Mkaa Mweupe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 654
- 183
Baada ya kusikika habari kuwa kuna mwanamke aliuwawa kule mwanza kwa kosa la kuiba simu, kweli nilisikitika kuwa pengine alikuwa ameonewa sana. Lakini sasa nimepata kujua kuwa kuuwawa kwake ni sawa tu na vibaka wengine.
Imenigusa kufikia uamuzi huu baada ya kugundua kuwa kwa sasa wanawake wadogo wadogo ndio wamekuwa vibaka maarufu wa simu za mikononi.
Katika tukio moja lililotokea hivi karibuni, binti mmoja mtanashati alikwenda kumuazima simu kijana mmoja mjasiria mali katika biashara zake kwa madai kuwa simu yake imekwisha chaji na kuna simu muhimu anataka kupiga ili aweze kukutana na mwenyeji wake katika mitaa hiyo. Yule kijana kwa uelewa wake alimjibu kuwa pale mbele kuna kibanda unaweza kwenda kupiga. Binti akasema kuwa hakuwa na hela ila line yake ina hela na kusisitiza kuazimwa simu. Kijana akamuelewa na kumpatia TZS 500 ili akapige hiyo simu pale kibandani.
Binti alipoke ile pesa na kwenda kuvunga pale kibandani pasi na kupiga simu kama alivyodai. Baada ya muda yule binti alirejea tena maeneo yale ya mjasiriamali (Shoe shine) pasi na kujua kuwa yule aliyempatia ile TZS 500 ndio mmiliki wa ile sehemu. Kijana alikuwepo pale ila alikuwa amegeukia nyuma. Binti alipofika alirudia maneno yale yale kwa mteja mwingine akimwomba amuazime simu yake. Mjasiriamali aliposikia yale maneno aligeuka na kumweleza yule binti, "Si nilikupatia hela uwasiliane? Imekuwaje tena?". Binti aliposikia alishtuka na kuingia mitini.
Katika tukio jingine kuna binti mdogo (miaka kati ya 10 na 12) alitumiwa na vibaka kwenda kuazima simu kwa mzee mmoja ili aweze kuwasiliana na ndugu yake. Mzee bila hiyana alimpatia ile simu. Hamadi yule binti aliposema tu "Hallo!", alitokea kibaka ambaye alimpora simu yule binti na kutokomea nayo.
Tahadhari: Tuendelee kuishi kwa amani ila tusiwe na imani na kila tumwonae, dunia imeharibika!
Imenigusa kufikia uamuzi huu baada ya kugundua kuwa kwa sasa wanawake wadogo wadogo ndio wamekuwa vibaka maarufu wa simu za mikononi.
Katika tukio moja lililotokea hivi karibuni, binti mmoja mtanashati alikwenda kumuazima simu kijana mmoja mjasiria mali katika biashara zake kwa madai kuwa simu yake imekwisha chaji na kuna simu muhimu anataka kupiga ili aweze kukutana na mwenyeji wake katika mitaa hiyo. Yule kijana kwa uelewa wake alimjibu kuwa pale mbele kuna kibanda unaweza kwenda kupiga. Binti akasema kuwa hakuwa na hela ila line yake ina hela na kusisitiza kuazimwa simu. Kijana akamuelewa na kumpatia TZS 500 ili akapige hiyo simu pale kibandani.
Binti alipoke ile pesa na kwenda kuvunga pale kibandani pasi na kupiga simu kama alivyodai. Baada ya muda yule binti alirejea tena maeneo yale ya mjasiriamali (Shoe shine) pasi na kujua kuwa yule aliyempatia ile TZS 500 ndio mmiliki wa ile sehemu. Kijana alikuwepo pale ila alikuwa amegeukia nyuma. Binti alipofika alirudia maneno yale yale kwa mteja mwingine akimwomba amuazime simu yake. Mjasiriamali aliposikia yale maneno aligeuka na kumweleza yule binti, "Si nilikupatia hela uwasiliane? Imekuwaje tena?". Binti aliposikia alishtuka na kuingia mitini.
Katika tukio jingine kuna binti mdogo (miaka kati ya 10 na 12) alitumiwa na vibaka kwenda kuazima simu kwa mzee mmoja ili aweze kuwasiliana na ndugu yake. Mzee bila hiyana alimpatia ile simu. Hamadi yule binti aliposema tu "Hallo!", alitokea kibaka ambaye alimpora simu yule binti na kutokomea nayo.
Tahadhari: Tuendelee kuishi kwa amani ila tusiwe na imani na kila tumwonae, dunia imeharibika!