Kelvin35
JF-Expert Member
- Feb 26, 2023
- 567
- 865
Saint Anne kama utapata kibali, basi Nakukaribisha hapa ili tuendelee kujifunza
Amen, tumebarikiwa Mtumishi, Atukuzwe Mungu baba kwa njia ya Yesu Kristo kwa kutukomboa kwa Damu yake takatifu, ninashukuru sana kwa zawadi na Neema ya Wokovu, Rehema ya Yesu Kristo ni kubwa sana kwa sisi tunaoamini na Mimi Leo muda huu ninshuhudiwa na roho ndani yangu nimepokea Neema na Rehema kwa sababu nimekisogelea kiti cha Neema na Rehema kwa ujasiri na nimeongozwa kwenye madhabau hii na kujaliwa mahitaji yote ya Wokovu, atukuzwe Mungu Mkuu litukuzwe Jina lake Takatifu kwa njia ya Yesu Kristo na Damu yake Takatifu, nashukuru Mimi nina uhai na uzima tele kwa kujiunga na madhabau hii, Mwana ameniweka huru na nipo huru kweli kweli. Yesu ni Bwana na Mwokozi wa maisha yangu, naombea wote tunaoamini tupokee Neema hii Amen.
Mungu yu pamoja nasi.
AGANO LA KISHETANI LA UTAJIRI,MALI,CHEO,MVUTO(MAFANIKIO) KATIKA MAUTI ZA NAFSI NA ROHO ZA HAO WAUTAFUTAO UTAJIRI:
17.12.2023.
Bwana Yesu apewe sifa sana.Nimerudi tena kwenu kuwapasha habari za ufalme wa Mungu na siri za kuzimu ili mpate kuzijua na kuzishinda hila za shetani.
Ujumbe huu unakuja kwenu hasa watumishi wa Mungu aliye hai ili mpate mbinu au kama mnazo hizi basi mziboreshe kupitia hiki nitakachokisema hapa.
Siyo kwamba mimi ni msemaji wenu,siyo kwamba mimi ninajua kuliko nyinyi,au siyo kwamba mimi ninafundishwa peke yangu,la hasha! Msinifikirie vibaya,mimi ninasema kitu nilichoambiwa nikiseme.
Kwako kinaweza kisiwe na manufaa, ila kwa wengine ni msaada mkubwa sana,hivi kwanini mtumishi wa Mungu huduma yako haikui, kwanini watu wakucheke kwamba huduma yako ni ya kimasikini?
Yaani wachawi wachezee kwenye madhabahu yako na kuinajisi halafu wewe uhubiri watu wasipone ,bado uyakatae haya maarifa.?
Baada ya masomo haya ninakuomba mtumishi wa Mungu tusaidiane kuzivunja hizi madhabahu za miungu,wachawi,waganga wa kienyeji na washirikina wote wapate kubarikiwa na moto wa Mungu.
Yaani tuwabariki kwa moto,tuwabariki kwa upanga wa Mungu, tuwabarikie kwa damu ya Yesu viwachome hadi wateketee mpaka wafuasi wao waseme huu ni ubarikio wa namna gani.
Naam! Nasi tutawaambia huu ni ubarikio wa moto wa Mungu, damu ya Yesu,Jina la Yesu na upanga wa Mungu kuanzia 2024 mpaka Yesu anarudi kutunyakua.
Mizaha sasa imetosha juu ya kanisa la BWANA na kwa watu wa Mungu. Mtumishi wa Mungu bila kuwa na hasira ya kimungu huwezi kutoka kwenye hayo maagano yanayokukwamisha wala hautaweza kutoboza.
Omba kama kichaa, omba kama mwendawazimu, usiweke silaha chini mpaka uone maadui zako wamesalimu amri,huwezi kuvikwa taji kama hujapata ushindi. Ushindi wa kwanza ni hapa hapa duniani. Usimchekee shetani,usimuonee aibu shetani atakuiabisha ukweni kwako.
Ukali wenu nitauona kwenye matokeo ya shuhuda zenu.Mimi nimevipiga vita sana nikiwa nyikani, ninajua hiki ninachokiongea, hakuna miungu wala shetani itakayoweza kusimama mbele yangu na ikashinda, Kwasababu Yesu aliye ndani yangu ni mkuu kuliko wote,lazima nimtukuze mahali popote pale atakaponituma, ila ninaanzia hapa nyumbani kwanza.
MUNGU AWABARIKI SANA:
Mwili wa mwanadamu usiokuwa na uhai huitwa maiti. Ni maiti kwasababu umekutwa na umauti.
Umauti ni roho ya kifo ambayo humvaa mtu na kuondoka na uhai wake.Uhai huu ukiondolewa ndani ya nafsi ya mtu ndipo mtu huwa mfu, nafsi isiyokuwa na uhai wala utambuzi wa aina yotote ile.
Mwili hupelekwa na kuhifadhiwa katika nyumba yake ya milele iitwayo Kaburi.Na hapa ndipo neno la BWANA linapotimizwa kwamba umeumbwa kwa udongo, utarudi tena udongoni.
Hakuna mwanadamu awezaye kukishinda kifo isipokuwa Yesu peke yake na wale waliopata neema mbele za macho ya BWANA.
Hawa ni wale walioandikiwa haki mbele za kiti cha enzi cha Mungu Baba.
Hata shetani na mbinu zake zote hawezi kukishinda wala kukiepuka;kwasababu tangu kipindi kile alivyoasi, alishahukumiwa adhabu ya kifo katika lile ziwa likawalo moto.
Watenda dhambi wote hukumu yao ilishatoka, ambayo ni kifo cha umauti wa milele pamoja na shetani.Labda wale watakaopata neema ya kuisikia Injili ya Yesu,hao ndio watakaourithi Uzima wa Milele.
Waliokufa katika dhambi,wote ni mauti ya milele maana watatupwa katika lile ziwa liwakalo moto usiku na mchana pasipo kuzimika.
Pamoja na kwamba mtu anakufa mwili wake na roho yake kwenda sehemu nyingine.Lakini kuna watu wengine wanaandikiwa VIFO WAKINGALI HAI,WANATEMBEA HUKU ROHO WA UMAUTI AKIWA JUU YAO.
Hapa kinachosubiriwa ni muda ,saa na sababu itakayomsababishia umauti. Vifo vya namna hii haviji pasipo sababu maalumu.
Inaweza kuwa ni sababu ya uchawi, visasi, chuki,wivu,maagano ya kichawi yaliyofanywa huko nyuma na wazazi au mababu za hao watu.n.k.
Wengine ni laana inayotoka ndani ya ukoo wa huyo mtu.Huyu roho akishamvaa mtu hujikuta anaanza kujichukia, kukata tamaa na kukosa matumaini, hukosa raha na uchangamfu, hupenda kujitenga na watu,pia ni mtu wa kuwa na wasiwasi wakati wote.
Akimtazama mtu usoni huwa na aibu aibu huku akiangalia chini,huyu ni roho anakuwa anajua unamuona ila ni ngumu kung'amua katika mwilini, uso wa huyu mtu hukosa nuru na kuwa na mpauko usoni kama rangi ya maiti.
Huwezi kumshinda roho wa mauti isipokuwa kwa njia ya nguvu ya MSALABA WA BWANA YESU.
Yesu alivyosema pale msalabani "IMEKWISHA",Alikuwa anaitoa roho yake ili kwenda kuzimu alipo shetani kumnyang'anya funguo za uzima na mauti na kuisimamisha juu ya watu wake wote dunia nzima.
Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya watu wote, watu wasidanganye eti alikufa kwa ajili ya Wakristo tu,siyo kweli yeyote anayeliamini Jina lake ni wake Yeye Kristo.
Pale ilikwisha nguvu,ilikosa uhalali wa kutuua kwasababu hati zote za mashtaka zilipigiliwa pale msalabani. Tulipewa uzima wa Milele mara tu baada ya kufufuka na kwenda(kupaa) juu mbinguni kwa Baba yetu.
Wanadamu wanapotea na kufa vifo ambavyo siyo vyao wala vifo vya haki kwasababu hawana maarifa ya Mungu, na kwa kuwa wamemkataa Yesu na kuamua kumfuata shetani.
Shetani amewadanganya na kuwapotosha macho yao ili wasipate kuona na kuijua kweli,neema na thamani ya nguvu ya msalaba iletayo ukombozi ndani ya mtu,badala yake wameyakumbatia mafundisho manyonge na madhaifu kwa kujipa matumaini kwamba mtu akifa ataombewa na kupata msamaha wa ondoleo la dhambi.
Wanasahau kwamba imeandikwa "bora wafu wafao katika BWANA maana hao watafufuliwa siku ya mwisho".
Maana yake ni watu waliokufa katika Kristo Yesu.
Hakuna siku ya mwisho nyingine, bali ni sasa,hizi ndizo nyakati za mwisho ambazo Bwana Yesu yuaja upesi kuja kulinyakua kanisa lake,ambapo kabla ya ujio wake atawaandaa watakatifu wake ili wapate kumpokea mawinguni.
Hata wale wafu waliokufa katika BWANA ambao maandiko yanawataja, watafufuliwa kwanza ili waungane na walio hai,waliolikiri Jina Langu.Hawa ni wateule Wangu na watakatifu WANGU, niliopendezwa nao.(JESUS SPEAKS HIMSELF THROUGH ME).
Wale waliolikataa Jina langu ,na wale walio vuguvugu;wale waniitao BWANA,BWANA.Lakini hapo hapo wanajihudhurisha kwa miungu ,hao sina haja nao.(Yesu anaongea saa hii).
Nitawakataa, nitawatema, hawataingia RAHANI Mwangu,maana hawa ni wafu wanaoishi. Hawajafa katika BWANA wala hawaishi katika maisha matakatifu. (Roho yake imeongea ndani yangu,kuweni makini watu wa Mungu).
Kumbuka Andiko "waache wafu wazikane. ".Hawa ni wafu maana hawana walijualo, linaloendelea katika UFALME WA MUNGU.
Hawajui saa wala dalili za kuja kwa Mwana wa Adamu.Akili zao na fahamu zao haziwazi yaliyo ya Mungu, bali hujitaabisha na mambo ya dunia na kujihudhurisha kwa shetani.
WANAZIKANA KWA NAMNA GANI?
Roho wa umauti anawasubiria ili aweze kuwavaa na kuwachukua maana hawana kinga wala zuio au kizuizi chochote. Yeye asiye na Yesu ana roho wa umauti anatembea naye,anasubiri apate chanzo na sababu ili amvae na kuondoka naye.
Kuna wengine wameandikiwa umauti au kifo na wazazi wao,ndugu zao, Rafiki zao,na jamaa zao KAMA KAFARA LA UTAJIRI NA MALI.
Shetani hupenda kujifananisha na Mungu. Jinsi Yesu alivyotolewa kafara kama ondoleo la dhambi ya Ulimwengu, ndivyo hivyo hivyo shetani apendavyo kupewa kafara ya damu ya mtu.
Kafara ya damu ya mtu ina thamani kubwa kuliko damu ya mnyama,Kwasababu ina uhusiano na damu ya Yesu.Damu ya Yesu ina uungu mkuu sana,hivyo wote walio na Yesu wana damu kama Yake.
Mtu wa Mungu nisome kwa umakini sana hapa.
Maandiko yanasema,Yesu alisema yeyote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni,huyu ndiye ndugu yangu,na umbu langu,na mama yangu.Umbu kwa lugha nyingine ni dada.
Kwahiyo watu hawaitwi ndugu pasipo kuwa na vinasaba vya damu.
Unadhani kwanini sisi Watanzania huwa tunaitana kaka na dada? Maana tunachukuliana kama ndg wamoja. Kiroho sisi ni ndg sana,ndio maana utasikia ndg yetu,zetu Watanzania wamepatwa na shida fulani tuwasaidie.
Sasa twende kwa Yesu kwa mtiririko wa hapo juu.
Tumerithi ufalme wa Mungu kupitia imani ya baba yetu Ibrahimu,Yesu ni ukoo wa Yuda mtoto wa Yakobo,Yakobo ni mjukuu wa Ibrahimu.
Yesu anatokea katika shina la Daudi ,ambalo ni ukoo wa Yuda. Hivyo basi Yesu alikuwa na damu ya kibinadamu kamili kwasababu pia alizaliwa na mwanamke kama vile ambavyo watoto wote huzaliwa na mwanamke.
Kwahiyo kitendo cha Yesu kusema sisi tulio wake ni ndugu zake,maana yake katika imani tunakuwa katika ukoo mmoja na Baba yake ndiye Baba yetu pia. Glory to God, hallelujah!!!
Kwahiyo katika ulimwengu wa roho kinaumbika kitu kipya.Maana hata maandiko yanasema sisi tumefanyika viumbe vipya ndani ya Yesu.Tumebadilishwa kutoka ule utu wa kale na kuwa mpya ndani ya Kristo Yesu.
Tunafanyika kuwa watoto wa Mungu kwasababu tumebadilishwa na kuwa na sifa kama za Mungu wetu aliyetuumba. Kwahiyo kila kitu chetu ni kipya.
Damu yetu ni mpya kwasababu imetakaswa upya, imechujwa na kuwa safi na damu halisi.
Kwahiyo hii damu ndio ambayo shetani anaiwinda usiku na mchana ili aweze kuipata na kuichukua. Hii ina nguvu kuliko damu ya viumbe vyote.
Wanyama hawana damu safi,salama,na yenye thamani kama damu ya mtu;mtu aliyeokoka. Hii damu akiinywa shetani inampa nguvu na mafunuo kujua kitu gani kinaendelea katika ulimwengu wa roho wa NURUNI.
Yesu alisema Yeye ni nuru ya Ulimwengu.Kwahiyo katika vinasaba vya damu yake zipo chembe chembe ambazo zimebeba maono na mafunuo yenye taarifa sahihi za siri za mbingu.
Kwa kuwa Yesu anao ndugu zake ambao ni watoto wake,ambao ni watoto wa Mungu, basi hujikuta damu Yake iko sawa sawa na ndugu zake hawa,watu waliomkiri au waliokiri Jina Lake.
Lasivyo asingesema, sisi ni ndugu zake.Na ndugu zake wote ni wana wa Mungu walio ndani ya Yesu.Yesu ni ukoo wa watoto wote waliozaliwa mara ya pili kwa ajili ya Mungu.
Kwahiyo Yesu anawakilisha ukoo wa Mungu kwa watoto wa Mungu, akiwa Yeye ndiye mzaliwa wa kwanza. Ndio maana shetani anapenda kuwashikilia watoto wote waliozaliwa wakiwa wa kwanza,Kwasababu ni malango.
Ni malango kwasababu ni kielelezo cha Yesu Kristo. Kama alivyo Lango la baraka,uzima wa milele na mrithi wa viti vyote vya Enzi vya baba yetu.
Mtoto wa kwanza akiwa ni lango la laana,basi watoto wote watakaofuata watapata laana na mikosi.Labda tu kwa neema ya msalaba na damu iliyomwagika msalabani ipate kuwakomboa na kuwaweka huru.
Mtoto wa kwanza akiwa ni baraka ,halafu yuko upande wa Mungu ;Yaani yuko ndani ya Yesu.Shetani hupenda damu yake maana anajua atapata taarifa zote zilizomo kwake na kujua mpango wa Mungu ili aweze kumuibia na kisha kumakwamisha.
Kuna watoto wanaozaliwa na Nuru ya ulimwengu. Hawa tangu wakiwa tumboni mwa mama zao tayari Mungu alishawapaka mafuta.
Maandiko yanasema kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa;nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Angalia hapa Kumbe Mungu anawajua watoto wake. Shetani naye akishawajua anaanza utaratibu wa kuwashika. Hawezi kuwashika Wala kuwamiliki pasipokuwa na ridhaa ya wazazi,ndugu au jamaa zake.
Atakachokifanya ni kumshawishi mzazi kupitia kwa wachawi,waganga wa kienyeji, wazee wa mila na waaguzi waonao kwa kutumia mapepo ya utambuzi.
Kwamba wamtoe huyo mtoto madhabahuni kwao;kisha yeye watampatia nyota ya utajiri.
Hata kama ni cheo, au mafanikio mengine, lakini mafanikio yoyote huleta mali na vitu zikiwemo fedha. Hivi vitu vyote au wingi wa vitu mbalimbali, au wingi wa mali ni UTAJIRI.
Kwasababu ya tamaa ya mwanadamu ya kupenda pesa na utajiri hujikuta anamtoa au anawatoa watoto wake ili wawe kafara ya ngekewa yake.
