Jinsi simu za touch screen zinavyotupa tabu kuandika texts

Jinsi simu za touch screen zinavyotupa tabu kuandika texts

maroon7

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
11,341
Reaction score
15,831
1620549_475771395867810_870678101_n.jpg



Hapa ndio namimi nazichukiaga hizi simu maana ukiandika 2 inakuja 5...lol,kazi kwelikweli
 
mwingine alipata sugu kwenye kifua kwani wakati wa kuandika kitu au kupiga lazima aweke ile password yake ambayo ipo kama Z hv, kila mara anapofanya hivyo mkono huishia kifuani mpaka kifua sasa kimeota sugu...kama wale wanaofanya mazoezi ya kupiga ngumi kwenye mchanga jinsi ngumi zao zilivyokuwa na sugu
 
yani mm sipendi kuchat na hizo simu, nina ki obama changu hapa, yani hata ki drive naweza reply meseji, ila ayo matouch kama hujaingia mtaloni.
 
Hahahahaaaa........ Jamani jamani..!!!
 
mie kwa kweli natumia bluestacks kwa laptop kwa hivyo viber, whatsapp sijui insta vyote nachati kwa laptop manake nimeona hizi touch zitakuja kufanya nipokonywe mke
 
mwingine alipata sugu kwenye kifua kwani wakati wa kuandika kitu au kupiga lazima aweke ile password yake ambayo ipo kama Z hv, kila mara anapofanya hivyo mkono huishia kifuani mpaka kifua sasa kimeota sugu...kama wale wanaofanya mazoezi ya kupiga ngumi kwenye mchanga jinsi ngumi zao zilivyokuwa na sugu
Hah!!!!!
Ni shida!!!
 
Kuna mdau mmoja alisema masist du ndio wanazipatia, tena wanaandika meseji fastaaa.
 
Ni Mtazamo tu.
Jaribuni kuchunguza sana,hizi sim zinapunguza uwezo wa kufikiri,zinachosha akili,zinauwa macho na kupunguza uwezo wa kuona vizuri,chanzo cha Taifa la wavivu.

Nenda Airport uangalie wenzetu wa magharibi uone kama wanashuka na midubwana hiyo,wanashuka na Sim Za kawaida sana.Maana hawataki usumbufu na wanajua hilo.

Maaan hizi zinaitwa sim za Kuuzia Sura,ukipanda boti basi watu wanashindana,maharusini ndio kabisaaa,full ushamba.

Halafu Kila nikiangalia Tamthilia na Maadhi ya Movies za majuu naona wanatumia sim za kawaida,sasa sijui hali ipoje.

Mie nilitumia siku moja ya jamaa,nikamuuliza hivi muda wote unafatua kitu kwenye sim na wakati mie yangu ni sekunde tu kila kitu mpango mzima.
Sasa umkute mtu kwenye Tigo pesa anatoa pesa ndio utaona kazi sasa.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Ni Mtazamo tu.
Jaribuni kuchunguza sana,hizi sim zinapunguza uwezo wa kufikiri,zinachosha akili,zinauwa macho na kupunguza uwezo wa kuona vizuri,chanzo cha Taifa la wavivu.

Nenda Airport uangalie wenzetu wa magharibi uone kama wanashuka na midubwana hiyo,wanashuka na Sim Za kawaida sana.Maana hawataki usumbufu na wanajua hilo.

Maaan hizi zinaitwa sim za Kuuzia Sura,ukipanda boti basi watu wanashindana,maharusini ndio kabisaaa,full ushamba.

Halafu Kila nikiangalia Tamthilia na Maadhi ya Movies za majuu naona wanatumia sim za kawaida,sasa sijui hali ipoje.

Mie nilitumia siku moja ya jamaa,nikamuuliza hivi muda wote unafatua kitu kwenye sim na wakati mie yangu ni sekunde tu kila kitu mpango mzima.
Sasa umkute mtu kwenye Tigo pesa anatoa pesa ndio utaona kazi sasa.

Ni ushamba sababu watu wa magharibi hawatumii au nini kigezo chako????!!!!
 
Ni rahisi mno ukizoea. Ila kama vidole vyako vya mkono ni vikubwa lazima upate shida.
 
Alaf zina tatizo moja tu, charge zinaisha haraka sana, mimi hizo nikirudi toka mzigoni hm naiwasha na kuchezea wasap na fb kwishney, asbh narudi kwenye za kawaida natumia kama sina shida!
 
Back
Top Bottom