Jinsi ya kumbaini Mganga tapeli

Jinsi ya kumbaini Mganga tapeli

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
2,144
Reaction score
3,459
Utamjuaje Mganga Taperi.

1) Muonekano wa Nje
Ukiona mganga amevaa matunguri mengi kwenye mwili wake huyo sio mganga amini,Hana uwezo wa Kufanya mambo makubwa huyo, Mganga kabisa Huwezi kukuta Amevaa kitu chochote au hata kama akivaa basi nikitu kimoja tu kiasi kwamba hata akipita hapa Huwezi Ukamjua.

Mganga anae vaa matunguri mengi ni taperi kwa sababu yeye tu ameshindwa kuipangilia mizimu yake ikubali asivae hayo mazaga ,Ataweza kukuagua wewe.😆✍️

Ujue waganga hua mizimu inapanda mixer majini ,Anaambiwa avae kitu flani na Flani Lakini sasa ,Hapo mganga atatakiwa apelekwe na yeye kwa mganga ili ,ile mizimu ikapangiliwe katika mpango sahihi ili iweze kutulia na Kufanya kazi kwa weledi.

Au yeye mwenyewe anatakiwa apambane kuhakikisha mizimu inatulia na kukaa katika mpangilio sasa kama yeye imemshinda ikalazim akae amevaa mazaga zaga mengi wew atakuwezea wapi?

Kila mganga nae ana mganga wake ,iko hivo Wanazidiana Ujuzi na maarifa ,kwahio hua wanaachana Madaraja.

2) Maneno Mengi
Mganga wa kweri hua hana maneno mengi ,wala Hua hajisifu akiongea maneno moja mawili imetosha.

3) Kwenye kutoa Dawa
Mganga wa kweri Dawa ambazo hua Anatoa nitudawa kidogo sana ,kwanini kidogo ,kwa sababu Dawa zake nizagharama Amechimba miti na ameweka vizimba humo.

Vizimba ni nini
Vizimba ni vitu vya kuchanganyia kwenye Dawa ili ifanye kazi kwa weledi Mfano wamechimba mizizi ya Mkwaju sasa ikiwa ivo ivo haiwezi kufanya kazi inabidi ,Liwekwe Kende La Simba au Kende La kasongo Sasa unalipataje? Hapo ndopo Pesa inahitajika. Kende likipatikana litachomwa moto au linakaushwa linasagwa unapatikana Unga wake ambao unachanganywa kwenye mti husika.

4) Kwenye Bei na Malipo
Mganga wa kweri Hajawai kua na Bei ndogo ,Unaenda kwa mganga anakuomba Laki 1 ili akupe Utajiri😆Utajiri wa laki moja we hushtuki Mganga wa kweri na Mkubwa Kumuona Tu kwanza kipengere,Bei sasa Utaskia Leta M2 au M10.

5) Maisha ya mganga
Unakuta mwamba Anatembelea Gari Tak-o la nyani Au anatembelea Kuruga,Au masediz Benz nyumbani kwake ukifika Nyumba Kari ,Pako safi Simanishi Wasio na maisha mazuri hawana Dawa za kutibu hapa ila wengi wao wanakua Mataperi hawana uwezo kidawa ndio maana hata mafanikio
Chakumalizia Tu ni kwamba Usiache kwenda kwa waganga we nenda; usione aibu kwenda eti watu watakuonaje, Pigwa chale, Oga dawa Fanya matambiko, Roga unavyoweza mambo yatakua🔥

Tawile 👴🏾


IMG-20260130-WA0557.jpg
 
Baba utapel ni nini!! Mbona kama unapalia tupigwe zaid hakuna mganga wa kwel atakuomba hela akupe utajir coz huwa wanajiamin na kaz zao anaweza kupa dawa bure ila zingua uone nimejionea kwa macho yangu matapel ndio wanaopenda kukuomb hela kabla ya kaz kijana mwenzangu wa kitanzania ogopa waganga wa 2010 hadi 3000 utapigika kwerikwer hakuna ukwel utachakaa
 
Baba utapel ni nini!! Mbona kama unapalia tupigwe zaid hakuna mganga wa kwel atakuomba hela akupe utajir coz huwa wanajiamin na kaz zao anaweza kupa dawa bure ila zingua uone nimejionea kwa macho yangu matapel ndio wanaopenda kukuomb hela kabla ya kaz kijana mwenzangu wa kitanzania ogopa waganga wa 2010 hadi 3000 utapigika kwerikwer hakuna ukwel utachakaa
Sasa kama umesaidiwa kwann umzingue mganga,nae anapiga ubaya ubwela 🤣🤣
 
Zamani walikuwa wanasema Uganga hauuzwi ila unaweza kurudisha shukrani, changamoto ni masharti yake ni magumu sana kuyatimiza.
 
Mganga hasaidii kitu... Mganga feki na mganga wa kweli, wote ni matapeli... Msaaada wa mtu upo kwa mtu mwenyewe
 
Kama ulienda kumjalibu anakuwai vile vile 🤣🤣
Hapana mkuu. Mfano mganga ameona shida yako ni kubwa na yeye hawezi kuitatua au anaweza ila anaona ni nzito mno kwahiyo atakufanyia tiba pale ambayo anajua kabisa sio suluhisho la tatizo lako kisha atachukua hela yako na hatokwambia ukweli.

Maana unakuta mteja pesa yake ndogo na tatizo lake kubwa mganga hawezi kumtibu kwa kiasi hicho cha pesa, sasa badala akwambie ukweli yeye anaamua kuchukua tu pesa yako kwa kukupa tiba isiyo sahihi kwa tatizo lako.
 
Hapana mkuu. Mfano mganga ameona shida yako ni kubwa na yeye hawezi kuitatua au anaweza ila anaona ni nzito mno kwahiyo atakufanyia tiba pale ambayo anajua kabisa sio suluhisho la tatizo lako kisha atachukua hela yako na hatokwambia ukweli.

Maana unakuta mteja pesa yake ndogo na tatizo lake kubwa mganga hawezi kumtibu kwa kiasi hicho cha pesa, sasa badala akwambie ukweli yeye anaamua kuchukua tu pesa yako kwa kukupa tiba isiyo sahihi kwa tatizo lako.
Uyu anatamaa naingia kwenye matapeli
 
Back
Top Bottom