Wapendwao kutolewa kafara huwa ni mabinti. Kwasababu hawa huwa ni rahisi kutoa damu zao kama sadaka kwa njia nyingi tofauti na watoto wa kiume ambao wao damu zao ni mpaka wapate ajali na vifo vyao.
Hawa watoto wa kike damu zao huanza kutoka pale wanapovunja ungo, damu ya ubikra, damu ya hedhi ya kila mwezi, damu ya wakati wa kujifungua, ajali n.k.
Kwahiyo wao wana damu nyingi na njia nyingi ya kutoa damu tofauti na wenzao wa kiume. Shetani anawapenda hawa wa kike kwa kuwa maungo yao ni rahisi kuwaingilia kwa kutumia tendo la ngono.
TENDO LA NGONO ni Agano rahisi kwa kuwa anakuwa anaziunganisha NAFSI za hawa watoto wa kike na mapepo yake,au waume wa kipepo.
Kwahiyo shetani anavyojua hawa watoto wana damu yenye uhusiano na Yesu ndipo hupenda kutumia Agano lenye nguvu na gumu kufunguka ambalo ni Agano la UMAUTI.
Hapa anamuapisha mzazi kwamba aseme binti yake/zake amewatoa moja kwa moja kwa mfalme mungu mkuu wa dunia (shetani) ili awe mume wao milele na milele na asikae akakiuka ndoa hii halali.
Wanaambatanisha kwamba kilichofungwa na Mungu mwanadamu asikifungue/asikitenganishe. (Wanaomba kinyume).
Akitaka kuivunja madhara yampate ikiwemo KIFO, kama jinsi mkataba ulivyoandikwa na cheti cha ndoa kilivyoandikwa ya kwamba binti yangu/zangu fulani na fulani nimewaozesha kwa mungu mkuu ambaye mume wenu atakuwa mume aitwaye PEPO MAUTI AU JINI MAITI.
Kwa kujua thamani ya maji yaliyomwagika msalabani. Wanatumia maji waliyooshea maiti, tena maiti iliyooza,kisha wanamnyesha huyu mtoto au watoto kwamba hii ni nadhiri na yamini kwamba sasa maji haya ya maiti yanakuunganisha na mume wako/wenu pepo maiti.
Hawataishia hapo tu,bali watamuosha au kuwaosha hawa watoto kwa kutumia hayo hayo maji waliyooshea maiti ili wamtakase katika ulimwengu wa giza kwa ajili ya kuolewa na huyo jini maiti.
Mambo yote haya yanafanyika kwa ajili ya kuua utu wa ndani,kuharibu nguvu za asili za ile damu ya Yesu ili anavyozidi kukua na kuongezeka na kupata maarifa asije akawasumbua.
Hapa ndipo KARAMA,VIPAWA,NDOTO NA NYOTA za watoto wa Mungu huanza kupotea, huandamwa na mikosi,nuksi kwa kila anachokifanya huwa hakifanikiwi.
Kwasababu yale maji yaliyooshea maiti iliyooza ndio hutumika kuleta roho za kuzaa mapooza na kumharibia maisha yake yote.
Mungu naye hayuko mbali huanza kumtafuta huyu mtoto/watoto wake.Hapa vita huibuka. Yeye anamtaka, na shetani hataki kumtoa, anadai alikabidhiwa na mzazi au wazazi wake.
Anatoa vifungu vyote vya mikataba,viapo na maagano waliyokubaliana na wazazi wake.
Mungu anaona isiwe taabu anaanza kumpa maarifa ya kutoka kwenye hivyo vifungo.
Njia rahisi, si nyingine bali damu ya Yesu. Kadri anavyozidi kutumia damu ya Yesu ndivyo yale maagano yaliyofanywa yanavyozidi kutoweka.Kwasababu ile damu ya huyu binti inazidi kuwa na nguvu kuzidi maagano yao yaliyofanyika au ambayo yalikuwa yakifanyika kwa kuchinja mnyama wa kafara.
Shetani anasema nilitumia maji ya maiti iliyooza, kwahiyo huyu atatakasika vipi?
Mungu ana maarifa zaidi ya shetani, Mungu anasema tumia maji yaliyomwagika msalabani kujiosha na kujtakasa.
Hapa ndipo nira huanza kukatika na kulegea hadi kuisha. Na zile nafsi za watu wote waliokuwa wamejiunganisha hapo kwenye hilo agano la utajiri ukatika pia.
Hapa itategemea waliapa viapo gani,kama ni viapo vya vifo, basi nafsi zao hukatika na mauti huwafikia Maana wao hawana damu iliyo safi na takatifu kama ya hawa waliokombolewa.
Kwahiyo huwa ni nafsi zao kupotea, sadaka zao ni damu yao.Shetani hapa hana msamaha;lazima uondoke maana anasema ulizipenda mali zangu kwahiyo huna budi kufa.
Vifo vya namna hii huwa havizuiliki maana huwa ni vya ghafla sana kwasababu vinasababishwa na huyo jini mauti au pepo mauti anayekuwa ni mauti katika mwili ila roho yake inafanya kazi kwa usaidizi wa mapepo mengine.
Turudi nyuma kidogo.
Na wanasema jinsi maiti alivyo wa baridi na mwili wa huyu binti uwe wa baridi,maisha yake yawe ya baridi ,asikae akawa na moto kwa kila akifanyacho.
Shetani hatendi kazi nje ya laana. Ni lazima kwanza aue vitu vya kiroho vilivyomo ndani ya mtu halafu apandikize roho nyingine ambazo ziko kinyume na mpango wa Mungu.
Kazi ya shetani na sifa kuu ya shetani ni kuiba, kuua na uongo.Anadanganya kwa kutenda kinyume na matarajio ya mwanadamu kisha anaua mpango wa Mungu ambao uko juu ya huyo mtu.
Mali za shetani hazidumu,utajiri wa shetani una mwisho wake.Lakini utajiri wa Mungu hauna mwisho wala ukomo;maana Yeye ndiye chanzo cha utajiri na mali.Shetani hana mali ispokuwa azipate kwa kuiba vitu walivyonavyo watoto wa Mungu.
KUNA WATU WANAFANYA VIAPO VYA KAFARA ZA NAFSI NA ROHO ZAO KWA AJILI YA MALI,UTAJIRI,MVUTO NA UMAARUFU.
Mtoto wa Mungu Kumbuka kule juu kichwa cha somo kilisemaje.Hapa ndipo tunakuja kwenye kiini cha somo.Kule nilikuwa ninawapitisha kwenye msingi wa haya maagano.
Wanafanya viapo hivi au vya namna hii kwa kujitoa wao kafara ili kwamba siku ikitokea mtu aliyekuwa ametolewa kafara akafunguka na kuyavunja maagano waliyokubaliana;basi wao ndio watumike kama mbadala wake.
Yaani zile nafsi za roho za watu wengine au ndugu,na jamaa zao walizokuwa wamezitoa kama sadaka za kafara kwa shetani,siku zikikombolewa kwa nguvu ya msalaba wa BWANA YESU basi wao hawana budi kutumikia kile kiapo chao cha awali.
Hapa ndipo watu hawa hujikuta wanadaiwa hizo mali,mvuto,utajiri,UMAARUFU, na cheo,na kwa kuwa walishaapa kwamba wao ndio watakuwa mbadala wake,hawawezi tena kupewa nafasi ya kuwatoa wengine.
Huwa wanaapa kwamba siku mtu huyu/hawa wakifunguka katika Kristo, basi mimi sina budi kuwa kafara kama mbadala wake.
Huwa wanajiaminisha na kuwa na ujasiri wa kufanya hivyo kwa vile wanajua vifungo walivyoviweka juu ya huyo mtu,havitawahi kuondolewa kamwe.
Lakini ashukuriwe Mungu aonaye sirini na kutujulisha mambo ya gizani. Jinsi anavyowapenda watu wake hata akaamua kumtoa mwanaye wa pekee ili awe KAFARA kwa ajili ya watu wake.
Naye si mwingine bali ni Yesu Kristo aliye hai.Yeye alivyokufa msalabani ilikuwa ni kafara ya ukombozi kwa wanadamu wote wa ulimwengu, ambao watahitaji msaada wake.
Hii kafara yake ndio inayoua nguvu za wale watu wote waliowatoa kafara ya viapo vya nafsi na roho ndugu zao au watoto wao au jamaa zao.
Kwa kuwa wao walitolewa kafara ya nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,na mvuto au cheo na umaarufu, hapa pia ukombozi wake unafanyika kwa njia ya Ukombozi wa kuuzwa nafsi yangu/zetu kwa shetani na baba,mama,kaka,mjomba,dada,bib na babu kwa kutumia kafara ya Yesu pale msalabani.
Hii ni lazima iandane na kanuni waliyoitumia kama ni kiapo, kivunjwe kwa kiapo.Kama ni sadaka ivunjwe kwa sadaka ,kama ni kafara ivunjwe kwa kafara katika ulimwengu wa Nuru,maana yote ya kwao yalifanyika katika ulimwengu wa giza.
TUSOME AYUBU 2:4
Shetani akamjibu BWANA,na kusema ,Ngozi kwa Ngozi,naam, yote aliyonayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
Kwahiyo shetani anavyokupa mali anategemea au anakupa kiapo cha kujitoa uhai iwapo kama utashindwa kukitunza kiapo chako na makubaliano yenu.
Ndio maana nikasema ni kiapo cha nafsi na roho kama kafara kwa ajili ya utajiri na mali,viapo vyako vinavyokuwa vikubwa, ndivyo na maagano yako yanavyozidi kuwa makubwa zaidi.
Maagano yako yanavyokuwa makubwa zaidi ndivyo na sadaka zako za kafara zinavyozidi kuwa nyingi na kubwa zaidi. Mtu haapi kwa shetani pasipo hakikisho la jambo analotaka kulifanya. Lazima kuwepo na kusudi au lengo.
Watu hawaendi kwenye ibada au maombi pasipo kusudi ndani ya mioyo yao;lazima wawe na dhamira iliyo ndani ya mioyo yao ambayo inawapelekea kwenda ibadani na kutaka maombi.
Dhamira hiyo ndio kusudi.Sasa tunaposema mtu anajitoa nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,mvuto,umaarufu, cheo au hata uchawi na uganga mkuu, ndio huo uhai anausema AYUBU.
KWANINI NI UHAI KWA AJILI YA UTAJIRI?
Kwasababu,nafsi inatunza roho,na roho ndio uhai wenyewe.Na mahali nafsi ya mtu ilipo ndipo mali yake ipo hapo.
Kwahiyo hawa watu wanatunza viapo vyao vya mali kwa kuzitoa au kuziweka nafsi na roho zao rehani ili mali zao zisiweze kupotea. Ili pia mtu waliyemuibia asiweze kuzidai.
Na ikitokea akaanza kuzidai basi umauti umkute;maana yeye alitolewa kama kafara kwa ajili ya mali za yule aliyeapa viapo vya nafsi na roho kwa ajili ya mali.
Ikitokea huyu aliyetolewa akawazidi nguvu na kuzichukua mali zake; ndipo ule usemi wa shetani unajidhihirisha,kwamba Ngozi kwa Ngozi na yote uliyonayo utayatoa kwa ajili ya uhai wako.
Lazima ajitoe yeye uhai wake,kwasababu hana mali tena,hana mtu tena wa kumtoa kafara maana si kila mtu unaweza kumtoa kafara, wengine damu zao ni chafu shetani hazihitaji.
Kwahiyo hapa inabidi wewe ndiye ufe kama mbadala wake.Tena mbaya zaidi yule aliyezikomboa yuko ndani ya Kristo;wanakuwa wanaona hakuna uwezekano tena wa kuzipata, maana nguvu zake hawaziwezi.
Shetani anamwambia uliapa kwamba utalizilinda, kwamba huyu uliyemtoa kafara hataweza kukuzidi nguvu,na uliapa hautanipa mwingine maana hakuna aliyekuwa na damu ya utakatifu kama huyu.
Sasa si mali zangu,si sadaka yako ya kafara, vyote vimeondoka, sasa ninauhitaji uhai wako mikononi mwangu,maana uliapa na kusaini HATI YA KIFO.Hivyo huna ujanja tena wa kutoka katika kiapo hiki
Hapa mtu hawezi kuchomoka tena.Hana jinsi tena ya kukwepa. Ndipo hujikuta mtu amekauka hapo hapo pasipo mjadala. Watu wanaapa hivi viapo pasipo kujua madhara yake huko mbeleni.
......................................................................
OMBA NAMI KWA IMANI SALA HII:
Sasa ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu uko ndani ya Yesu na unahitaji kujikomboa kutoka huko,ni vizuri na wewe kwenda na sheria,kanuni na utaratibu wao.
Wao wanafanyia gizani,wewe jiombee au fanyia nuruni.
Na wewe sema Ngozi kwa Ngozi katika kuchukua nyota yangu,mali zangu,utajiri wangu,pesa zangu,cheo changu kwa kubatilisha sadaka ya kafara ya mwili wangu kwa sadaka ya kafara ya mwili wa Yesu uliokufa msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kuchukua nafsi yangu, roho yangu na uhai wangu kudai mali zangu na vitu vyangu vyote vilivyokuwa vimetolewa kama sadaka ya uhai,kubatilisha viapo vyao vya uhai wangu kwa kutumia uhai wa Yesu Kristo uliotolewa kama kafara ya ulimwengu pale msalabani.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi,kudai mali zangu ambazo ni uhai wangu uliomo katika damu yangu uliotolewa sadaka ya uhai wa damu yangu kwa shetani ,nabatilisha viapo vya hao Watu kwa kutumia sadaka ya kafara ya uhai uliomo katika damu ya Yesu.
Hii itakusaidia kuua kila chembe chembe za mawasiliano ambazo shetani alizipandikiza katika damu yako ili aweze kujua baraka zako zinazoingia ndani yako ambazo Mungu amezirejesha kwako.
Sina muda wa kutosha kufafanua sana ila twende na mtiririko huu.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi kwa ajili ya kubatilisha viapo vya nafsi vilivyoapwa juu yangu ili maji yaliyomo mwilini mwangu yatumike kama maji ya uzima kwa ajili ya shetani; sasa ninayabatilisha kwa kafara ya maji ya Yesu yaliyomwagika msalabani ili yanirejeshee uzima wangu maeneo yote.
Endelea kusema, Ngozi kwa Ngozi, wale wote waliodhani kwamba nitakufa siku ya kuzidai mali zangu kwa wao kujiapisha viapo vya nafsi,sasa sitakufa maana BwanaYesu alikishinda kifo kwa kafara ya msalabani,wao ndio watakufa na kuniachia baraka zangu zote.
Bwana Yesu alikishinda kifo kwa ajili yangu au yetu kwa kujitoa kafara pale msalabani, hivyo hamna mamlaka yoyote kuendelea kutushikilia katika viapo vya kafara za nafsi na roho kwa ajili ya mali na utajiri.
Ngozi kwa Ngozi: Viapo vyote vilivyoapwa kwa ajili yangu au yetu juu ya kuibiwa baraka za ku-renew au kurejesha mikataba ya kila mwisho wa mwaka ,sasa visiapwe tena kwasababu baraka zangu zinalindwa ndani ya kiapo cha damu ya Yesu iliyotolewa kafara pale msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kwa wale wote walioapa viapo vya nafsi ili miungu izuilie baraka zetu zisiturudie, sasa miungu yote haina nguvu tena ,kwasababu kimiminika cha damu ya Yesu mara 12 iliyomwagika msalabani ninakimimina juu ya miungu 12 na miungu yote inayozuia baraka zetu iungue hadi iachie baraka zetu zote na ziturudie.
Ngozi kwa Ngozi, vile viapo vyote vilivyofanywa na wazazi ,ndugu ,jamaa na marafiki juu yetu wakaapa kwamba hata kama watakufa ,basi viapo vyao vife katika uhai wa kuendelea kutumika.
Ya kwamba hata siku moja tusikae tukazirejesha baraka zetu kama jinsi ile miili iliyofanya viapo hivyo haiwezi kurejewa na uhai tena.Ngozi kwa Ngozi kama ambavyo Yesu alirejewa na uhai katika mwili wake ,na sisi tunazirejesha baraka zetu ambazo ziko katika miili yote ambayo ni marehemu iliyokufa katika viapo vya nafsi na roho zao.
Ngozi kwa Ngozi. Vile viapo mlivyoviapa kwamba mwezi huu wa 12 hatutauvuka na kuuona mwaka mpya, tayari tumeshavuka kwa kafara ya matone 12 ya damu ya Yesu aliyekafarishwa pale msalabani.Amen.
