulikuwa wa kuvaa sketi ndefu basi siku hiyo vaa pensi usawa wa magoti (mkiwa nyumbani kwenu na si vazi la kazini) hakikisha mumeo anakuona hii huleta hamasa ya kutaka kujua mke wangu kesho atatokaje hivo kumuongezea hamasa ya kukuangalia kila siku.

3. Unajua tabia za haose girl nyumbani kwako anapomuhudumia mumeo au hata anapowahudumua wewe na mumeo, mfano anavowaandalia chakula na kuwakaribisha, anavokuwa amevaa, sauti na lugha yake anapoongea na nyie. (hapa ni kuwakamata waume wanaotamani kutoka/kutembea na housegirls) siku moja moja hasa week end ondosha watu wote nyumbani kwako na ubaki wewe na mumeo kisha vaa kama haouse girl (like kanga ya lubega kiblose simple na sketi simple) anza kumkaribisha mumeo karibu kuoga (kwa sauti ya kinyalu) mnisamehe wanyalu si kwamba housegirl wote ni wanyalu.
Huku ukiwa unajibinya vidole kama mto mwenye woga unamuita mumeo, samahani shemeji chai tayari na kagoi kwa mbali cha heshima. Hapa mumeo lazma akutizame na hakikisha siku hiyo hatoki.
Akiwa anakunywa chai unamwambia samahani shemeji naomba nikakusaidie kutandika kitanda, akikuruhusu unakimbia mbio huku unatandika kwa mikao ya kimitego mitego lazima aje akuchungulie leo nini kimekupata hapo ataona mikao yako ya kimitego ukitandika kitanda ukimaliza unamtaarifu chumbani pako tayari shemeji(hii unajifanya wewe ni house girl na akili yake itawaza u r a house girl so anapata huduma tofauti).

Mtu huyo aliendelea kuelezea kuwa wanaume akili zao huwa zinawaza kitu kilichopo mbele yake na si cha baadae sana hivo ukifanikiwa kuiteka akili yake kwa wakati huo ndo umemnasa. Mwanaume pia hapendi kuambiwa kuwa amekosea hata kama amekosa hivo mke usipende sana kumwambia mumeo makosa yake hata kama amekosa, ikibidi unatumia lugha ambayo hatajisikia vibaya.
Kila siku umpende na kumjali mumeo tuu hata kama yeye hakurudishii mapenzi hayo vile wewe unamuonesha.

4. Siku nyingine unakuwa baa medi wewe mke ndio na siku hiyo unampa ofa mumeo akiwa nyumbani kwenu. Mke unavaa kama baa medi wanavovaa kisha baada ya mlo unaanza kumkatia kanywaji na ukiwa nae mezani wewe usinywe sana ili uweze kumuhudumia, unafanya kama baa medi wanavofanyaga, unamkaribisha kinywaji na baada ya bia mbili tatu unamuomba kukaa nae muongee obvious atakubali. Hapo nawe unaomba uagize kinywaji kimoja akulipie (kumbuka unafanya kama uko baa ila uko nyumbani kwako) lengo ni kumteka mume akili asikuone kama mke akuone kama baa medi na unampa huduma zote za baa medi. Ili kesho yake ukirudi kuwa kama mke anakuwa ameshabadili mtazamo wa kuwa mke wangu nimemkinahi.
Akikuruhusu kukununulia kinywaji hunywi kwanza unaka tuu nakuanza kustorisha nae habari za kawaida tuu za kitaa au za maisha. Akikuuliza mbona hunywi kinywaji nilichokununulia unamwambia ntakunywa baadae niko kazini, hapo unakuwa umezidi kumteka kiakili na anakuwa anajiuliza niko baa niko nyumbani, kwakuwa kanywaji katakuwa kamemtembelea vizuri tayari atakubembeleza tuu kunywa bana hata moja tuu hutalewa maana wanywaji huwa wanapenda kampani ya kunywa. (waweza mtolea sababu kinywaji ulichoninunulia nimelipia short ya jana hivo siwezi kunywa, atakununulia kingine) kunogesha uhalisia wa baa ukiwa nyumba

5. Siku nyingine unakuwa mama ntilie, pata vionjo vyo te wanavyofanya mama ntilie kuwakaribisha wateja wao kisha nawe umkaribishe mume kwa staili hiyo.

Wenyeji wa hilo eneo waliendelea kuelezea mengi ila haya ndo yalinikodolesha masikio nikaona niwashirikishe wenzangu.

Kazi kwenu wadada wenye waume na P.O.Box zao
Valentine njema wapendwa wote.
 
Kuzaliwa mwanaume raha sana nakushukuru Muumba kwa kuniumba Mwanaume.
 
Wengine sisi ni
Kunguru,hatufugiki,hata tupewe au tufanyiwe nini,tutarudi tu porin
tukipata nafasi(tunahitaji maombi, honestly)
Yaani sijui nicheke au tu nikupe saluti kwa kuwa mkweli! Tutakuombea lakini ni muhimu ujiombee na wewe
 
Hayo yote yanajulikana, kwenye utekelezaji ndiyo wanapata division 5.
 
Sipendi kumuweka kiganjani, napenda mishemishe ili kukeep relationship exciting.
Napenda ile hofu ya anytime he can be taken au kupigwa chepuo. Inafanya game ya mapenzi iwe tait hivi. Mara mbona unamchekea Rose, mara nambana bana, mara ana confess she was hitting on him.
Nalia lia pale, ananibembeleza, akipiga mechi ya baby am sore, uuwiii ni dk 90 za maana lazima aseno apigwe 5.

Nini kumweka mtoto wa watu kiganjani awe zezeta? Atashindwa hata tafuta pesa bure.
 
hivyo kwa wanaume wengi Not Applicable kabisa, tunataka kuona sura mpya hata kama ni mbaya kuliko ya mkeo, Mtu ashakujaza stress miaka nenda rudi anawezaje kukusahaulisha stress kwa kujifanya baa medi wa nyumbani, au housegirl wakati tunajua fika ni fake characters hapo. labda huko kwenye mikoa ya mpakani ulikoikuta ila hapa kwa ------ NOT APPLICABLE
 
Sipendi kumuweka kiganjani, napenda mishemishe ili kukeep relationship exciting.
Napenda ile hofu ya anytime he can be taken au kupigwa chepuo. Inafanya game ya mapenzi iwe tait hivi. Mara mbona unamchekea Rose, mara nambana bana, mara ana confess she was hitting on him.
Nalia lia pale, ananibembeleza, akipiga mechi ya baby am sore, uuwiii ni dk 90 za maana lazima aseno apigwe 5.

Nini kumweka mtoto wa watu kiganjani awe zezeta? Atashindwa hata tafuta pesa bure.

Njoo nikuoe tena.
 
Mmmh! Nimependa hapo pa hauzgelo!! ofkoz creativity katika ndoa ni jambo la msingi sana kwa wanawake katika kudumisha ndoa mana wao ndio wajenzi wakuu wa familia. Ila wanawake wa siku hizi walivyobize kutafuta pesa mmmmmh! Sijui!! Wangu ntamfunga kamba miguuni kila akirudi nyumbani haki vilee!!
 
Back
Top Bottom