JINSI YA KUJUA UJAZO WA FREEZER

JINSI YA KUJUA UJAZO WA FREEZER

Mayova

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2018
Posts
231
Reaction score
217
Ndugu zanngu mambo vip?
Kumekuwa na upigaji mwingi sana kwenye biashara za mafriji hasa mafriza. Wengi tunauziwa mafriza tunaambiwa freezer hilo ni ujazo fulani kumbe sio. Mfano unaweza kuambiwa freezer lina ujazo wa lita 100 kumbe ni lita 50. Naomba mwenye utaalamu wa kujua ujazo wa mafreezer au jinsi ya kusoma ujazo wa freezer atupatie uzoefu. Ahsanteni sana
 
Ndugu zanngu mambo vip?
Kumekuwa na upigaji mwingi sana kwenye biashara za mafriji hasa mafriza. Wengi tunauziwa mafriza tunaambiwa freezer hilo ni ujazo fulani kumbe sio. Mfano unaweza kuambiwa freezer lina ujazo wa lita 100 kumbe ni lita 50. Naomba mwenye utaalamu wa kujua ujazo wa mafreezer au jinsi ya kusoma ujazo wa freezer atupatie uzoefu. Ahsanteni sana
sticker ya kampuni inaandika lita 50 --- muuzaji anasema lita 100


hatari sana
 
Kuna njia kama tatu za haraka haraka;

1. Kusoma label

2. Kujaza maji mwenyewe kwa vipimo kama ndoo au dumu ambalo unajua ujazo wake.

3. Kwa njia ya mahesabu kwa maana kupima urefu, upana na kina. Mfano
Ujazo (litres) = Urefu (cm) × Upana (cm) × Kina (cm) gawanya kwa 1000

👉 Kwa mfano:

Urefu = 80 cm

Upana = 60 cm

Kina = 50 cm


80 × 60 × 50 = 240,000 cm3

Chukua 240,000 gawanya kwa 1000 = 240 litres.

Kwa freezer hili litakua na ujazo wa lita 240.
 
Kuna njia tatu.
1. Kusoma label

2. Kujaza maji mwenyewe kwa vipimo kama ndoo au dumu ambalo unajua ujazo wake.

3. Kwa njia ya mahesabu kwa maana kupima urefu, upana na kina. Mfano
Ujazo (litres) = Urefu (cm) × Upana (cm) × Kina (cm) gawanya kwa 1000

👉 Kwa mfano:

Urefu = 80 cm

Upana = 60 cm

Kina = 50 cm


80 × 60 × 50 = 240,000 cm3

Chukua 240,000 gawanya kwa 1000 = 240 litres.

Kwa freezer hili litakua na ujazo wa lita 240.
Utaenda kuhakiki dukani na hayo maji!
 
Back
Top Bottom