.............................................................
Mpenzi msomaji mtoto wa Mungu hapo lazima uwe katika roho uombe haya maombi kwa imani ili uweze kutoka katika vifungo hivi vya nguvu za giza na makafara yaliyofanyika juu yako.
Ninawatahadharisha haya maombi siyo ya kitoto wala masihara yeyote aliyekuwa amememfanyia ndugu yake maagano ya namna hii, maombi haya ni upanga wa Mungu, sijui utakataje lakini habari mtaipata.
Kipindi hiki siyo cha mzaha na mimi huduma yangu ni ya kuvunja madhabahu na maagano, kwahiyo sina maombi ya rehema kwa waovu, upanga kwa upanga na jino kwa jino.
Naachiliaa moto wa Yesu kwa kila mchawi na mganga wa kienyeji na yeyote aliye na mpango wa kunitumia roho za mauti zimrudie yeye na wote waliojipanga kuwa kinyume nami.
Nawazingira wote wanisomao kwa nia ya kupata maarifa kutoka kwa Mungu uliye juu uwakinge na roho za visasi kutoka katika madhabahu za miungu yao ambazo kuanzia sasa wanaanza kuzipiga na kuzivunja katika Jina la Yesu Kristo aliye hai.
Mtoto wa Mungu ikiwa una sadaka itoe kwa imani na Mungu atakujibu katika maombi yako. Sindikiza maombi yako kwa njia ya kutoa sadaka.
Ahsante Bwana Yesu kwa ajili ya hizi roho ambazo nimezikomboa kwa mamlaka ya Jina lako,nazikukabidhi uzitunze na kuzilinda isipotee hata roho moja mpaka siku ile unarudi uikute iko kundini na uweze kuinyakua na kwenda nayo juu mbinguni kwa Baba,Amen.
MUNGU AWABARIKI SANA WATOTO WA MUNGU.
Mkuu unamaanisha astral projectionsOk,nimekupata mkuu,hilo ni zoezi la kutenga nafsi,mwili na roho na kuelekeza nguvu nyingi kwenye roho ili kuipa nguvu ya kufanya marekebisho kwenye nafsi na mwili.Nayo inafanya kazi ila usipokuwa makini roho inaweza kujitenga moja kwa moja.Asante kwa elimu na kama unaweza kuelezea zaidi itakuwa vizuri.
Sawa,tulia kwanza huku ukiendelea na huo utaratibu wa kusali kwa njia ya redio na television, soma sana neno la Mungu. Jiwekee utaratibu wa kusoma Biblia kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo ili uweze kupata maarifa mengi na kuwa na maadiko ya kutosha.asante mwalimu,nakaa musoma
Amen.Ubarikiwe sana mtu wa Mungu kwa haya unayoyashuhudia maana ni ukamilifu na utimilifu kwamba Injili imehubiriwa na imepokelewa kwa ushuhuda wa Neno la Mungu katika madhabahu hii.Amen, tumebarikiwa Mtumishi, Atukuzwe Mungu baba kwa njia ya Yesu Kristo kwa kutukomboa kwa Damu yake takatifu, ninashukuru sana kwa zawadi na Neema ya Wokovu, Rehema ya Yesu Kristo ni kubwa sana kwa sisi tunaoamini na Mimi Leo muda huu ninshuhudiwa na roho ndani yangu nimepokea Neema na Rehema kwa sababu nimekisogelea kiti cha Neema na Rehema kwa ujasiri na nimeongozwa kwenye madhabau hii na kujaliwa mahitaji yote ya Wokovu, atukuzwe Mungu Mkuu litukuzwe Jina lake Takatifu kwa njia ya Yesu Kristo na Damu yake Takatifu, nashukuru Mimi nina uhai na uzima tele kwa kujiunga na madhabau hii, Mwana ameniweka huru na nipo huru kweli kweli. Yesu ni Bwana na Mwokozi wa maisha yangu, naombea wote tunaoamini tupokee Neema hii Amen.
Mungu yu pamoja nasi.
OkNawasalimu wote wanajukwaa,leo nataka tujifunze silaha kuu tano zinazotumika katika ulimwengu wa kiroho.
Kama wengi tunavyojua kuwa katika ulimwengu wa kiroho kuna falme kuu mbili,falme ya kwanza ni ufalme wa nuru na falme ya pili ni ufalme wa giza.
Falme zote hizi zina muundo na uongozi na mamlaka kamili.Katika viumbe vyote binadamu ndiyo kiumbe pekee mwenye sifa ya kuweza kuishi katika ulimwengu wa kiroho na ulimwengu huu wa kimwili kwa wakati mmoja.Inawezekana umesoma vitabu vingi sana na kufanya jitihada nyingi sana ili ufanikiwe katika maisha yako lakini bado umeshindwa.
Nakushauri fuatilia darasa hili kwa umakini na siku ukimaliza Lazima ufanikiwe kwa kuwa manbo yote huanzia katika ulimwengu wa kiroho na ndicho utakachojifunza hapa.
Zifuatazo ni silaha kuu tano za ulimwengu wa kiroho.
1. Damu
2. Jina
3. Kiti
4. Maneno
5. Ardhi na Mbingu
Ukiweza kujifunza silaha hizi kwa umakini,utaweza kujua ulimwengu wa kiroho unavyofanya kazi,utapata nguvu za kuingia katika ulimwengu wa kiroho,utashinda vita vya kiroho na kimwili kwa urahisi na utafanikiwa kimwili na kiroho katika mambo yako.
Somo hiki litakuwa na jumla ya vipande kumi (10),yaana tutajadili silaha moja moja inavyotumika katika ulimwengu wa kiroho upande wa ufalme wa giza na moja moja inavyotumika katika ulimwengu wa kiroho upande wa ufalme wa nuru.
Naomba maoni yenu ya tuanze kuijadili silaha ipi, na tuanze na falme ipi kati ya falme ya nuru au ya giza au somo liishie hapa maana watu wengi hawaamini kama kuna ulimwengu wa kiriho.
AMENTumekombolewa katika Yeye atutiaye Nguvu, Amina mtumishi wa Mungu, tumelipokea somo kwa Roho
Asante sana Mkuu kwa tag hii,Saint Anne kama utapata kibali, basi Nakukaribisha hapa ili tuendelee kujifunza
Amen! Namshukuru Mungu sana kwa kubarikiwa na masomo haya,namuomba Mungu azidi kuwabariki na wengine kama alivyokubariki wewe katika Jina la Yesu Kristo aliye hai. Amen.Ninabarikiwa sana mtumishi wa Mungu na mafundisho yako,ubarikiwe nawe katika kazi yako ya utumishi,kwa jina la Yesu Kristo aliye hai,Amen...
Maombi haya ya Ngozi kwa Ngozi.Yaombeni kwa muda siku 7 pasipo kuruka hata siku moja.Pia hayana mwisho ni kama Zaburi ,kwahiyo mtu anaweza kuyaomba wakati wowote anapohitaji baada ya hizo siku 7.AGANO LA KISHETANI LA UTAJIRI,MALI,CHEO,MVUTO(MAFANIKIO) KATIKA MAUTI ZA NAFSI NA ROHO ZA HAO WAUTAFUTAO UTAJIRI:
17.12.2023.
Bwana Yesu apewe sifa sana.Nimerudi tena kwenu kuwapasha habari za ufalme wa Mungu na siri za kuzimu ili mpate kuzijua na kuzishinda hila za shetani.
Ujumbe huu unakuja kwenu hasa watumishi wa Mungu aliye hai ili mpate mbinu au kama mnazo hizi basi mziboreshe kupitia hiki nitakachokisema hapa.
Siyo kwamba mimi ni msemaji wenu,siyo kwamba mimi ninajua kuliko nyinyi,au siyo kwamba mimi ninafundishwa peke yangu,la hasha! Msinifikirie vibaya,mimi ninasema kitu nilichoambiwa nikiseme.
Kwako kinaweza kisiwe na manufaa, ila kwa wengine ni msaada mkubwa sana,hivi kwanini mtumishi wa Mungu huduma yako haikui, kwanini watu wakucheke kwamba huduma yako ni ya kimasikini?
Yaani wachawi wachezee kwenye madhabahu yako na kuinajisi halafu wewe uhubiri watu wasipone ,bado uyakatae haya maarifa.?
Baada ya masomo haya ninakuomba mtumishi wa Mungu tusaidiane kuzivunja hizi madhabahu za miungu,wachawi,waganga wa kienyeji na washirikina wote wapate kubarikiwa na moto wa Mungu.
Yaani tuwabariki kwa moto,tuwabariki kwa upanga wa Mungu, tuwabarikie kwa damu ya Yesu viwachome hadi wateketee mpaka wafuasi wao waseme huu ni ubarikio wa namna gani.
Naam! Nasi tutawaambia huu ni ubarikio wa moto wa Mungu, damu ya Yesu,Jina la Yesu na upanga wa Mungu kuanzia 2024 mpaka Yesu anarudi kutunyakua.
Mizaha sasa imetosha juu ya kanisa la BWANA na kwa watu wa Mungu. Mtumishi wa Mungu bila kuwa na hasira ya kimungu huwezi kutoka kwenye hayo maagano yanayokukwamisha wala hautaweza kutoboza.
Omba kama kichaa, omba kama mwendawazimu, usiweke silaha chini mpaka uone maadui zako wamesalimu amri,huwezi kuvikwa taji kama hujapata ushindi. Ushindi wa kwanza ni hapa hapa duniani. Usimchekee shetani,usimuonee aibu shetani atakuiabisha ukweni kwako.
Ukali wenu nitauona kwenye matokeo ya shuhuda zenu.Mimi nimevipiga vita sana nikiwa nyikani, ninajua hiki ninachokiongea, hakuna miungu wala shetani itakayoweza kusimama mbele yangu na ikashinda, Kwasababu Yesu aliye ndani yangu ni mkuu kuliko wote,lazima nimtukuze mahali popote pale atakaponituma, ila ninaanzia hapa nyumbani kwanza.
MUNGU AWABARIKI SANA:
Mwili wa mwanadamu usiokuwa na uhai huitwa maiti. Ni maiti kwasababu umekutwa na umauti.
Umauti ni roho ya kifo ambayo humvaa mtu na kuondoka na uhai wake.Uhai huu ukiondolewa ndani ya nafsi ya mtu ndipo mtu huwa mfu, nafsi isiyokuwa na uhai wala utambuzi wa aina yotote ile.
Mwili hupelekwa na kuhifadhiwa katika nyumba yake ya milele iitwayo Kaburi.Na hapa ndipo neno la BWANA linapotimizwa kwamba umeumbwa kwa udongo, utarudi tena udongoni.
Hakuna mwanadamu awezaye kukishinda kifo isipokuwa Yesu peke yake na wale waliopata neema mbele za macho ya BWANA.
Hawa ni wale walioandikiwa haki mbele za kiti cha enzi cha Mungu Baba.
Hata shetani na mbinu zake zote hawezi kukishinda wala kukiepuka;kwasababu tangu kipindi kile alivyoasi, alishahukumiwa adhabu ya kifo katika lile ziwa likawalo moto.
Watenda dhambi wote hukumu yao ilishatoka, ambayo ni kifo cha umauti wa milele pamoja na shetani.Labda wale watakaopata neema ya kuisikia Injili ya Yesu,hao ndio watakaourithi Uzima wa Milele.
Waliokufa katika dhambi,wote ni mauti ya milele maana watatupwa katika lile ziwa liwakalo moto usiku na mchana pasipo kuzimika.
Pamoja na kwamba mtu anakufa mwili wake na roho yake kwenda sehemu nyingine.Lakini kuna watu wengine wanaandikiwa VIFO WAKINGALI HAI,WANATEMBEA HUKU ROHO WA UMAUTI AKIWA JUU YAO.
Hapa kinachosubiriwa ni muda ,saa na sababu itakayomsababishia umauti. Vifo vya namna hii haviji pasipo sababu maalumu.
Inaweza kuwa ni sababu ya uchawi, visasi, chuki,wivu,maagano ya kichawi yaliyofanywa huko nyuma na wazazi au mababu za hao watu.n.k.
Wengine ni laana inayotoka ndani ya ukoo wa huyo mtu.Huyu roho akishamvaa mtu hujikuta anaanza kujichukia, kukata tamaa na kukosa matumaini, hukosa raha na uchangamfu, hupenda kujitenga na watu,pia ni mtu wa kuwa na wasiwasi wakati wote.
Akimtazama mtu usoni huwa na aibu aibu huku akiangalia chini,huyu ni roho anakuwa anajua unamuona ila ni ngumu kung'amua katika mwilini, uso wa huyu mtu hukosa nuru na kuwa na mpauko usoni kama rangi ya maiti.
Huwezi kumshinda roho wa mauti isipokuwa kwa njia ya nguvu ya MSALABA WA BWANA YESU.
Yesu alivyosema pale msalabani "IMEKWISHA",Alikuwa anaitoa roho yake ili kwenda kuzimu alipo shetani kumnyang'anya funguo za uzima na mauti na kuisimamisha juu ya watu wake wote dunia nzima.
Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya watu wote, watu wasidanganye eti alikufa kwa ajili ya Wakristo tu,siyo kweli yeyote anayeliamini Jina lake ni wake Yeye Kristo.
Pale ilikwisha nguvu,ilikosa uhalali wa kutuua kwasababu hati zote za mashtaka zilipigiliwa pale msalabani. Tulipewa uzima wa Milele mara tu baada ya kufufuka na kwenda(kupaa) juu mbinguni kwa Baba yetu.
Wanadamu wanapotea na kufa vifo ambavyo siyo vyao wala vifo vya haki kwasababu hawana maarifa ya Mungu, na kwa kuwa wamemkataa Yesu na kuamua kumfuata shetani.
Shetani amewadanganya na kuwapotosha macho yao ili wasipate kuona na kuijua kweli,neema na thamani ya nguvu ya msalaba iletayo ukombozi ndani ya mtu,badala yake wameyakumbatia mafundisho manyonge na madhaifu kwa kujipa matumaini kwamba mtu akifa ataombewa na kupata msamaha wa ondoleo la dhambi.
Wanasahau kwamba imeandikwa "bora wafu wafao katika BWANA maana hao watafufuliwa siku ya mwisho".
Maana yake ni watu waliokufa katika Kristo Yesu.
Hakuna siku ya mwisho nyingine, bali ni sasa,hizi ndizo nyakati za mwisho ambazo Bwana Yesu yuaja upesi kuja kulinyakua kanisa lake,ambapo kabla ya ujio wake atawaandaa watakatifu wake ili wapate kumpokea mawinguni.
Hata wale wafu waliokufa katika BWANA ambao maandiko yanawataja, watafufuliwa kwanza ili waungane na walio hai,waliolikiri Jina Langu.Hawa ni wateule Wangu na watakatifu WANGU, niliopendezwa nao.(JESUS SPEAKS HIMSELF THROUGH ME).
Wale waliolikataa Jina langu ,na wale walio vuguvugu;wale waniitao BWANA,BWANA.Lakini hapo hapo wanajihudhurisha kwa miungu ,hao sina haja nao.(Yesu anaongea saa hii).
Nitawakataa, nitawatema, hawataingia RAHANI Mwangu,maana hawa ni wafu wanaoishi. Hawajafa katika BWANA wala hawaishi katika maisha matakatifu. (Roho yake imeongea ndani yangu,kuweni makini watu wa Mungu).
Kumbuka Andiko "waache wafu wazikane. ".Hawa ni wafu maana hawana walijualo, linaloendelea katika UFALME WA MUNGU.
Hawajui saa wala dalili za kuja kwa Mwana wa Adamu.Akili zao na fahamu zao haziwazi yaliyo ya Mungu, bali hujitaabisha na mambo ya dunia na kujihudhurisha kwa shetani.
WANAZIKANA KWA NAMNA GANI?
Roho wa umauti anawasubiria ili aweze kuwavaa na kuwachukua maana hawana kinga wala zuio au kizuizi chochote. Yeye asiye na Yesu ana roho wa umauti anatembea naye,anasubiri apate chanzo na sababu ili amvae na kuondoka naye.
Kuna wengine wameandikiwa umauti au kifo na wazazi wao,ndugu zao, Rafiki zao,na jamaa zao KAMA KAFARA LA UTAJIRI NA MALI.
Shetani hupenda kujifananisha na Mungu. Jinsi Yesu alivyotolewa kafara kama ondoleo la dhambi ya Ulimwengu, ndivyo hivyo hivyo shetani apendavyo kupewa kafara ya damu ya mtu.
