Aaron Arsenal
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 24,504
- 28,692
Wiki iliyopita nilileta uzi wa kumuelezea rafiki yangu Hosea Chamungu aliyetumia ujinga wa Watanzania wengi kujikwamua kimaisha, baada ya kutoka masomoni Kenya na kurudi Tanzania na kukumbana na Sakata la uhaba wa ajira.
Leo, nawaletea mtu wangu wa karibu tuliyesoma nae chuo kikuu Mlimani (UDSM), japo Mimi mwaka wa pili sikuendelea na chuo kutokana na matatizo yaliyo nje ya uwezo wangu , japo kwasasa nimeshahitimu Degree .
Huyu bwana anaitwa Mwasha , tumepishana mwaka mmoja, mimi nimezaliwa 1993 yeye 1992, alinitangulia kuhitimu Elimu ya juu hapo UDSM kama nilivyosema awali,
Alipohitimu Na yeye alikutana na Sakata lile lile linalotukumbuka vijana linaloitwa UHABA WA AJIRA ,
Hakumlalamikia mtu wala serikali, nilipotezana nae kwa muda kidogo maana mimi masomo niliishia njiani .
Mwaka jana nimekutana nae akiwa ndani ya Range Rover nyekundu na mkewe.Tukasalimiana akanialika kwake, nilipanga siku nikaenda kuonana nae.
Nilimuuliza siri ya utajiri wake wa haraka hivo, majibu yake yalikuwa ya shortcut sana ila main point ilikuwa ni kuwatumia wajinga kama fursa na kunisihi niache kulialia na kuilalamikia serikali.
Anauza mafuta, maji, vitambaa kwa mgongo kuwa vina upako na anavitoa Israeli, maji anasema anayachukua mto Yordan.
Na sasa tayari ameshafungua kanisa ana waumini wengi sana hapa Dar. Maombi yake kuna kulipia kiasi cha pesa.
Kwasasa tayari ameshajenga nyumba ya kisasa, na ana magari ya kubadilisha ana miaka 27 tu.
Kitu ambacho najiuliza hadi leo kuanzia kwa Hosea Chamungu na huyu Mwasha hii sayansi ya kunena, hizi wanazoita kunena kwa lugha na kuwaangusha chini watu kwa kigezo wana mapepo wanajifunzia wapi, hili swali wote waligoma kufunguka.
Kwasasa yupo Dar -Bunju, Kilimani. Ana kanisa na anafanya hapo mazingaombwe (miujiza fake) na kuuza mafuta, maji na vitambaa.
Jina alishabadilisha anajiita NABII NA MTUME Mwasha
SWALI: Ni halali kuwageuza wajinga fursa?
Yeremia 14:14,16
“Ndipo BWANA akaniambia, Hao manabii wanatabiri uongo kwa jina langu mimi; mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo, na uaguzi, na neno la ubatili, na hadaa ya mioyo yao. Na watu hao, waliopewa unabii na wao, watatupwa nje katika njia kuu za Yerusalemu kwa sababu ya upanga na njaa; wala hawatakuwa na mtu wa kuwazika, wao na wake zao, na wana wao, na binti zao; maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.”
Yeremia 23:31-32
“Tazama, mimi ni juu ya manabii, asema BWANA, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema, Tazama, mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA.”
KUNA MWINGINE NILISOMA NAE SECONDARY, CHUO KIKUU AMEMALIZA SUA, TAYARI SASA NI NABII.
