Jinsi Kampuni za Simu zinavyowaibia wateja wao!

Mimi waliniunganisha na huduma ambayo hata sijaiomba (tigo hao) , dah walikuwa wananikata, nilikaa we nikajaribu kuwauliza wenzangu, nao wakawa wanalalamika kama mimi, nikaona isiwe tabu, nikawapigia simu wakaniambia eti Kuna huduma nilijiunga ya kusikiliza hadithi, nikawaambia mm sijawahi kujiunga na huduma yyt Ile, nilibishana nao, baadaye wakaniambia jinsi ya kujitoa, hii ilikuwa kama miezi miwili iliyopita. Sasa wiki iliyopita nilinunua vocha ya elfu mbili, nikajiunga na kifurushi cha buku jero, mia tano ikabaki,naamka asubuhi nijiunge na kifurushi cha jero, inashindikana kumbe wamekata mia tatu, nikaona haina haja nikachomoa line yao nikaweka kabatini, nikaweka line ya mtandao mwengine. Tigo badilikeni ndio wenye tabia za kihuni, ningeitumia TTCL ila tatizo vocha zao tabu ila karibia mitandao yote ni wahuni wamekaa kiwiziwizi, wanaziendekeza njaa za kipumbav. u.
 
Kampuni zote za simu wana michezo hii ila Vodacom ndio kinara wao, tatizo kubwa ni kwamba wakuu wetu na ofisi zao wanategemea sana kampuni hizi pindi chaguzi zinapofika hivyo sidhani kama wana uwezo wa kukomesha uhuni huo kama Kagame alivyofanya
 
Duuuh...kumbe bado wapo watu hupenda vya bure...! Dezo gharama...!
Hapa haviongelewi vya bure tu ndg yangu,kinaongelewa kitu kinacho gusa nyanja zote ktk sekta ya mawasiliano. Mfano ninao hata mimi. Wiki jana nilikuwa na bando kwenye akaunti yangu na pia nikawa na kiasi cha 7,000/= kama salio kwenye akaunti kuu. Niliperuzi kama dk.3-4 hivi kisha nikatumiwa sms kuwa nimetumia sh.100 kutoka ktk kiwango cha 50,000/= cha matumizi ya internet. Kuona ujumbe huo nikajua kuna uwezekano bando limefyekwa hivyo nikakimbilia kuangalia salio kama hiyo 100 imekatwa kwenye 7,000/= ili ninunue bandle lingine. Nilicho kikuta ni salio kusomeka 0. Nikalazimika kutafuta salio jingine. Kama una salio taarifa ya bando haitolewi pindi bando liishapo mpaka na salio la akaunti kuu likiisha ndiyo unataarifiwa kuisha kwa bando. Jana mida ya mchana wakati nasafu bandle likaisha hapo sijaacha salio lolote ndiyo wananitumia ujumbe tena eti umetumia kiasi cha 7,000/= kutoka ktk kiwango chako cha 50,000/= cha matumizi yako ya internet kana kwamba ndiyo niliyo kuwa naitumia kumbe kiasi hiki nilisha kwapuliwa siku nyingi zilizo pita. Ushahidi huu hapa kwenye kiambata. Sasa kwa mfano hapo kuna cha bure kipi kilicho niponza mimi?
 
Hapo kwenye Facebook bure, maelezo yako yanapishana na uzoefu wa miaka 10 kwasababu Facebook wenyewe wanaoption ya huduma Bure lakini huku tunaambiwa ni hisani ya makampuni ya Simu
 
Pamoja na yote mazuri uliyoyaandika na kufafanua vizuri na kuyafahamu kwa miaka kumi halafu eti unayatoa Leo basi na wewe kama ilikuwa inakuuma ungeacha kazi Mara moja 10 yrs back na kutoa taarifa hii kwa Mamlaka husika.

Lakini kwa kutuambia Leo baada ya kufanya kazi miaka 10 basi ulikuwa miongoni mwao ktk huo wizi.

Na hapo ndiyo napesema kujua uzalendo wa watz ni ngumu sana,Leo tunamuona huyu mtoa mada wa maana sana wakati ametuibia kwa miaka 10.

Wewe bwana ni miongoni mwa mliowaibia watz ktk mitandao ya simu unatakiwa ukiri hayo kwani ulikuwa unapokea mshahara wa kampuni inayowaibia ndugu zako na wewe ukaendelea tu sasa aidha umeshiba pesa au umepunguzwa kazi ndiyo unatoa taarifa kwa umma kuhusu wizi sijakupenda.
 
makampuni ya simu ni sumu kwa wanyonge....hushirikiana na TCRA kuwaibia wanyonge mshabara bila chenga.
 
Swala LA kifurushi cha bure lilioanzoshwa na kampuni moja jana tu limenikamua vi mb vyangu nikajua si mzigo wa bure fb basi nikafungua mipicha ya wadau kuja kucheck kile kimnara cha bure kimetokea nikajua nimeshaumia,so ukweli ni kuwa wanakula data zako zote zikiisha ndio wanakuunga bure fb pekee,ila jambo lililonikera zaidi ni pale nilipotumia reminder msg ya kuwa mb zako za bure zimebaki 8 ilihali nimezima data Muda huo nikaona haya mbona maluweluwe baada ya masaa manne ikaja msg salio lako LA kifurushi cha bure limekwisha

Ajabu wanakulaje data wakati data bundle iko off?
 
Dakika ina sekunde 60, lakini unaweza ukakuta dakika zao zina sekunde 40 hadi 45.
Vodacom ndiyo wanaongoza kwa wizi.
 
Unayosema ni kweli kabisa na mimi yamenikuta Vodacom ila niliwakoromea haswa eti unanunua kifurushi leo kesho au muda huohuo unatumiwa ujumbe kifurushi kimeisha
 
Inakuaje kampuni ya simu inakwambia, inaomba imei ya simu yako pamoja na number yako?
ilikuwaje hadi ukaombwa hivyo vitu mkuu? ulipotelewa simu? fafanua.
 
Kaz nikwakooooo......hawawez kukutumia sms yakumalizika mbs kweny bundle lako wakat unasalio lakawaida wanachofanya nikukuacha utiririke uwape faida
 
Huu wiz had kwa ndugu zetu HALOTEL, ukiacha salio kila siku lapungua. Sometimes ukituma sms unarudishiwa sms kuwa umetumia dakika kadhaa, mtandao wa internet kwa baadh ya sehem unakata Hadi week na wala hawaoneshi kujali
 
Kuna wizi mwingine huu,unanunua vocha ya mia tano lakini ukijiunga kifurushi unaambiwa umejiunga kifurushi cha sh 499.Hii shilingi moja inaenda wapi?Piga hesabu sh 1×wateja milioni 4 mwezi ×mwaka.
 
Tigo hayo mambo wanaweza sana. Sasa hivi tunakaribia mwezi eti mitambo yao inasumbua.

Unafungua youtube,inaload tu bila kuona chochote. Ila mwisho wa siku Mb zinaenda.

Msg unatuma sasa hivi,inafika baada ya nusu saa.

Jamaa ananipigia simu anaambiwa simu yangu inatumika,wakati mimi simu ipo charge.

Shame on you tigo Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…