Kafara ya damu ya mtu ina thamani kubwa kuliko damu ya mnyama,Kwasababu ina uhusiano na damu ya Yesu.Damu ya Yesu ina uungu mkuu sana,hivyo wote walio na Yesu wana damu kama Yake.
Mtu wa Mungu nisome kwa umakini sana hapa.
Maandiko yanasema,Yesu alisema yeyote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni,huyu ndiye ndugu yangu,na umbu langu,na mama yangu.Umbu kwa lugha nyingine ni dada.
Kwahiyo watu hawaitwi ndugu pasipo kuwa na vinasaba vya damu.
Unadhani kwanini sisi Watanzania huwa tunaitana kaka na dada? Maana tunachukuliana kama ndg wamoja. Kiroho sisi ni ndg sana,ndio maana utasikia ndg yetu,zetu Watanzania wamepatwa na shida fulani tuwasaidie.
Sasa twende kwa Yesu kwa mtiririko wa hapo juu.
Tumerithi ufalme wa Mungu kupitia imani ya baba yetu Ibrahimu,Yesu ni ukoo wa Yuda mtoto wa Yakobo,Yakobo ni mjukuu wa Ibrahimu.
Yesu anatokea katika shina la Daudi ,ambalo ni ukoo wa Yuda. Hivyo basi Yesu alikuwa na damu ya kibinadamu kamili kwasababu pia alizaliwa na mwanamke kama vile ambavyo watoto wote huzaliwa na mwanamke.
Kwahiyo kitendo cha Yesu kusema sisi tulio wake ni ndugu zake,maana yake katika imani tunakuwa katika ukoo mmoja na Baba yake ndiye Baba yetu pia. Glory to God, hallelujah!!!
Kwahiyo katika ulimwengu wa roho kinaumbika kitu kipya.Maana hata maandiko yanasema sisi tumefanyika viumbe vipya ndani ya Yesu.Tumebadilishwa kutoka ule utu wa kale na kuwa mpya ndani ya Kristo Yesu.
Tunafanyika kuwa watoto wa Mungu kwasababu tumebadilishwa na kuwa na sifa kama za Mungu wetu aliyetuumba. Kwahiyo kila kitu chetu ni kipya.
Damu yetu ni mpya kwasababu imetakaswa upya, imechujwa na kuwa safi na damu halisi.
Kwahiyo hii damu ndio ambayo shetani anaiwinda usiku na mchana ili aweze kuipata na kuichukua. Hii ina nguvu kuliko damu ya viumbe vyote.
Wanyama hawana damu safi,salama,na yenye thamani kama damu ya mtu;mtu aliyeokoka. Hii damu akiinywa shetani inampa nguvu na mafunuo kujua kitu gani kinaendelea katika ulimwengu wa roho wa NURUNI.
Yesu alisema Yeye ni nuru ya Ulimwengu.Kwahiyo katika vinasaba vya damu yake zipo chembe chembe ambazo zimebeba maono na mafunuo yenye taarifa sahihi za siri za mbingu.
Kwa kuwa Yesu anao ndugu zake ambao ni watoto wake,ambao ni watoto wa Mungu, basi hujikuta damu Yake iko sawa sawa na ndugu zake hawa,watu waliomkiri au waliokiri Jina Lake.
Lasivyo asingesema, sisi ni ndugu zake.Na ndugu zake wote ni wana wa Mungu walio ndani ya Yesu.Yesu ni ukoo wa watoto wote waliozaliwa mara ya pili kwa ajili ya Mungu.
Kwahiyo Yesu anawakilisha ukoo wa Mungu kwa watoto wa Mungu, akiwa Yeye ndiye mzaliwa wa kwanza. Ndio maana shetani anapenda kuwashikilia watoto wote waliozaliwa wakiwa wa kwanza,Kwasababu ni malango.
Ni malango kwasababu ni kielelezo cha Yesu Kristo. Kama alivyo Lango la baraka,uzima wa milele na mrithi wa viti vyote vya Enzi vya baba yetu.
Mtoto wa kwanza akiwa ni lango la laana,basi watoto wote watakaofuata watapata laana na mikosi.Labda tu kwa neema ya msalaba na damu iliyomwagika msalabani ipate kuwakomboa na kuwaweka huru.
Mtoto wa kwanza akiwa ni baraka ,halafu yuko upande wa Mungu ;Yaani yuko ndani ya Yesu.Shetani hupenda damu yake maana anajua atapata taarifa zote zilizomo kwake na kujua mpango wa Mungu ili aweze kumuibia na kisha kumakwamisha.
Kuna watoto wanaozaliwa na Nuru ya ulimwengu. Hawa tangu wakiwa tumboni mwa mama zao tayari Mungu alishawapaka mafuta.
Maandiko yanasema kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa;nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Angalia hapa Kumbe Mungu anawajua watoto wake. Shetani naye akishawajua anaanza utaratibu wa kuwashika. Hawezi kuwashika Wala kuwamiliki pasipokuwa na ridhaa ya wazazi,ndugu au jamaa zake.
Atakachokifanya ni kumshawishi mzazi kupitia kwa wachawi,waganga wa kienyeji, wazee wa mila na waaguzi waonao kwa kutumia mapepo ya utambuzi.
Kwamba wamtoe huyo mtoto madhabahuni kwao;kisha yeye watampatia nyota ya utajiri.
Hata kama ni cheo, au mafanikio mengine, lakini mafanikio yoyote huleta mali na vitu zikiwemo fedha. Hivi vitu vyote au wingi wa vitu mbalimbali, au wingi wa mali ni UTAJIRI.
Kwasababu ya tamaa ya mwanadamu ya kupenda pesa na utajiri hujikuta anamtoa au anawatoa watoto wake ili wawe kafara ya ngekewa yake.
Wapendwao kutolewa kafara huwa ni mabinti. Kwasababu hawa huwa ni rahisi kutoa damu zao kama sadaka kwa njia nyingi tofauti na watoto wa kiume ambao wao damu zao ni mpaka wapate ajali na vifo vyao.
Hawa watoto wa kike damu zao huanza kutoka pale wanapovunja ungo, damu ya ubikra, damu ya hedhi ya kila mwezi, damu ya wakati wa kujifungua, ajali n.k.
Kwahiyo wao wana damu nyingi na njia nyingi ya kutoa damu tofauti na wenzao wa kiume. Shetani anawapenda hawa wa kike kwa kuwa maungo yao ni rahisi kuwaingilia kwa kutumia tendo la ngono.
TENDO LA NGONO ni Agano rahisi kwa kuwa anakuwa anaziunganisha NAFSI za hawa watoto wa kike na mapepo yake,au waume wa kipepo.
Kwahiyo shetani anavyojua hawa watoto wana damu yenye uhusiano na Yesu ndipo hupenda kutumia Agano lenye nguvu na gumu kufunguka ambalo ni Agano la UMAUTI.
Hapa anamuapisha mzazi kwamba aseme binti yake/zake amewatoa moja kwa moja kwa mfalme mungu mkuu wa dunia (shetani) ili awe mume wao milele na milele na asikae akakiuka ndoa hii halali.
Wanaambatanisha kwamba kilichofungwa na Mungu mwanadamu asikifungue/asikitenganishe. (Wanaomba kinyume).
Akitaka kuivunja madhara yampate ikiwemo KIFO, kama jinsi mkataba ulivyoandikwa na cheti cha ndoa kilivyoandikwa ya kwamba binti yangu/zangu fulani na fulani nimewaozesha kwa mungu mkuu ambaye mume wenu atakuwa mume aitwaye PEPO MAUTI AU JINI MAITI.
Kwa kujua thamani ya maji yaliyomwagika msalabani. Wanatumia maji waliyooshea maiti, tena maiti iliyooza,kisha wanamnyesha huyu mtoto au watoto kwamba hii ni nadhiri na yamini kwamba sasa maji haya ya maiti yanakuunganisha na mume wako/wenu pepo maiti.
Hawataishia hapo tu,bali watamuosha au kuwaosha hawa watoto kwa kutumia hayo hayo maji waliyooshea maiti ili wamtakase katika ulimwengu wa giza kwa ajili ya kuolewa na huyo jini maiti.
Mambo yote haya yanafanyika kwa ajili ya kuua utu wa ndani,kuharibu nguvu za asili za ile damu ya Yesu ili anavyozidi kukua na kuongezeka na kupata maarifa asije akawasumbua.
Hapa ndipo KARAMA,VIPAWA,NDOTO NA NYOTA za watoto wa Mungu huanza kupotea, huandamwa na mikosi,nuksi kwa kila anachokifanya huwa hakifanikiwi.
Kwasababu yale maji yaliyooshea maiti iliyooza ndio hutumika kuleta roho za kuzaa mapooza na kumharibia maisha yake yote.
Mungu naye hayuko mbali huanza kumtafuta huyu mtoto/watoto wake.Hapa vita huibuka. Yeye anamtaka, na shetani hataki kumtoa, anadai alikabidhiwa na mzazi au wazazi wake.
Anatoa vifungu vyote vya mikataba,viapo na maagano waliyokubaliana na wazazi wake.
Mungu anaona isiwe taabu anaanza kumpa maarifa ya kutoka kwenye hivyo vifungo.
Njia rahisi, si nyingine bali damu ya Yesu. Kadri anavyozidi kutumia damu ya Yesu ndivyo yale maagano yaliyofanywa yanavyozidi kutoweka.Kwasababu ile damu ya huyu binti inazidi kuwa na nguvu kuzidi maagano yao yaliyofanyika au ambayo yalikuwa yakifanyika kwa kuchinja mnyama wa kafara.
Shetani anasema nilitumia maji ya maiti iliyooza, kwahiyo huyu atatakasika vipi?
Mungu ana maarifa zaidi ya shetani, Mungu anasema tumia maji yaliyomwagika msalabani kujiosha na kujtakasa.
Hapa ndipo nira huanza kukatika na kulegea hadi kuisha. Na zile nafsi za watu wote waliokuwa wamejiunganisha hapo kwenye hilo agano la utajiri ukatika pia.
Hapa itategemea waliapa viapo gani,kama ni viapo vya vifo, basi nafsi zao hukatika na mauti huwafikia Maana wao hawana damu iliyo safi na takatifu kama ya hawa waliokombolewa.
Kwahiyo huwa ni nafsi zao kupotea, sadaka zao ni damu yao.Shetani hapa hana msamaha;lazima uondoke maana anasema ulizipenda mali zangu kwahiyo huna budi kufa.
Vifo vya namna hii huwa havizuiliki maana huwa ni vya ghafla sana kwasababu vinasababishwa na huyo jini mauti au pepo mauti anayekuwa ni mauti katika mwili ila roho yake inafanya kazi kwa usaidizi wa mapepo mengine.
Turudi nyuma kidogo.
Na wanasema jinsi maiti alivyo wa baridi na mwili wa huyu binti uwe wa baridi,maisha yake yawe ya baridi ,asikae akawa na moto kwa kila akifanyacho.
Shetani hatendi kazi nje ya laana. Ni lazima kwanza aue vitu vya kiroho vilivyomo ndani ya mtu halafu apandikize roho nyingine ambazo ziko kinyume na mpango wa Mungu.
Kazi ya shetani na sifa kuu ya shetani ni kuiba, kuua na uongo.Anadanganya kwa kutenda kinyume na matarajio ya mwanadamu kisha anaua mpango wa Mungu ambao uko juu ya huyo mtu.
Mali za shetani hazidumu,utajiri wa shetani una mwisho wake.Lakini utajiri wa Mungu hauna mwisho wala ukomo;maana Yeye ndiye chanzo cha utajiri na mali.Shetani hana mali ispokuwa azipate kwa kuiba vitu walivyonavyo watoto wa Mungu.
KUNA WATU WANAFANYA VIAPO VYA KAFARA ZA NAFSI NA ROHO ZAO KWA AJILI YA MALI,UTAJIRI,MVUTO NA UMAARUFU.
Mtoto wa Mungu Kumbuka kule juu kichwa cha somo kilisemaje.Hapa ndipo tunakuja kwenye kiini cha somo.Kule nilikuwa ninawapitisha kwenye msingi wa haya maagano.
Wanafanya viapo hivi au vya namna hii kwa kujitoa wao kafara ili kwamba siku ikitokea mtu aliyekuwa ametolewa kafara akafunguka na kuyavunja maagano waliyokubaliana;basi wao ndio watumike kama mbadala wake.
Yaani zile nafsi za roho za watu wengine au ndugu,na jamaa zao walizokuwa wamezitoa kama sadaka za kafara kwa shetani,siku zikikombolewa kwa nguvu ya msalaba wa BWANA YESU basi wao hawana budi kutumikia kile kiapo chao cha awali.
Hapa ndipo watu hawa hujikuta wanadaiwa hizo mali,mvuto,utajiri,UMAARUFU, na cheo,na kwa kuwa walishaapa kwamba wao ndio watakuwa mbadala wake,hawawezi tena kupewa nafasi ya kuwatoa wengine.
Huwa wanaapa kwamba siku mtu huyu/hawa wakifunguka katika Kristo, basi mimi sina budi kuwa kafara kama mbadala wake.
Huwa wanajiaminisha na kuwa na ujasiri wa kufanya hivyo kwa vile wanajua vifungo walivyoviweka juu ya huyo mtu,havitawahi kuondolewa kamwe.
Lakini ashukuriwe Mungu aonaye sirini na kutujulisha mambo ya gizani. Jinsi anavyowapenda watu wake hata akaamua kumtoa mwanaye wa pekee ili awe KAFARA kwa ajili ya watu wake.
Naye si mwingine bali ni Yesu Kristo aliye hai.Yeye alivyokufa msalabani ilikuwa ni kafara ya ukombozi kwa wanadamu wote wa ulimwengu, ambao watahitaji msaada wake.
Hii kafara yake ndio inayoua nguvu za wale watu wote waliowatoa kafara ya viapo vya nafsi na roho ndugu zao au watoto wao au jamaa zao.
Kwa kuwa wao walitolewa kafara ya nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,na mvuto au cheo na umaarufu, hapa pia ukombozi wake unafanyika kwa njia ya Ukombozi wa kuuzwa nafsi yangu/zetu kwa shetani na baba,mama,kaka,mjomba,dada,bib na babu kwa kutumia kafara ya Yesu pale msalabani.
Hii ni lazima iandane na kanuni waliyoitumia kama ni kiapo, kivunjwe kwa kiapo.Kama ni sadaka ivunjwe kwa sadaka ,kama ni kafara ivunjwe kwa kafara katika ulimwengu wa Nuru,maana yote ya kwao yalifanyika katika ulimwengu wa giza.
TUSOME AYUBU 2:4
Shetani akamjibu BWANA,na kusema ,Ngozi kwa Ngozi,naam, yote aliyonayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
Kwahiyo shetani anavyokupa mali anategemea au anakupa kiapo cha kujitoa uhai iwapo kama utashindwa kukitunza kiapo chako na makubaliano yenu.
Ndio maana nikasema ni kiapo cha nafsi na roho kama kafara kwa ajili ya utajiri na mali,viapo vyako vinavyokuwa vikubwa, ndivyo na maagano yako yanavyozidi kuwa makubwa zaidi.
Maagano yako yanavyokuwa makubwa zaidi ndivyo na sadaka zako za kafara zinavyozidi kuwa nyingi na kubwa zaidi. Mtu haapi kwa shetani pasipo hakikisho la jambo analotaka kulifanya. Lazima kuwepo na kusudi au lengo.
Watu hawaendi kwenye ibada au maombi pasipo kusudi ndani ya mioyo yao;lazima wawe na dhamira iliyo ndani ya mioyo yao ambayo inawapelekea kwenda ibadani na kutaka maombi.
Dhamira hiyo ndio kusudi.Sasa tunaposema mtu anajitoa nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,mvuto,umaarufu, cheo au hata uchawi na uganga mkuu, ndio huo uhai anausema AYUBU.
KWANINI NI UHAI KWA AJILI YA UTAJIRI?
Kwasababu,nafsi inatunza roho,na roho ndio uhai wenyewe.Na mahali nafsi ya mtu ilipo ndipo mali yake ipo hapo.
Kwahiyo hawa watu wanatunza viapo vyao vya mali kwa kuzitoa au kuziweka nafsi na roho zao rehani ili mali zao zisiweze kupotea. Ili pia mtu waliyemuibia asiweze kuzidai.
Na ikitokea akaanza kuzidai basi umauti umkute;maana yeye alitolewa kama kafara kwa ajili ya mali za yule aliyeapa viapo vya nafsi na roho kwa ajili ya mali.