Nitamtembelea kuendelea na utafiti wa WAJINGA KUGEUZWA FURSA
Leo nimemkumbuka rafiki yangu aliyetumia ujinga wa watu kama mtaji na fursa
Dunia hii ina mambo ya kufurahisha na kuhuzunisha. Leo nikiwa nimetulia home, ghafla nimemkumbuka rafiki yangu wa Iringa ni mkubwa kwangu kwa miaka kama sita hivi kwa sasa yupo mikoani anapiga hela tu. Huyu jamaa alienda kusoma Kenya Degree ya Agriculture Engineering kwenye chuo cha Egerton...
www.jamiiforums.com
Leo, nawaletea mtu wangu wa karibu tuliyesoma nae chuo kikuu Mlimani (UDSM), japo Mimi mwaka wa pili sikuendelea na chuo kutokana na matatizo yaliyo nje ya uwezo wangu , japo kwasasa nimeshahitimu Degree .
Huyu bwana anaitwa Mwasha , tumepishana mwaka mmoja, mimi nimezaliwa 1993 yeye 1992, alinitangulia kuhitimu Elimu ya juu hapo UDSM kama nilivyosema awali,
Alipohitimu Na yeye alikutana na Sakata lile lile linalotukumbuka vijana linaloitwa UHABA WA AJIRA ,
Hakumlalamikia mtu wala serikali, nilipotezana nae kwa muda kidogo maana mimi masomo niliishia njiani .
Mwaka jana nimekutana nae akiwa ndani ya Range Rover nyekundu na mkewe.Tukasalimiana akanialika kwake, nilipanga siku nikaenda kuonana nae.
Nilimuuliza siri ya utajiri wake wa haraka hivo, majibu yake yalikuwa ya shortcut sana ila main point ilikuwa ni kuwatumia wajinga kama fursa na kunisihi niache kulialia na kuilalamikia serikali.
Anauza mafuta, maji, vitambaa kwa mgongo kuwa vina upako na anavitoa Israeli, maji anasema anayachukua mto Yordan.
Na sasa tayari ameshafungua kanisa ana waumini wengi sana hapa Dar. Maombi yake kuna kulipia kiasi cha pesa.
Kwasasa tayari ameshajenga nyumba ya kisasa, na ana magari ya kubadilisha ana miaka 27 tu.
Kitu ambacho najiuliza hadi leo kuanzia kwa Hosea Chamungu na huyu Mwasha hii sayansi ya kunena, hizi wanazoita kunena kwa lugha na kuwaangusha chini watu kwa kigezo wana mapepo wanajifunzia wapi, hili swali wote waligoma kufunguka.
Kwasasa yupo Dar -Bunju, Kilimani. Ana kanisa na anafanya hapo mazingaombwe (miujiza fake) na kuuza mafuta, maji na vitambaa.
Jina alishabadilisha anajiita NABII NA MTUME Mwasha
SWALI: Ni halali kuwageuza wajinga fursa?
Yeremia 14:14,16
“Ndipo BWANA akaniambia, Hao manabii wanatabiri uongo kwa jina langu mimi; mimi sikuwatuma, wala sikuwaamuru, wala sikusema nao; wanawapeni unabii wa maono ya uongo, na uaguzi, na neno la ubatili, na hadaa ya mioyo yao. Na watu hao, waliopewa unabii na wao, watatupwa nje katika njia kuu za Yerusalemu kwa sababu ya upanga na njaa; wala hawatakuwa na mtu wa kuwazika, wao na wake zao, na wana wao, na binti zao; maana nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao.”
Yeremia 23:31-32
“Tazama, mimi ni juu ya manabii, asema BWANA, wanaotumia ndimi zao na kusema, Yeye asema, Tazama, mimi ni juu ya hao wanaotabiri ndoto za uongo, asema BWANA, na kuzisema, na kuwakosesha watu wangu kwa uongo wao, na kwa majivuno yao ya upuzi, lakini mimi sikuwatuma, wala sikuwapa amri; wala hawatawafaidia watu hawa hata kidogo, asema BWANA.”
KUNA MWINGINE NILISOMA NAE SECONDARY, CHUO KIKUU AMEMALIZA SUA, TAYARI SASA NI NABII.
Nitamtembelea kuendelea na utafiti wa WAJINGA KUGEUZWA FURSA