Jinsi madereva wa Uber wanavyoibia wateja kupitia kuchakachua navigation map.

Jinsi madereva wa Uber wanavyoibia wateja kupitia kuchakachua navigation map.

Swali la kizushi kwani hii itasoma kote kote? Namanisha kwa dereva na abilia?ikichakachuliwa
Ndugu, sijui unaiahi wapi ila ukiita Uber unaielekeza unaelekea wapi, inakuonyesha ramani au barabara mtakayopita, ingawa sio lazima mpite hiyo ramani mnaweza kupitia njia nyingine ila mkafika mnapoenda.

Sasa chukulia mmepita njia yoyote, njia inajulikana mfano hapa Dar kutoka gongolamboto hadi posta njia inajulikana na imenyooka, unaita uber mnafika posta kutokea gongolamboto ila ramani inaonyesha mmepitia Temeke, mkarudi Buguruni, mkatembea hadi Magomeni, mkarudi Kariakoo mkatokea Kamata mkapitia kilwa road kisha mkaingia Posta lakini wewe unajua kabisa mlipitia Nyerere road moja kwa moja hadi mkafika hamjapinda mahala popote, je hiyo ramani itakua sahihi au sio sahihi?

Utalipa hela utakayoambiwa au utakataa?
 
Kama mtu unajua unapoishi kwanini hizo zigzag zitokee?
Uongo mtupu kuharibu biashara
Sio uongo mkuu, jamaa wamewahi kuniibia unaweza kutokea Karume unaenda Morocco, route inaanza ubungo tazara na mizunguko mingine, mjirekebishe.
 
Ndugu, sijui unaiahi wapi ila ukiita Uber unaielekeza unaelekea wapi, inakuonyesha ramani au barabara mtakayopita, ingawa sio lazima mpite hiyo ramani mnaweza kupitia njia nyingine ila mkafika mnapoenda.

Sasa chukulia mmepita njia yoyote, njia inajulikana mfano hapa Dar kutoka gongolamboto hadi posta njia inajulikana na imenyooka, unaita uber mnafika posta kutokea gongolamboto ila ramani inaonyesha mmepitia Temeke, mkarudi Buguruni, mkatembea hadi Magomeni, mkarudi Kariakoo mkatokea Kamata mkapitia kilwa road kisha mkaingia Posta lakini wewe unajua kabisa mlipitia Nyerere road moja kwa moja hadi mkafika hamjapinda mahala popote, je hiyo ramani itakua sahihi au sio sahihi?

Utalipa hela utakayoambiwa au utakataa?
Kweli mkuu, imewahi nitokea, wasibishe.
 
Asante sana mleata uzi huu,niliusoma jumamosi jana jumapili kwa mara ya kwanza driver akanipiga kwa ku turn off gps yake na hiyo route kila siku nalipia 2000-3000/= ila jana jamaa kanipiga 9,000/= nikamwambia mzee umenipiga na nikampa hela yake sikutaka kelele,baadae nikareport tu uber leo wakanirudishia 4,500/= yangu
 
yap, mimi JUmamos juzi, nilitokea airport hadi Kifuru shule ya msingi, safari ambayo haina foleni lakini nililipishwa shs 20,000/= kiasi cha pesa ambacho sijawahi kulipa tangu nimeanza kutumia usafiri wa uber. nafikiri niliibiwa hapo.
 
Aisee wabongo tunajua kujiongeza,sijui kama wenye kampuni wanajua hilo
 
Sijui kama mtoa mada ni dereva wa Taxify ama katumwa na hao Taxify.
Mimi ni shuhuda wa kupewa bili kubwa kuliko maelezo na Uber....sina hakika kama ni wizi wa makusudi au ni kosa la kiufundi. Ni jambo ambalo Uber wanapaswa kuliangalia.


Taxi FYI promo kazini.
 
Back
Top Bottom