Ikitokea huyu aliyetolewa akawazidi nguvu na kuzichukua mali zake; ndipo ule usemi wa shetani unajidhihirisha,kwamba Ngozi kwa Ngozi na yote uliyonayo utayatoa kwa ajili ya uhai wako.
Lazima ajitoe yeye uhai wake,kwasababu hana mali tena,hana mtu tena wa kumtoa kafara maana si kila mtu unaweza kumtoa kafara, wengine damu zao ni chafu shetani hazihitaji.
Kwahiyo hapa inabidi wewe ndiye ufe kama mbadala wake.Tena mbaya zaidi yule aliyezikomboa yuko ndani ya Kristo;wanakuwa wanaona hakuna uwezekano tena wa kuzipata, maana nguvu zake hawaziwezi.
Shetani anamwambia uliapa kwamba utalizilinda, kwamba huyu uliyemtoa kafara hataweza kukuzidi nguvu,na uliapa hautanipa mwingine maana hakuna aliyekuwa na damu ya utakatifu kama huyu.
Sasa si mali zangu,si sadaka yako ya kafara, vyote vimeondoka, sasa ninauhitaji uhai wako mikononi mwangu,maana uliapa na kusaini HATI YA KIFO.Hivyo huna ujanja tena wa kutoka katika kiapo hiki
Hapa mtu hawezi kuchomoka tena.Hana jinsi tena ya kukwepa. Ndipo hujikuta mtu amekauka hapo hapo pasipo mjadala. Watu wanaapa hivi viapo pasipo kujua madhara yake huko mbeleni.
......................................................................
OMBA NAMI KWA IMANI SALA HII:
Sasa ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu uko ndani ya Yesu na unahitaji kujikomboa kutoka huko,ni vizuri na wewe kwenda na sheria,kanuni na utaratibu wao.
Wao wanafanyia gizani,wewe jiombee au fanyia nuruni.
Na wewe sema Ngozi kwa Ngozi katika kuchukua nyota yangu,mali zangu,utajiri wangu,pesa zangu,cheo changu kwa kubatilisha sadaka ya kafara ya mwili wangu kwa sadaka ya kafara ya mwili wa Yesu uliokufa msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kuchukua nafsi yangu, roho yangu na uhai wangu kudai mali zangu na vitu vyangu vyote vilivyokuwa vimetolewa kama sadaka ya uhai,kubatilisha viapo vyao vya uhai wangu kwa kutumia uhai wa Yesu Kristo uliotolewa kama kafara ya ulimwengu pale msalabani.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi,kudai mali zangu ambazo ni uhai wangu uliomo katika damu yangu uliotolewa sadaka ya uhai wa damu yangu kwa shetani ,nabatilisha viapo vya hao Watu kwa kutumia sadaka ya kafara ya uhai uliomo katika damu ya Yesu.
Hii itakusaidia kuua kila chembe chembe za mawasiliano ambazo shetani alizipandikiza katika damu yako ili aweze kujua baraka zako zinazoingia ndani yako ambazo Mungu amezirejesha kwako.
Sina muda wa kutosha kufafanua sana ila twende na mtiririko huu.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi kwa ajili ya kubatilisha viapo vya nafsi vilivyoapwa juu yangu ili maji yaliyomo mwilini mwangu yatumike kama maji ya uzima kwa ajili ya shetani; sasa ninayabatilisha kwa kafara ya maji ya Yesu yaliyomwagika msalabani ili yanirejeshee uzima wangu maeneo yote.
Endelea kusema, Ngozi kwa Ngozi, wale wote waliodhani kwamba nitakufa siku ya kuzidai mali zangu kwa wao kujiapisha viapo vya nafsi,sasa sitakufa maana BwanaYesu alikishinda kifo kwa kafara ya msalabani,wao ndio watakufa na kuniachia baraka zangu zote.
Bwana Yesu alikishinda kifo kwa ajili yangu au yetu kwa kujitoa kafara pale msalabani, hivyo hamna mamlaka yoyote kuendelea kutushikilia katika viapo vya kafara za nafsi na roho kwa ajili ya mali na utajiri.
Ngozi kwa Ngozi: Viapo vyote vilivyoapwa kwa ajili yangu au yetu juu ya kuibiwa baraka za ku-renew au kurejesha mikataba ya kila mwisho wa mwaka ,sasa visiapwe tena kwasababu baraka zangu zinalindwa ndani ya kiapo cha damu ya Yesu iliyotolewa kafara pale msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kwa wale wote walioapa viapo vya nafsi ili miungu izuilie baraka zetu zisiturudie, sasa miungu yote haina nguvu tena ,kwasababu kimiminika cha damu ya Yesu mara 12 iliyomwagika msalabani ninakimimina juu ya miungu 12 na miungu yote inayozuia baraka zetu iungue hadi iachie baraka zetu zote na ziturudie.
Ngozi kwa Ngozi, vile viapo vyote vilivyofanywa na wazazi ,ndugu ,jamaa na marafiki juu yetu wakaapa kwamba hata kama watakufa ,basi viapo vyao vife katika uhai wa kuendelea kutumika.
Ya kwamba hata siku moja tusikae tukazirejesha baraka zetu kama jinsi ile miili iliyofanya viapo hivyo haiwezi kurejewa na uhai tena.Ngozi kwa Ngozi kama ambavyo Yesu alirejewa na uhai katika mwili wake ,na sisi tunazirejesha baraka zetu ambazo ziko katika miili yote ambayo ni marehemu iliyokufa katika viapo vya nafsi na roho zao.
Ngozi kwa Ngozi. Vile viapo mlivyoviapa kwamba mwezi huu wa 12 hatutauvuka na kuuona mwaka mpya, tayari tumeshavuka kwa kafara ya matone 12 ya damu ya Yesu aliyekafarishwa pale msalabani.Amen.
.............................................................
Mpenzi msomaji mtoto wa Mungu hapo lazima uwe katika roho uombe haya maombi kwa imani ili uweze kutoka katika vifungo hivi vya nguvu za giza na makafara yaliyofanyika juu yako.
Ninawatahadharisha haya maombi siyo ya kitoto wala masihara yeyote aliyekuwa amememfanyia ndugu yake maagano ya namna hii, maombi haya ni upanga wa Mungu, sijui utakataje lakini habari mtaipata.
Kipindi hiki siyo cha mzaha na mimi huduma yangu ni ya kuvunja madhabahu na maagano, kwahiyo sina maombi ya rehema kwa waovu, upanga kwa upanga na jino kwa jino.
Naachiliaa moto wa Yesu kwa kila mchawi na mganga wa kienyeji na yeyote aliye na mpango wa kunitumia roho za mauti zimrudie yeye na wote waliojipanga kuwa kinyume nami.
Nawazingira wote wanisomao kwa nia ya kupata maarifa kutoka kwa Mungu uliye juu uwakinge na roho za visasi kutoka katika madhabahu za miungu yao ambazo kuanzia sasa wanaanza kuzipiga na kuzivunja katika Jina la Yesu Kristo aliye hai.
Mtoto wa Mungu ikiwa una sadaka itoe kwa imani na Mungu atakujibu katika maombi yako. Sindikiza maombi yako kwa njia ya kutoa sadaka.
Ahsante Bwana Yesu kwa ajili ya hizi roho ambazo nimezikomboa kwa mamlaka ya Jina lako,nazikukabidhi uzitunze na kuzilinda isipotee hata roho moja mpaka siku ile unarudi uikute iko kundini na uweze kuinyakua na kwenda nayo juu mbinguni kwa Baba,Amen.
MUNGU AWABARIKI SANA WATOTO WA MUNGU.
Haloooo hii ni kiboko ubarikiwe sana mtumishi wa mungu na akuongezee upako na rehema kwa masomo mazito mazito kam hayaAGANO LA KISHETANI LA UTAJIRI,MALI,CHEO,MVUTO(MAFANIKIO) KATIKA MAUTI ZA NAFSI NA ROHO ZA HAO WAUTAFUTAO UTAJIRI:
17.12.2023.
Bwana Yesu apewe sifa sana.Nimerudi tena kwenu kuwapasha habari za ufalme wa Mungu na siri za kuzimu ili mpate kuzijua na kuzishinda hila za shetani.
Ujumbe huu unakuja kwenu hasa watumishi wa Mungu aliye hai ili mpate mbinu au kama mnazo hizi basi mziboreshe kupitia hiki nitakachokisema hapa.
Siyo kwamba mimi ni msemaji wenu,siyo kwamba mimi ninajua kuliko nyinyi,au siyo kwamba mimi ninafundishwa peke yangu,la hasha! Msinifikirie vibaya,mimi ninasema kitu nilichoambiwa nikiseme.
Kwako kinaweza kisiwe na manufaa, ila kwa wengine ni msaada mkubwa sana,hivi kwanini mtumishi wa Mungu huduma yako haikui, kwanini watu wakucheke kwamba huduma yako ni ya kimasikini?
Yaani wachawi wachezee kwenye madhabahu yako na kuinajisi halafu wewe uhubiri watu wasipone ,bado uyakatae haya maarifa.?
Baada ya masomo haya ninakuomba mtumishi wa Mungu tusaidiane kuzivunja hizi madhabahu za miungu,wachawi,waganga wa kienyeji na washirikina wote wapate kubarikiwa na moto wa Mungu.
Yaani tuwabariki kwa moto,tuwabariki kwa upanga wa Mungu, tuwabarikie kwa damu ya Yesu viwachome hadi wateketee mpaka wafuasi wao waseme huu ni ubarikio wa namna gani.
Naam! Nasi tutawaambia huu ni ubarikio wa moto wa Mungu, damu ya Yesu,Jina la Yesu na upanga wa Mungu kuanzia 2024 mpaka Yesu anarudi kutunyakua.
Mizaha sasa imetosha juu ya kanisa la BWANA na kwa watu wa Mungu. Mtumishi wa Mungu bila kuwa na hasira ya kimungu huwezi kutoka kwenye hayo maagano yanayokukwamisha wala hautaweza kutoboza.
Omba kama kichaa, omba kama mwendawazimu, usiweke silaha chini mpaka uone maadui zako wamesalimu amri,huwezi kuvikwa taji kama hujapata ushindi. Ushindi wa kwanza ni hapa hapa duniani. Usimchekee shetani,usimuonee aibu shetani atakuiabisha ukweni kwako.
Ukali wenu nitauona kwenye matokeo ya shuhuda zenu.Mimi nimevipiga vita sana nikiwa nyikani, ninajua hiki ninachokiongea, hakuna miungu wala shetani itakayoweza kusimama mbele yangu na ikashinda, Kwasababu Yesu aliye ndani yangu ni mkuu kuliko wote,lazima nimtukuze mahali popote pale atakaponituma, ila ninaanzia hapa nyumbani kwanza.
MUNGU AWABARIKI SANA:
Mwili wa mwanadamu usiokuwa na uhai huitwa maiti. Ni maiti kwasababu umekutwa na umauti.
Umauti ni roho ya kifo ambayo humvaa mtu na kuondoka na uhai wake.Uhai huu ukiondolewa ndani ya nafsi ya mtu ndipo mtu huwa mfu, nafsi isiyokuwa na uhai wala utambuzi wa aina yotote ile.
Mwili hupelekwa na kuhifadhiwa katika nyumba yake ya milele iitwayo Kaburi.Na hapa ndipo neno la BWANA linapotimizwa kwamba umeumbwa kwa udongo, utarudi tena udongoni.
Hakuna mwanadamu awezaye kukishinda kifo isipokuwa Yesu peke yake na wale waliopata neema mbele za macho ya BWANA.
Hawa ni wale walioandikiwa haki mbele za kiti cha enzi cha Mungu Baba.
Hata shetani na mbinu zake zote hawezi kukishinda wala kukiepuka;kwasababu tangu kipindi kile alivyoasi, alishahukumiwa adhabu ya kifo katika lile ziwa likawalo moto.
Watenda dhambi wote hukumu yao ilishatoka, ambayo ni kifo cha umauti wa milele pamoja na shetani.Labda wale watakaopata neema ya kuisikia Injili ya Yesu,hao ndio watakaourithi Uzima wa Milele.
Waliokufa katika dhambi,wote ni mauti ya milele maana watatupwa katika lile ziwa liwakalo moto usiku na mchana pasipo kuzimika.
Pamoja na kwamba mtu anakufa mwili wake na roho yake kwenda sehemu nyingine.Lakini kuna watu wengine wanaandikiwa VIFO WAKINGALI HAI,WANATEMBEA HUKU ROHO WA UMAUTI AKIWA JUU YAO.
Hapa kinachosubiriwa ni muda ,saa na sababu itakayomsababishia umauti. Vifo vya namna hii haviji pasipo sababu maalumu.
Inaweza kuwa ni sababu ya uchawi, visasi, chuki,wivu,maagano ya kichawi yaliyofanywa huko nyuma na wazazi au mababu za hao watu.n.k.
Wengine ni laana inayotoka ndani ya ukoo wa huyo mtu.Huyu roho akishamvaa mtu hujikuta anaanza kujichukia, kukata tamaa na kukosa matumaini, hukosa raha na uchangamfu, hupenda kujitenga na watu,pia ni mtu wa kuwa na wasiwasi wakati wote.
Akimtazama mtu usoni huwa na aibu aibu huku akiangalia chini,huyu ni roho anakuwa anajua unamuona ila ni ngumu kung'amua katika mwilini, uso wa huyu mtu hukosa nuru na kuwa na mpauko usoni kama rangi ya maiti.
Huwezi kumshinda roho wa mauti isipokuwa kwa njia ya nguvu ya MSALABA WA BWANA YESU.
Yesu alivyosema pale msalabani "IMEKWISHA",Alikuwa anaitoa roho yake ili kwenda kuzimu alipo shetani kumnyang'anya funguo za uzima na mauti na kuisimamisha juu ya watu wake wote dunia nzima.
Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya watu wote, watu wasidanganye eti alikufa kwa ajili ya Wakristo tu,siyo kweli yeyote anayeliamini Jina lake ni wake Yeye Kristo.
Pale ilikwisha nguvu,ilikosa uhalali wa kutuua kwasababu hati zote za mashtaka zilipigiliwa pale msalabani. Tulipewa uzima wa Milele mara tu baada ya kufufuka na kwenda(kupaa) juu mbinguni kwa Baba yetu.
Wanadamu wanapotea na kufa vifo ambavyo siyo vyao wala vifo vya haki kwasababu hawana maarifa ya Mungu, na kwa kuwa wamemkataa Yesu na kuamua kumfuata shetani.
Shetani amewadanganya na kuwapotosha macho yao ili wasipate kuona na kuijua kweli,neema na thamani ya nguvu ya msalaba iletayo ukombozi ndani ya mtu,badala yake wameyakumbatia mafundisho manyonge na madhaifu kwa kujipa matumaini kwamba mtu akifa ataombewa na kupata msamaha wa ondoleo la dhambi.
Wanasahau kwamba imeandikwa "bora wafu wafao katika BWANA maana hao watafufuliwa siku ya mwisho".
Maana yake ni watu waliokufa katika Kristo Yesu.
Hakuna siku ya mwisho nyingine, bali ni sasa,hizi ndizo nyakati za mwisho ambazo Bwana Yesu yuaja upesi kuja kulinyakua kanisa lake,ambapo kabla ya ujio wake atawaandaa watakatifu wake ili wapate kumpokea mawinguni.
Hata wale wafu waliokufa katika BWANA ambao maandiko yanawataja, watafufuliwa kwanza ili waungane na walio hai,waliolikiri Jina Langu.Hawa ni wateule Wangu na watakatifu WANGU, niliopendezwa nao.(JESUS SPEAKS HIMSELF THROUGH ME).
Wale waliolikataa Jina langu ,na wale walio vuguvugu;wale waniitao BWANA,BWANA.Lakini hapo hapo wanajihudhurisha kwa miungu ,hao sina haja nao.(Yesu anaongea saa hii).
Nitawakataa, nitawatema, hawataingia RAHANI Mwangu,maana hawa ni wafu wanaoishi. Hawajafa katika BWANA wala hawaishi katika maisha matakatifu. (Roho yake imeongea ndani yangu,kuweni makini watu wa Mungu).
Kumbuka Andiko "waache wafu wazikane. ".Hawa ni wafu maana hawana walijualo, linaloendelea katika UFALME WA MUNGU.
Hawajui saa wala dalili za kuja kwa Mwana wa Adamu.Akili zao na fahamu zao haziwazi yaliyo ya Mungu, bali hujitaabisha na mambo ya dunia na kujihudhurisha kwa shetani.
