Kama mnavyo jua changamoto za maisha zimetufanya tuwe mbali na familia zetu, hivyo yanapo kuja mambo muhimu ambayo yanahitaji usaidizi wa kifamilia imekuwa shida sana kwa vijana wengi.... Mimi ni kiwa kama kijana ambaye nahitaji kuwa na mwenza wangu wa maisha nimepitia katika kipindi kigumu sana hasa cha kupata watu wakaribu ambao watanisaidia kufanikisha jambo ili..
Nahitaji kupeleka barua ya posa kwa wazazi wa mchumba wangu, tatizo nililokumbana nalo ni watu wakaribu yangu ambao wanaona ili swala kama vile ni kubwa mna, Kabila langu ni mchaga mila na desturi zetu zinatofautiana na baadhi ya makabila ya hapa Tanzania hasa kwenye swala la kuposa binti.
Mila zetu ni kwamba unatafuta wazee watatu mnawatuma kwenda kwa wazazi wa binti wakiwa na Soda au Mbege, na wakifika kule watajieleza wenyewe kwajinsi wanavyo jua na baada ya hapo watajibiwa na wazazi wa binti na kupangiwa mahari na baada ya hapo wanarudi kukujulisha...
Mchumba wangu ni Mnyaturu, kwa mujibu wa mchumba wangu ameambiwa na wazazi wake natakiwa niandike barua ya posa ikiwa na kishika uchumba, ambapo itapelekwa na watu wazima kama wa 3 hivi.. Hapo ndipo palipo nipa mtihani kidogo, kwamba hiyo barua inaandikwa vipi? nimejaribu kuongea na ndugu zangu wameniambia wao hawakupitia utaratibu wa kuandika barua bali walituma watu tu...
Jamani naombeni mnifungue macho kwa maelekezo wa jinsi ya kuandika hiyo barua..
Kwa mujibu wa thread moja humu JF imenipa mwaga kidogo,
Kujitambulisha kwa wazazi wa binti ina maana ifuatayo:
1. Unapeleka posa rasmi kwa wazazi wa binti kuwa unamchumbia binti yao na siku si nyingi utafunga naye ndoa
2. Kujitambulisha na kupeleka posa rasmi unatangaza kwamba sasa umeji-commit kwa huyo binti na utatambuliwa rasmi na familia pamoja na ukoo mzima wa upande wa binti.
Kujitambulisha kunaambatana na kupangiwa mahari (kulingana na taratibu za kabila husika)
3. Ukishapangiwa mahari utatoa sehemu ya hiyo mahari au yote siku hiyohiyo (kutegemeana na taratibu zao), unatakiwa kufanya homework kabla hujaenda ili kujua mahari ikoje au inahusisha mambo/vitu gani.
Mambo muhimu ya kuzingatia:
1. Usiende wewe peke yako au vijana wa rika yakeo pekee
2. Unatakiwa uende na mzazi wako au mzazi mlezi au mwakilishi wa mzazi wako ambaye ana umri sawa na baba yako mzazi atakayekuwa mzungumzaji kwa niaba yako, wewe utatambulishwa kwa wazazi wa binti na huyo mzazi wako. Pia andaa mtu mwingine atayekuwa mshenga wako, atakayekuwa anawasiliana na familia ya binti pale kutakapokuwa na ulazima wa kufanya hivyo.
3. Kujitambulisha ni tukio kubwa kwa upande wa wazazi wa binti, hivyo usiende kwa kushtukiza, mwambie binti awaambie wazazi wake kuwa kuna ugeni muhimu unakuja siku fulani kwa shughuli fulani (kadri utakavyokuwa umepanga), maana familia nzima, ndugu na ukoo wa binti utajiandaa kuwapokea, hakikisha unaenda siku hiyo.
4. Fanya homework yako mapema ya mahitaji muhimu yanayotakiwa kwa shughuli husika (kama vile barua ya uchumba, ama anakabidhiwa binti mapema ili apeleke kwa wazazi wake) siku kadhaa kabla haujaenda.
N.K.
Ng'ongoampoku Amenifungua hapa kwa jinsi ya kuiandika barua ya posa, pia ningependa kujua zaidi ya hapa.
Nimepata Sampuli ya barua ya posa inavyo takiwa kuwa toka kwa ndugu Lighondiwapendwa wazazi watarajiwa!
Mimi naitwa fulani bin fulani, ni mzaliwa wa pili katika familia ya Obama yenye jumla ya watoto watano, naomba kuzaliwa katika familia yenu kupitia kwa binti yenu mpendwa Pretta niliyefahamiana naye hapa Jamii forum na facebook. Naomba Kumposa Preta kufuatana na mila desturi na dini na msichana.
katika familia yetu hakuna wala sijawahi kusikia kama kuna magonjwa ya kurithi.
Naambatanisha barua hii na kishika uchumba cha laptop moja aina ya Dell optilex yenye thamani ya dolari elfu mbili.
Wenu mwanenu mtarajiwa
Fulani bin Fulani wa Kigambonino Dar
:A S-heart-2::A S-heart-2::A S-heart-2:
Na imani hii thread itakuwa msaada kwangu na kwa wengine wengi tu, Tafadhalini na wakaribisha kwa michago yenu.