Baba Mtakatifu Fransic amemteua Askofu Damian Dennis Dallu wa Jimbo la Geita kuwa Askofu mkuu wa jimbo kuu la Songea,hivyo kwa sasa Jimbo kuu la Songea litaongozwa na Askofu Mkuu Damian Dennis Dallu.
Nafasi hiyo imezibwa baada ya Askofu Nobert Wendelin Mtega kuachia nafasi kutokana na matatizo ya kiafya.
Askofu Damian Dennis Dallu alizaliwa mwaka1956 Kijiji cha Kiponzero,Parokia ya Ifunda,Jimbo katoliki la Iringa,baada ya masomo,malezi na majiundo yake ya kitume alipadirishwa 15/11/1984,Baba Mtakatifu Yohane Paul II alimteua Askofu wa pili wa Jimbo la Geita 06/05/2000 na 30/07/2000 aliwekwa wakfu kuwa askofu wa Geita.
Akizungumza leo na Radio Vatican,Askofu Mkuu D.D.Dallu amesema kwa miongozo ya katekisimu ya Kanisa katoliki na Mtaguso wa pili wa Vatican vinatoa muongozo wa uinjilishaji katika ulimwengu wa sasa wenye changamoto ya utandawazi,nafasi ya kuimarisha haki za binadamu na utu wa mwanadamu,Ametoa mwaliko wa kanisa katoliki kukuza mashauriano na ushirikiano wa kidini katika ulimwengu wa leo.
Kila la kheri waumini wa jimbo Kuu la Songea,ambapo metopolitan yake ni majimbo ya Mbeya,Njombe,Mbinga,Iringa,Mtwara,Lindi na Tunduru-Masasi,hivyo Askofu mkuu Dallu atasimamia majimbo hayo.
BRAVO S.E MONS DAMIAN DENIS DALU