WANAZIKANA KWA NAMNA GANI?
Roho wa umauti anawasubiria ili aweze kuwavaa na kuwachukua maana hawana kinga wala zuio au kizuizi chochote. Yeye asiye na Yesu ana roho wa umauti anatembea naye,anasubiri apate chanzo na sababu ili amvae na kuondoka naye.
Kuna wengine wameandikiwa umauti au kifo na wazazi wao,ndugu zao, Rafiki zao,na jamaa zao KAMA KAFARA LA UTAJIRI NA MALI.
Shetani hupenda kujifananisha na Mungu. Jinsi Yesu alivyotolewa kafara kama ondoleo la dhambi ya Ulimwengu, ndivyo hivyo hivyo shetani apendavyo kupewa kafara ya damu ya mtu.
Kafara ya damu ya mtu ina thamani kubwa kuliko damu ya mnyama,Kwasababu ina uhusiano na damu ya Yesu.Damu ya Yesu ina uungu mkuu sana,hivyo wote walio na Yesu wana damu kama Yake.
Mtu wa Mungu nisome kwa umakini sana hapa.
Maandiko yanasema,Yesu alisema yeyote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni,huyu ndiye ndugu yangu,na umbu langu,na mama yangu.Umbu kwa lugha nyingine ni dada.
Kwahiyo watu hawaitwi ndugu pasipo kuwa na vinasaba vya damu.
Unadhani kwanini sisi Watanzania huwa tunaitana kaka na dada? Maana tunachukuliana kama ndg wamoja. Kiroho sisi ni ndg sana,ndio maana utasikia ndg yetu,zetu Watanzania wamepatwa na shida fulani tuwasaidie.
Sasa twende kwa Yesu kwa mtiririko wa hapo juu.
Tumerithi ufalme wa Mungu kupitia imani ya baba yetu Ibrahimu,Yesu ni ukoo wa Yuda mtoto wa Yakobo,Yakobo ni mjukuu wa Ibrahimu.
Yesu anatokea katika shina la Daudi ,ambalo ni ukoo wa Yuda. Hivyo basi Yesu alikuwa na damu ya kibinadamu kamili kwasababu pia alizaliwa na mwanamke kama vile ambavyo watoto wote huzaliwa na mwanamke.
Kwahiyo kitendo cha Yesu kusema sisi tulio wake ni ndugu zake,maana yake katika imani tunakuwa katika ukoo mmoja na Baba yake ndiye Baba yetu pia. Glory to God, hallelujah!!!
Kwahiyo katika ulimwengu wa roho kinaumbika kitu kipya.Maana hata maandiko yanasema sisi tumefanyika viumbe vipya ndani ya Yesu.Tumebadilishwa kutoka ule utu wa kale na kuwa mpya ndani ya Kristo Yesu.
Tunafanyika kuwa watoto wa Mungu kwasababu tumebadilishwa na kuwa na sifa kama za Mungu wetu aliyetuumba. Kwahiyo kila kitu chetu ni kipya.
Damu yetu ni mpya kwasababu imetakaswa upya, imechujwa na kuwa safi na damu halisi.
Kwahiyo hii damu ndio ambayo shetani anaiwinda usiku na mchana ili aweze kuipata na kuichukua. Hii ina nguvu kuliko damu ya viumbe vyote.
Wanyama hawana damu safi,salama,na yenye thamani kama damu ya mtu;mtu aliyeokoka. Hii damu akiinywa shetani inampa nguvu na mafunuo kujua kitu gani kinaendelea katika ulimwengu wa roho wa NURUNI.
Yesu alisema Yeye ni nuru ya Ulimwengu.Kwahiyo katika vinasaba vya damu yake zipo chembe chembe ambazo zimebeba maono na mafunuo yenye taarifa sahihi za siri za mbingu.
Kwa kuwa Yesu anao ndugu zake ambao ni watoto wake,ambao ni watoto wa Mungu, basi hujikuta damu Yake iko sawa sawa na ndugu zake hawa,watu waliomkiri au waliokiri Jina Lake.
Lasivyo asingesema, sisi ni ndugu zake.Na ndugu zake wote ni wana wa Mungu walio ndani ya Yesu.Yesu ni ukoo wa watoto wote waliozaliwa mara ya pili kwa ajili ya Mungu.
Kwahiyo Yesu anawakilisha ukoo wa Mungu kwa watoto wa Mungu, akiwa Yeye ndiye mzaliwa wa kwanza. Ndio maana shetani anapenda kuwashikilia watoto wote waliozaliwa wakiwa wa kwanza,Kwasababu ni malango.
Ni malango kwasababu ni kielelezo cha Yesu Kristo. Kama alivyo Lango la baraka,uzima wa milele na mrithi wa viti vyote vya Enzi vya baba yetu.
Mtoto wa kwanza akiwa ni lango la laana,basi watoto wote watakaofuata watapata laana na mikosi.Labda tu kwa neema ya msalaba na damu iliyomwagika msalabani ipate kuwakomboa na kuwaweka huru.
Mtoto wa kwanza akiwa ni baraka ,halafu yuko upande wa Mungu ;Yaani yuko ndani ya Yesu.Shetani hupenda damu yake maana anajua atapata taarifa zote zilizomo kwake na kujua mpango wa Mungu ili aweze kumuibia na kisha kumakwamisha.
Kuna watoto wanaozaliwa na Nuru ya ulimwengu. Hawa tangu wakiwa tumboni mwa mama zao tayari Mungu alishawapaka mafuta.
Maandiko yanasema kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa;nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Angalia hapa Kumbe Mungu anawajua watoto wake. Shetani naye akishawajua anaanza utaratibu wa kuwashika. Hawezi kuwashika Wala kuwamiliki pasipokuwa na ridhaa ya wazazi,ndugu au jamaa zake.
Atakachokifanya ni kumshawishi mzazi kupitia kwa wachawi,waganga wa kienyeji, wazee wa mila na waaguzi waonao kwa kutumia mapepo ya utambuzi.
Kwamba wamtoe huyo mtoto madhabahuni kwao;kisha yeye watampatia nyota ya utajiri.
Hata kama ni cheo, au mafanikio mengine, lakini mafanikio yoyote huleta mali na vitu zikiwemo fedha. Hivi vitu vyote au wingi wa vitu mbalimbali, au wingi wa mali ni UTAJIRI.
Kwasababu ya tamaa ya mwanadamu ya kupenda pesa na utajiri hujikuta anamtoa au anawatoa watoto wake ili wawe kafara ya ngekewa yake.
Wapendwao kutolewa kafara huwa ni mabinti. Kwasababu hawa huwa ni rahisi kutoa damu zao kama sadaka kwa njia nyingi tofauti na watoto wa kiume ambao wao damu zao ni mpaka wapate ajali na vifo vyao.
Hawa watoto wa kike damu zao huanza kutoka pale wanapovunja ungo, damu ya ubikra, damu ya hedhi ya kila mwezi, damu ya wakati wa kujifungua, ajali n.k.
Kwahiyo wao wana damu nyingi na njia nyingi ya kutoa damu tofauti na wenzao wa kiume. Shetani anawapenda hawa wa kike kwa kuwa maungo yao ni rahisi kuwaingilia kwa kutumia tendo la ngono.
TENDO LA NGONO ni Agano rahisi kwa kuwa anakuwa anaziunganisha NAFSI za hawa watoto wa kike na mapepo yake,au waume wa kipepo.
Kwahiyo shetani anavyojua hawa watoto wana damu yenye uhusiano na Yesu ndipo hupenda kutumia Agano lenye nguvu na gumu kufunguka ambalo ni Agano la UMAUTI.
Hapa anamuapisha mzazi kwamba aseme binti yake/zake amewatoa moja kwa moja kwa mfalme mungu mkuu wa dunia (shetani) ili awe mume wao milele na milele na asikae akakiuka ndoa hii halali.
Wanaambatanisha kwamba kilichofungwa na Mungu mwanadamu asikifungue/asikitenganishe. (Wanaomba kinyume).
Akitaka kuivunja madhara yampate ikiwemo KIFO, kama jinsi mkataba ulivyoandikwa na cheti cha ndoa kilivyoandikwa ya kwamba binti yangu/zangu fulani na fulani nimewaozesha kwa mungu mkuu ambaye mume wenu atakuwa mume aitwaye PEPO MAUTI AU JINI MAITI.
Kwa kujua thamani ya maji yaliyomwagika msalabani. Wanatumia maji waliyooshea maiti, tena maiti iliyooza,kisha wanamnyesha huyu mtoto au watoto kwamba hii ni nadhiri na yamini kwamba sasa maji haya ya maiti yanakuunganisha na mume wako/wenu pepo maiti.
Hawataishia hapo tu,bali watamuosha au kuwaosha hawa watoto kwa kutumia hayo hayo maji waliyooshea maiti ili wamtakase katika ulimwengu wa giza kwa ajili ya kuolewa na huyo jini maiti.
Mambo yote haya yanafanyika kwa ajili ya kuua utu wa ndani,kuharibu nguvu za asili za ile damu ya Yesu ili anavyozidi kukua na kuongezeka na kupata maarifa asije akawasumbua.
Hapa ndipo KARAMA,VIPAWA,NDOTO NA NYOTA za watoto wa Mungu huanza kupotea, huandamwa na mikosi,nuksi kwa kila anachokifanya huwa hakifanikiwi.
Kwasababu yale maji yaliyooshea maiti iliyooza ndio hutumika kuleta roho za kuzaa mapooza na kumharibia maisha yake yote.
Mungu naye hayuko mbali huanza kumtafuta huyu mtoto/watoto wake.Hapa vita huibuka. Yeye anamtaka, na shetani hataki kumtoa, anadai alikabidhiwa na mzazi au wazazi wake.
Anatoa vifungu vyote vya mikataba,viapo na maagano waliyokubaliana na wazazi wake.
Mungu anaona isiwe taabu anaanza kumpa maarifa ya kutoka kwenye hivyo vifungo.
Njia rahisi, si nyingine bali damu ya Yesu. Kadri anavyozidi kutumia damu ya Yesu ndivyo yale maagano yaliyofanywa yanavyozidi kutoweka.Kwasababu ile damu ya huyu binti inazidi kuwa na nguvu kuzidi maagano yao yaliyofanyika au ambayo yalikuwa yakifanyika kwa kuchinja mnyama wa kafara.
Shetani anasema nilitumia maji ya maiti iliyooza, kwahiyo huyu atatakasika vipi?
Mungu ana maarifa zaidi ya shetani, Mungu anasema tumia maji yaliyomwagika msalabani kujiosha na kujtakasa.
Hapa ndipo nira huanza kukatika na kulegea hadi kuisha. Na zile nafsi za watu wote waliokuwa wamejiunganisha hapo kwenye hilo agano la utajiri ukatika pia.
Hapa itategemea waliapa viapo gani,kama ni viapo vya vifo, basi nafsi zao hukatika na mauti huwafikia Maana wao hawana damu iliyo safi na takatifu kama ya hawa waliokombolewa.
Kwahiyo huwa ni nafsi zao kupotea, sadaka zao ni damu yao.Shetani hapa hana msamaha;lazima uondoke maana anasema ulizipenda mali zangu kwahiyo huna budi kufa.
Vifo vya namna hii huwa havizuiliki maana huwa ni vya ghafla sana kwasababu vinasababishwa na huyo jini mauti au pepo mauti anayekuwa ni mauti katika mwili ila roho yake inafanya kazi kwa usaidizi wa mapepo mengine.
Turudi nyuma kidogo.
Na wanasema jinsi maiti alivyo wa baridi na mwili wa huyu binti uwe wa baridi,maisha yake yawe ya baridi ,asikae akawa na moto kwa kila akifanyacho.
Shetani hatendi kazi nje ya laana. Ni lazima kwanza aue vitu vya kiroho vilivyomo ndani ya mtu halafu apandikize roho nyingine ambazo ziko kinyume na mpango wa Mungu.
Kazi ya shetani na sifa kuu ya shetani ni kuiba, kuua na uongo.Anadanganya kwa kutenda kinyume na matarajio ya mwanadamu kisha anaua mpango wa Mungu ambao uko juu ya huyo mtu.
Mali za shetani hazidumu,utajiri wa shetani una mwisho wake.Lakini utajiri wa Mungu hauna mwisho wala ukomo;maana Yeye ndiye chanzo cha utajiri na mali.Shetani hana mali ispokuwa azipate kwa kuiba vitu walivyonavyo watoto wa Mungu.
KUNA WATU WANAFANYA VIAPO VYA KAFARA ZA NAFSI NA ROHO ZAO KWA AJILI YA MALI,UTAJIRI,MVUTO NA UMAARUFU.
Mtoto wa Mungu Kumbuka kule juu kichwa cha somo kilisemaje.Hapa ndipo tunakuja kwenye kiini cha somo.Kule nilikuwa ninawapitisha kwenye msingi wa haya maagano.
Wanafanya viapo hivi au vya namna hii kwa kujitoa wao kafara ili kwamba siku ikitokea mtu aliyekuwa ametolewa kafara akafunguka na kuyavunja maagano waliyokubaliana;basi wao ndio watumike kama mbadala wake.
Yaani zile nafsi za roho za watu wengine au ndugu,na jamaa zao walizokuwa wamezitoa kama sadaka za kafara kwa shetani,siku zikikombolewa kwa nguvu ya msalaba wa BWANA YESU basi wao hawana budi kutumikia kile kiapo chao cha awali.
Hapa ndipo watu hawa hujikuta wanadaiwa hizo mali,mvuto,utajiri,UMAARUFU, na cheo,na kwa kuwa walishaapa kwamba wao ndio watakuwa mbadala wake,hawawezi tena kupewa nafasi ya kuwatoa wengine.
Huwa wanaapa kwamba siku mtu huyu/hawa wakifunguka katika Kristo, basi mimi sina budi kuwa kafara kama mbadala wake.
Huwa wanajiaminisha na kuwa na ujasiri wa kufanya hivyo kwa vile wanajua vifungo walivyoviweka juu ya huyo mtu,havitawahi kuondolewa kamwe.
Lakini ashukuriwe Mungu aonaye sirini na kutujulisha mambo ya gizani. Jinsi anavyowapenda watu wake hata akaamua kumtoa mwanaye wa pekee ili awe KAFARA kwa ajili ya watu wake.
Naye si mwingine bali ni Yesu Kristo aliye hai.Yeye alivyokufa msalabani ilikuwa ni kafara ya ukombozi kwa wanadamu wote wa ulimwengu, ambao watahitaji msaada wake.
Hii kafara yake ndio inayoua nguvu za wale watu wote waliowatoa kafara ya viapo vya nafsi na roho ndugu zao au watoto wao au jamaa zao.
Kwa kuwa wao walitolewa kafara ya nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,na mvuto au cheo na umaarufu, hapa pia ukombozi wake unafanyika kwa njia ya Ukombozi wa kuuzwa nafsi yangu/zetu kwa shetani na baba,mama,kaka,mjomba,dada,bib na babu kwa kutumia kafara ya Yesu pale msalabani.
Hii ni lazima iandane na kanuni waliyoitumia kama ni kiapo, kivunjwe kwa kiapo.Kama ni sadaka ivunjwe kwa sadaka ,kama ni kafara ivunjwe kwa kafara katika ulimwengu wa Nuru,maana yote ya kwao yalifanyika katika ulimwengu wa giza.
TUSOME AYUBU 2:4
Shetani akamjibu BWANA,na kusema ,Ngozi kwa Ngozi,naam, yote aliyonayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
Kwahiyo shetani anavyokupa mali anategemea au anakupa kiapo cha kujitoa uhai iwapo kama utashindwa kukitunza kiapo chako na makubaliano yenu.
Ndio maana nikasema ni kiapo cha nafsi na roho kama kafara kwa ajili ya utajiri na mali,viapo vyako vinavyokuwa vikubwa, ndivyo na maagano yako yanavyozidi kuwa makubwa zaidi.
Maagano yako yanavyokuwa makubwa zaidi ndivyo na sadaka zako za kafara zinavyozidi kuwa nyingi na kubwa zaidi. Mtu haapi kwa shetani pasipo hakikisho la jambo analotaka kulifanya. Lazima kuwepo na kusudi au lengo.
Watu hawaendi kwenye ibada au maombi pasipo kusudi ndani ya mioyo yao;lazima wawe na dhamira iliyo ndani ya mioyo yao ambayo inawapelekea kwenda ibadani na kutaka maombi.
Dhamira hiyo ndio kusudi.Sasa tunaposema mtu anajitoa nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,mvuto,umaarufu, cheo au hata uchawi na uganga mkuu, ndio huo uhai anausema AYUBU.
KWANINI NI UHAI KWA AJILI YA UTAJIRI?
Kwasababu,nafsi inatunza roho,na roho ndio uhai wenyewe.Na mahali nafsi ya mtu ilipo ndipo mali yake ipo hapo.
Kwahiyo hawa watu wanatunza viapo vyao vya mali kwa kuzitoa au kuziweka nafsi na roho zao rehani ili mali zao zisiweze kupotea. Ili pia mtu waliyemuibia asiweze kuzidai.
Na ikitokea akaanza kuzidai basi umauti umkute;maana yeye alitolewa kama kafara kwa ajili ya mali za yule aliyeapa viapo vya nafsi na roho kwa ajili ya mali.
Ikitokea huyu aliyetolewa akawazidi nguvu na kuzichukua mali zake; ndipo ule usemi wa shetani unajidhihirisha,kwamba Ngozi kwa Ngozi na yote uliyonayo utayatoa kwa ajili ya uhai wako.
Lazima ajitoe yeye uhai wake,kwasababu hana mali tena,hana mtu tena wa kumtoa kafara maana si kila mtu unaweza kumtoa kafara, wengine damu zao ni chafu shetani hazihitaji.
Kwahiyo hapa inabidi wewe ndiye ufe kama mbadala wake.Tena mbaya zaidi yule aliyezikomboa yuko ndani ya Kristo;wanakuwa wanaona hakuna uwezekano tena wa kuzipata, maana nguvu zake hawaziwezi.
Shetani anamwambia uliapa kwamba utalizilinda, kwamba huyu uliyemtoa kafara hataweza kukuzidi nguvu,na uliapa hautanipa mwingine maana hakuna aliyekuwa na damu ya utakatifu kama huyu.
Sasa si mali zangu,si sadaka yako ya kafara, vyote vimeondoka, sasa ninauhitaji uhai wako mikononi mwangu,maana uliapa na kusaini HATI YA KIFO.Hivyo huna ujanja tena wa kutoka katika kiapo hiki
Hapa mtu hawezi kuchomoka tena.Hana jinsi tena ya kukwepa. Ndipo hujikuta mtu amekauka hapo hapo pasipo mjadala. Watu wanaapa hivi viapo pasipo kujua madhara yake huko mbeleni.
......................................................................
OMBA NAMI KWA IMANI SALA HII:
Sasa ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu uko ndani ya Yesu na unahitaji kujikomboa kutoka huko,ni vizuri na wewe kwenda na sheria,kanuni na utaratibu wao.
Wao wanafanyia gizani,wewe jiombee au fanyia nuruni.
Na wewe sema Ngozi kwa Ngozi katika kuchukua nyota yangu,mali zangu,utajiri wangu,pesa zangu,cheo changu kwa kubatilisha sadaka ya kafara ya mwili wangu kwa sadaka ya kafara ya mwili wa Yesu uliokufa msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kuchukua nafsi yangu, roho yangu na uhai wangu kudai mali zangu na vitu vyangu vyote vilivyokuwa vimetolewa kama sadaka ya uhai,kubatilisha viapo vyao vya uhai wangu kwa kutumia uhai wa Yesu Kristo uliotolewa kama kafara ya ulimwengu pale msalabani.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi,kudai mali zangu ambazo ni uhai wangu uliomo katika damu yangu uliotolewa sadaka ya uhai wa damu yangu kwa shetani ,nabatilisha viapo vya hao Watu kwa kutumia sadaka ya kafara ya uhai uliomo katika damu ya Yesu.
Hii itakusaidia kuua kila chembe chembe za mawasiliano ambazo shetani alizipandikiza katika damu yako ili aweze kujua baraka zako zinazoingia ndani yako ambazo Mungu amezirejesha kwako.
Sina muda wa kutosha kufafanua sana ila twende na mtiririko huu.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi kwa ajili ya kubatilisha viapo vya nafsi vilivyoapwa juu yangu ili maji yaliyomo mwilini mwangu yatumike kama maji ya uzima kwa ajili ya shetani; sasa ninayabatilisha kwa kafara ya maji ya Yesu yaliyomwagika msalabani ili yanirejeshee uzima wangu maeneo yote.
Endelea kusema, Ngozi kwa Ngozi, wale wote waliodhani kwamba nitakufa siku ya kuzidai mali zangu kwa wao kujiapisha viapo vya nafsi,sasa sitakufa maana BwanaYesu alikishinda kifo kwa kafara ya msalabani,wao ndio watakufa na kuniachia baraka zangu zote.
Bwana Yesu alikishinda kifo kwa ajili yangu au yetu kwa kujitoa kafara pale msalabani, hivyo hamna mamlaka yoyote kuendelea kutushikilia katika viapo vya kafara za nafsi na roho kwa ajili ya mali na utajiri.
Ngozi kwa Ngozi: Viapo vyote vilivyoapwa kwa ajili yangu au yetu juu ya kuibiwa baraka za ku-renew au kurejesha mikataba ya kila mwisho wa mwaka ,sasa visiapwe tena kwasababu baraka zangu zinalindwa ndani ya kiapo cha damu ya Yesu iliyotolewa kafara pale msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kwa wale wote walioapa viapo vya nafsi ili miungu izuilie baraka zetu zisiturudie, sasa miungu yote haina nguvu tena ,kwasababu kimiminika cha damu ya Yesu mara 12 iliyomwagika msalabani ninakimimina juu ya miungu 12 na miungu yote inayozuia baraka zetu iungue hadi iachie baraka zetu zote na ziturudie.
Ngozi kwa Ngozi, vile viapo vyote vilivyofanywa na wazazi ,ndugu ,jamaa na marafiki juu yetu wakaapa kwamba hata kama watakufa ,basi viapo vyao vife katika uhai wa kuendelea kutumika.
Ya kwamba hata siku moja tusikae tukazirejesha baraka zetu kama jinsi ile miili iliyofanya viapo hivyo haiwezi kurejewa na uhai tena.Ngozi kwa Ngozi kama ambavyo Yesu alirejewa na uhai katika mwili wake ,na sisi tunazirejesha baraka zetu ambazo ziko katika miili yote ambayo ni marehemu iliyokufa katika viapo vya nafsi na roho zao.
Ngozi kwa Ngozi. Vile viapo mlivyoviapa kwamba mwezi huu wa 12 hatutauvuka na kuuona mwaka mpya, tayari tumeshavuka kwa kafara ya matone 12 ya damu ya Yesu aliyekafarishwa pale msalabani.Amen.
.............................................................
Mpenzi msomaji mtoto wa Mungu hapo lazima uwe katika roho uombe haya maombi kwa imani ili uweze kutoka katika vifungo hivi vya nguvu za giza na makafara yaliyofanyika juu yako.
Ninawatahadharisha haya maombi siyo ya kitoto wala masihara yeyote aliyekuwa amememfanyia ndugu yake maagano ya namna hii, maombi haya ni upanga wa Mungu, sijui utakataje lakini habari mtaipata.
Kipindi hiki siyo cha mzaha na mimi huduma yangu ni ya kuvunja madhabahu na maagano, kwahiyo sina maombi ya rehema kwa waovu, upanga kwa upanga na jino kwa jino.
Naachiliaa moto wa Yesu kwa kila mchawi na mganga wa kienyeji na yeyote aliye na mpango wa kunitumia roho za mauti zimrudie yeye na wote waliojipanga kuwa kinyume nami.
Nawazingira wote wanisomao kwa nia ya kupata maarifa kutoka kwa Mungu uliye juu uwakinge na roho za visasi kutoka katika madhabahu za miungu yao ambazo kuanzia sasa wanaanza kuzipiga na kuzivunja katika Jina la Yesu Kristo aliye hai.
Mtoto wa Mungu ikiwa una sadaka itoe kwa imani na Mungu atakujibu katika maombi yako. Sindikiza maombi yako kwa njia ya kutoa sadaka.
Ahsante Bwana Yesu kwa ajili ya hizi roho ambazo nimezikomboa kwa mamlaka ya Jina lako,nazikukabidhi uzitunze na kuzilinda isipotee hata roho moja mpaka siku ile unarudi uikute iko kundini na uweze kuinyakua na kwenda nayo juu mbinguni kwa Baba,Amen.
MUNGU AWABARIKI SANA WATOTO WA MUNGU.
Amen! Ahsante sana,ubarikiwe sana na wewe pia kwa jinsi unavyofuatilia masomo haya pasipo kukoma. Na watu wote mnaotufuatilia hapa Jamvini katika madhabahu hii Mungu awabariki sana na kuwatendea kadri ya mahitaji yenu myaombayo katika njia ya haki.Haloooo hii ni kiboko ubarikiwe sana mtumishi wa mungu na akuongezee upako na rehema kwa masomo mazito mazito kam haya![]()
Ubarikiwe sana mtumishi imenipasa kurudia somo hili na la mke hapo juu ili kufungua zaidi ubongo na kuelewa zaidi...AGANO LA KISHETANI LA UTAJIRI,MALI,CHEO,MVUTO(MAFANIKIO) KATIKA MAUTI ZA NAFSI NA ROHO ZA HAO WAUTAFUTAO UTAJIRI:
17.12.2023.
Bwana Yesu apewe sifa sana.Nimerudi tena kwenu kuwapasha habari za ufalme wa Mungu na siri za kuzimu ili mpate kuzijua na kuzishinda hila za shetani.
Ujumbe huu unakuja kwenu hasa watumishi wa Mungu aliye hai ili mpate mbinu au kama mnazo hizi basi mziboreshe kupitia hiki nitakachokisema hapa.
Siyo kwamba mimi ni msemaji wenu,siyo kwamba mimi ninajua kuliko nyinyi,au siyo kwamba mimi ninafundishwa peke yangu,la hasha! Msinifikirie vibaya,mimi ninasema kitu nilichoambiwa nikiseme.
Kwako kinaweza kisiwe na manufaa, ila kwa wengine ni msaada mkubwa sana,hivi kwanini mtumishi wa Mungu huduma yako haikui, kwanini watu wakucheke kwamba huduma yako ni ya kimasikini?
Yaani wachawi wachezee kwenye madhabahu yako na kuinajisi halafu wewe uhubiri watu wasipone ,bado uyakatae haya maarifa.?
Baada ya masomo haya ninakuomba mtumishi wa Mungu tusaidiane kuzivunja hizi madhabahu za miungu,wachawi,waganga wa kienyeji na washirikina wote wapate kubarikiwa na moto wa Mungu.
Yaani tuwabariki kwa moto,tuwabariki kwa upanga wa Mungu, tuwabarikie kwa damu ya Yesu viwachome hadi wateketee mpaka wafuasi wao waseme huu ni ubarikio wa namna gani.
Naam! Nasi tutawaambia huu ni ubarikio wa moto wa Mungu, damu ya Yesu,Jina la Yesu na upanga wa Mungu kuanzia 2024 mpaka Yesu anarudi kutunyakua.
Mizaha sasa imetosha juu ya kanisa la BWANA na kwa watu wa Mungu. Mtumishi wa Mungu bila kuwa na hasira ya kimungu huwezi kutoka kwenye hayo maagano yanayokukwamisha wala hautaweza kutoboza.
Omba kama kichaa, omba kama mwendawazimu, usiweke silaha chini mpaka uone maadui zako wamesalimu amri,huwezi kuvikwa taji kama hujapata ushindi. Ushindi wa kwanza ni hapa hapa duniani. Usimchekee shetani,usimuonee aibu shetani atakuiabisha ukweni kwako.
Ukali wenu nitauona kwenye matokeo ya shuhuda zenu.Mimi nimevipiga vita sana nikiwa nyikani, ninajua hiki ninachokiongea, hakuna miungu wala shetani itakayoweza kusimama mbele yangu na ikashinda, Kwasababu Yesu aliye ndani yangu ni mkuu kuliko wote,lazima nimtukuze mahali popote pale atakaponituma, ila ninaanzia hapa nyumbani kwanza.
MUNGU AWABARIKI SANA:
Mwili wa mwanadamu usiokuwa na uhai huitwa maiti. Ni maiti kwasababu umekutwa na umauti.
Umauti ni roho ya kifo ambayo humvaa mtu na kuondoka na uhai wake.Uhai huu ukiondolewa ndani ya nafsi ya mtu ndipo mtu huwa mfu, nafsi isiyokuwa na uhai wala utambuzi wa aina yotote ile.
Mwili hupelekwa na kuhifadhiwa katika nyumba yake ya milele iitwayo Kaburi.Na hapa ndipo neno la BWANA linapotimizwa kwamba umeumbwa kwa udongo, utarudi tena udongoni.
Hakuna mwanadamu awezaye kukishinda kifo isipokuwa Yesu peke yake na wale waliopata neema mbele za macho ya BWANA.
Hawa ni wale walioandikiwa haki mbele za kiti cha enzi cha Mungu Baba.
Hata shetani na mbinu zake zote hawezi kukishinda wala kukiepuka;kwasababu tangu kipindi kile alivyoasi, alishahukumiwa adhabu ya kifo katika lile ziwa likawalo moto.
Watenda dhambi wote hukumu yao ilishatoka, ambayo ni kifo cha umauti wa milele pamoja na shetani.Labda wale watakaopata neema ya kuisikia Injili ya Yesu,hao ndio watakaourithi Uzima wa Milele.
Waliokufa katika dhambi,wote ni mauti ya milele maana watatupwa katika lile ziwa liwakalo moto usiku na mchana pasipo kuzimika.
Pamoja na kwamba mtu anakufa mwili wake na roho yake kwenda sehemu nyingine.Lakini kuna watu wengine wanaandikiwa VIFO WAKINGALI HAI,WANATEMBEA HUKU ROHO WA UMAUTI AKIWA JUU YAO.
Hapa kinachosubiriwa ni muda ,saa na sababu itakayomsababishia umauti. Vifo vya namna hii haviji pasipo sababu maalumu.
Inaweza kuwa ni sababu ya uchawi, visasi, chuki,wivu,maagano ya kichawi yaliyofanywa huko nyuma na wazazi au mababu za hao watu.n.k.
Wengine ni laana inayotoka ndani ya ukoo wa huyo mtu.Huyu roho akishamvaa mtu hujikuta anaanza kujichukia, kukata tamaa na kukosa matumaini, hukosa raha na uchangamfu, hupenda kujitenga na watu,pia ni mtu wa kuwa na wasiwasi wakati wote.
Akimtazama mtu usoni huwa na aibu aibu huku akiangalia chini,huyu ni roho anakuwa anajua unamuona ila ni ngumu kung'amua katika mwilini, uso wa huyu mtu hukosa nuru na kuwa na mpauko usoni kama rangi ya maiti.
Huwezi kumshinda roho wa mauti isipokuwa kwa njia ya nguvu ya MSALABA WA BWANA YESU.
Yesu alivyosema pale msalabani "IMEKWISHA",Alikuwa anaitoa roho yake ili kwenda kuzimu alipo shetani kumnyang'anya funguo za uzima na mauti na kuisimamisha juu ya watu wake wote dunia nzima.
Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya watu wote, watu wasidanganye eti alikufa kwa ajili ya Wakristo tu,siyo kweli yeyote anayeliamini Jina lake ni wake Yeye Kristo.
Pale ilikwisha nguvu,ilikosa uhalali wa kutuua kwasababu hati zote za mashtaka zilipigiliwa pale msalabani. Tulipewa uzima wa Milele mara tu baada ya kufufuka na kwenda(kupaa) juu mbinguni kwa Baba yetu.
Wanadamu wanapotea na kufa vifo ambavyo siyo vyao wala vifo vya haki kwasababu hawana maarifa ya Mungu, na kwa kuwa wamemkataa Yesu na kuamua kumfuata shetani.
Shetani amewadanganya na kuwapotosha macho yao ili wasipate kuona na kuijua kweli,neema na thamani ya nguvu ya msalaba iletayo ukombozi ndani ya mtu,badala yake wameyakumbatia mafundisho manyonge na madhaifu kwa kujipa matumaini kwamba mtu akifa ataombewa na kupata msamaha wa ondoleo la dhambi.
Wanasahau kwamba imeandikwa "bora wafu wafao katika BWANA maana hao watafufuliwa siku ya mwisho".
Maana yake ni watu waliokufa katika Kristo Yesu.
Hakuna siku ya mwisho nyingine, bali ni sasa,hizi ndizo nyakati za mwisho ambazo Bwana Yesu yuaja upesi kuja kulinyakua kanisa lake,ambapo kabla ya ujio wake atawaandaa watakatifu wake ili wapate kumpokea mawinguni.
Hata wale wafu waliokufa katika BWANA ambao maandiko yanawataja, watafufuliwa kwanza ili waungane na walio hai,waliolikiri Jina Langu.Hawa ni wateule Wangu na watakatifu WANGU, niliopendezwa nao.(JESUS SPEAKS HIMSELF THROUGH ME).
Wale waliolikataa Jina langu ,na wale walio vuguvugu;wale waniitao BWANA,BWANA.Lakini hapo hapo wanajihudhurisha kwa miungu ,hao sina haja nao.(Yesu anaongea saa hii).
Nitawakataa, nitawatema, hawataingia RAHANI Mwangu,maana hawa ni wafu wanaoishi. Hawajafa katika BWANA wala hawaishi katika maisha matakatifu. (Roho yake imeongea ndani yangu,kuweni makini watu wa Mungu).
Kumbuka Andiko "waache wafu wazikane. ".Hawa ni wafu maana hawana walijualo, linaloendelea katika UFALME WA MUNGU.
Hawajui saa wala dalili za kuja kwa Mwana wa Adamu.Akili zao na fahamu zao haziwazi yaliyo ya Mungu, bali hujitaabisha na mambo ya dunia na kujihudhurisha kwa shetani.
WANAZIKANA KWA NAMNA GANI?
Roho wa umauti anawasubiria ili aweze kuwavaa na kuwachukua maana hawana kinga wala zuio au kizuizi chochote. Yeye asiye na Yesu ana roho wa umauti anatembea naye,anasubiri apate chanzo na sababu ili amvae na kuondoka naye.
Kuna wengine wameandikiwa umauti au kifo na wazazi wao,ndugu zao, Rafiki zao,na jamaa zao KAMA KAFARA LA UTAJIRI NA MALI.
Shetani hupenda kujifananisha na Mungu. Jinsi Yesu alivyotolewa kafara kama ondoleo la dhambi ya Ulimwengu, ndivyo hivyo hivyo shetani apendavyo kupewa kafara ya damu ya mtu.
Kafara ya damu ya mtu ina thamani kubwa kuliko damu ya mnyama,Kwasababu ina uhusiano na damu ya Yesu.Damu ya Yesu ina uungu mkuu sana,hivyo wote walio na Yesu wana damu kama Yake.
Mtu wa Mungu nisome kwa umakini sana hapa.
Maandiko yanasema,Yesu alisema yeyote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni,huyu ndiye ndugu yangu,na umbu langu,na mama yangu.Umbu kwa lugha nyingine ni dada.
Kwahiyo watu hawaitwi ndugu pasipo kuwa na vinasaba vya damu.
Unadhani kwanini sisi Watanzania huwa tunaitana kaka na dada? Maana tunachukuliana kama ndg wamoja. Kiroho sisi ni ndg sana,ndio maana utasikia ndg yetu,zetu Watanzania wamepatwa na shida fulani tuwasaidie.
Sasa twende kwa Yesu kwa mtiririko wa hapo juu.
Tumerithi ufalme wa Mungu kupitia imani ya baba yetu Ibrahimu,Yesu ni ukoo wa Yuda mtoto wa Yakobo,Yakobo ni mjukuu wa Ibrahimu.
Yesu anatokea katika shina la Daudi ,ambalo ni ukoo wa Yuda. Hivyo basi Yesu alikuwa na damu ya kibinadamu kamili kwasababu pia alizaliwa na mwanamke kama vile ambavyo watoto wote huzaliwa na mwanamke.
Kwahiyo kitendo cha Yesu kusema sisi tulio wake ni ndugu zake,maana yake katika imani tunakuwa katika ukoo mmoja na Baba yake ndiye Baba yetu pia. Glory to God, hallelujah!!!
Kwahiyo katika ulimwengu wa roho kinaumbika kitu kipya.Maana hata maandiko yanasema sisi tumefanyika viumbe vipya ndani ya Yesu.Tumebadilishwa kutoka ule utu wa kale na kuwa mpya ndani ya Kristo Yesu.
Tunafanyika kuwa watoto wa Mungu kwasababu tumebadilishwa na kuwa na sifa kama za Mungu wetu aliyetuumba. Kwahiyo kila kitu chetu ni kipya.
Damu yetu ni mpya kwasababu imetakaswa upya, imechujwa na kuwa safi na damu halisi.
Kwahiyo hii damu ndio ambayo shetani anaiwinda usiku na mchana ili aweze kuipata na kuichukua. Hii ina nguvu kuliko damu ya viumbe vyote.
Wanyama hawana damu safi,salama,na yenye thamani kama damu ya mtu;mtu aliyeokoka. Hii damu akiinywa shetani inampa nguvu na mafunuo kujua kitu gani kinaendelea katika ulimwengu wa roho wa NURUNI.
Yesu alisema Yeye ni nuru ya Ulimwengu.Kwahiyo katika vinasaba vya damu yake zipo chembe chembe ambazo zimebeba maono na mafunuo yenye taarifa sahihi za siri za mbingu.
Kwa kuwa Yesu anao ndugu zake ambao ni watoto wake,ambao ni watoto wa Mungu, basi hujikuta damu Yake iko sawa sawa na ndugu zake hawa,watu waliomkiri au waliokiri Jina Lake.
Lasivyo asingesema, sisi ni ndugu zake.Na ndugu zake wote ni wana wa Mungu walio ndani ya Yesu.Yesu ni ukoo wa watoto wote waliozaliwa mara ya pili kwa ajili ya Mungu.
Kwahiyo Yesu anawakilisha ukoo wa Mungu kwa watoto wa Mungu, akiwa Yeye ndiye mzaliwa wa kwanza. Ndio maana shetani anapenda kuwashikilia watoto wote waliozaliwa wakiwa wa kwanza,Kwasababu ni malango.
Ni malango kwasababu ni kielelezo cha Yesu Kristo. Kama alivyo Lango la baraka,uzima wa milele na mrithi wa viti vyote vya Enzi vya baba yetu.
Mtoto wa kwanza akiwa ni lango la laana,basi watoto wote watakaofuata watapata laana na mikosi.Labda tu kwa neema ya msalaba na damu iliyomwagika msalabani ipate kuwakomboa na kuwaweka huru.
Mtoto wa kwanza akiwa ni baraka ,halafu yuko upande wa Mungu ;Yaani yuko ndani ya Yesu.Shetani hupenda damu yake maana anajua atapata taarifa zote zilizomo kwake na kujua mpango wa Mungu ili aweze kumuibia na kisha kumakwamisha.
Kuna watoto wanaozaliwa na Nuru ya ulimwengu. Hawa tangu wakiwa tumboni mwa mama zao tayari Mungu alishawapaka mafuta.
Maandiko yanasema kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa;nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.
Angalia hapa Kumbe Mungu anawajua watoto wake. Shetani naye akishawajua anaanza utaratibu wa kuwashika. Hawezi kuwashika Wala kuwamiliki pasipokuwa na ridhaa ya wazazi,ndugu au jamaa zake.
Atakachokifanya ni kumshawishi mzazi kupitia kwa wachawi,waganga wa kienyeji, wazee wa mila na waaguzi waonao kwa kutumia mapepo ya utambuzi.
Kwamba wamtoe huyo mtoto madhabahuni kwao;kisha yeye watampatia nyota ya utajiri.
Hata kama ni cheo, au mafanikio mengine, lakini mafanikio yoyote huleta mali na vitu zikiwemo fedha. Hivi vitu vyote au wingi wa vitu mbalimbali, au wingi wa mali ni UTAJIRI.
Kwasababu ya tamaa ya mwanadamu ya kupenda pesa na utajiri hujikuta anamtoa au anawatoa watoto wake ili wawe kafara ya ngekewa yake.
Wapendwao kutolewa kafara huwa ni mabinti. Kwasababu hawa huwa ni rahisi kutoa damu zao kama sadaka kwa njia nyingi tofauti na watoto wa kiume ambao wao damu zao ni mpaka wapate ajali na vifo vyao.
Hawa watoto wa kike damu zao huanza kutoka pale wanapovunja ungo, damu ya ubikra, damu ya hedhi ya kila mwezi, damu ya wakati wa kujifungua, ajali n.k.
Kwahiyo wao wana damu nyingi na njia nyingi ya kutoa damu tofauti na wenzao wa kiume. Shetani anawapenda hawa wa kike kwa kuwa maungo yao ni rahisi kuwaingilia kwa kutumia tendo la ngono.
TENDO LA NGONO ni Agano rahisi kwa kuwa anakuwa anaziunganisha NAFSI za hawa watoto wa kike na mapepo yake,au waume wa kipepo.
Kwahiyo shetani anavyojua hawa watoto wana damu yenye uhusiano na Yesu ndipo hupenda kutumia Agano lenye nguvu na gumu kufunguka ambalo ni Agano la UMAUTI.
Hapa anamuapisha mzazi kwamba aseme binti yake/zake amewatoa moja kwa moja kwa mfalme mungu mkuu wa dunia (shetani) ili awe mume wao milele na milele na asikae akakiuka ndoa hii halali.
Wanaambatanisha kwamba kilichofungwa na Mungu mwanadamu asikifungue/asikitenganishe. (Wanaomba kinyume).
Akitaka kuivunja madhara yampate ikiwemo KIFO, kama jinsi mkataba ulivyoandikwa na cheti cha ndoa kilivyoandikwa ya kwamba binti yangu/zangu fulani na fulani nimewaozesha kwa mungu mkuu ambaye mume wenu atakuwa mume aitwaye PEPO MAUTI AU JINI MAITI.
Kwa kujua thamani ya maji yaliyomwagika msalabani. Wanatumia maji waliyooshea maiti, tena maiti iliyooza,kisha wanamnyesha huyu mtoto au watoto kwamba hii ni nadhiri na yamini kwamba sasa maji haya ya maiti yanakuunganisha na mume wako/wenu pepo maiti.
Hawataishia hapo tu,bali watamuosha au kuwaosha hawa watoto kwa kutumia hayo hayo maji waliyooshea maiti ili wamtakase katika ulimwengu wa giza kwa ajili ya kuolewa na huyo jini maiti.
Mambo yote haya yanafanyika kwa ajili ya kuua utu wa ndani,kuharibu nguvu za asili za ile damu ya Yesu ili anavyozidi kukua na kuongezeka na kupata maarifa asije akawasumbua.
Hapa ndipo KARAMA,VIPAWA,NDOTO NA NYOTA za watoto wa Mungu huanza kupotea, huandamwa na mikosi,nuksi kwa kila anachokifanya huwa hakifanikiwi.
Kwasababu yale maji yaliyooshea maiti iliyooza ndio hutumika kuleta roho za kuzaa mapooza na kumharibia maisha yake yote.
Mungu naye hayuko mbali huanza kumtafuta huyu mtoto/watoto wake.Hapa vita huibuka. Yeye anamtaka, na shetani hataki kumtoa, anadai alikabidhiwa na mzazi au wazazi wake.
Anatoa vifungu vyote vya mikataba,viapo na maagano waliyokubaliana na wazazi wake.
Mungu anaona isiwe taabu anaanza kumpa maarifa ya kutoka kwenye hivyo vifungo.
Njia rahisi, si nyingine bali damu ya Yesu. Kadri anavyozidi kutumia damu ya Yesu ndivyo yale maagano yaliyofanywa yanavyozidi kutoweka.Kwasababu ile damu ya huyu binti inazidi kuwa na nguvu kuzidi maagano yao yaliyofanyika au ambayo yalikuwa yakifanyika kwa kuchinja mnyama wa kafara.
Shetani anasema nilitumia maji ya maiti iliyooza, kwahiyo huyu atatakasika vipi?
Mungu ana maarifa zaidi ya shetani, Mungu anasema tumia maji yaliyomwagika msalabani kujiosha na kujtakasa.
Hapa ndipo nira huanza kukatika na kulegea hadi kuisha. Na zile nafsi za watu wote waliokuwa wamejiunganisha hapo kwenye hilo agano la utajiri ukatika pia.
Hapa itategemea waliapa viapo gani,kama ni viapo vya vifo, basi nafsi zao hukatika na mauti huwafikia Maana wao hawana damu iliyo safi na takatifu kama ya hawa waliokombolewa.
Kwahiyo huwa ni nafsi zao kupotea, sadaka zao ni damu yao.Shetani hapa hana msamaha;lazima uondoke maana anasema ulizipenda mali zangu kwahiyo huna budi kufa.
Vifo vya namna hii huwa havizuiliki maana huwa ni vya ghafla sana kwasababu vinasababishwa na huyo jini mauti au pepo mauti anayekuwa ni mauti katika mwili ila roho yake inafanya kazi kwa usaidizi wa mapepo mengine.
Turudi nyuma kidogo.
Na wanasema jinsi maiti alivyo wa baridi na mwili wa huyu binti uwe wa baridi,maisha yake yawe ya baridi ,asikae akawa na moto kwa kila akifanyacho.
Shetani hatendi kazi nje ya laana. Ni lazima kwanza aue vitu vya kiroho vilivyomo ndani ya mtu halafu apandikize roho nyingine ambazo ziko kinyume na mpango wa Mungu.
Kazi ya shetani na sifa kuu ya shetani ni kuiba, kuua na uongo.Anadanganya kwa kutenda kinyume na matarajio ya mwanadamu kisha anaua mpango wa Mungu ambao uko juu ya huyo mtu.
Mali za shetani hazidumu,utajiri wa shetani una mwisho wake.Lakini utajiri wa Mungu hauna mwisho wala ukomo;maana Yeye ndiye chanzo cha utajiri na mali.Shetani hana mali ispokuwa azipate kwa kuiba vitu walivyonavyo watoto wa Mungu.
KUNA WATU WANAFANYA VIAPO VYA KAFARA ZA NAFSI NA ROHO ZAO KWA AJILI YA MALI,UTAJIRI,MVUTO NA UMAARUFU.
Mtoto wa Mungu Kumbuka kule juu kichwa cha somo kilisemaje.Hapa ndipo tunakuja kwenye kiini cha somo.Kule nilikuwa ninawapitisha kwenye msingi wa haya maagano.
Wanafanya viapo hivi au vya namna hii kwa kujitoa wao kafara ili kwamba siku ikitokea mtu aliyekuwa ametolewa kafara akafunguka na kuyavunja maagano waliyokubaliana;basi wao ndio watumike kama mbadala wake.
Yaani zile nafsi za roho za watu wengine au ndugu,na jamaa zao walizokuwa wamezitoa kama sadaka za kafara kwa shetani,siku zikikombolewa kwa nguvu ya msalaba wa BWANA YESU basi wao hawana budi kutumikia kile kiapo chao cha awali.
Hapa ndipo watu hawa hujikuta wanadaiwa hizo mali,mvuto,utajiri,UMAARUFU, na cheo,na kwa kuwa walishaapa kwamba wao ndio watakuwa mbadala wake,hawawezi tena kupewa nafasi ya kuwatoa wengine.
Huwa wanaapa kwamba siku mtu huyu/hawa wakifunguka katika Kristo, basi mimi sina budi kuwa kafara kama mbadala wake.
Huwa wanajiaminisha na kuwa na ujasiri wa kufanya hivyo kwa vile wanajua vifungo walivyoviweka juu ya huyo mtu,havitawahi kuondolewa kamwe.
Lakini ashukuriwe Mungu aonaye sirini na kutujulisha mambo ya gizani. Jinsi anavyowapenda watu wake hata akaamua kumtoa mwanaye wa pekee ili awe KAFARA kwa ajili ya watu wake.
Naye si mwingine bali ni Yesu Kristo aliye hai.Yeye alivyokufa msalabani ilikuwa ni kafara ya ukombozi kwa wanadamu wote wa ulimwengu, ambao watahitaji msaada wake.
Hii kafara yake ndio inayoua nguvu za wale watu wote waliowatoa kafara ya viapo vya nafsi na roho ndugu zao au watoto wao au jamaa zao.
Kwa kuwa wao walitolewa kafara ya nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,na mvuto au cheo na umaarufu, hapa pia ukombozi wake unafanyika kwa njia ya Ukombozi wa kuuzwa nafsi yangu/zetu kwa shetani na baba,mama,kaka,mjomba,dada,bib na babu kwa kutumia kafara ya Yesu pale msalabani.
Hii ni lazima iandane na kanuni waliyoitumia kama ni kiapo, kivunjwe kwa kiapo.Kama ni sadaka ivunjwe kwa sadaka ,kama ni kafara ivunjwe kwa kafara katika ulimwengu wa Nuru,maana yote ya kwao yalifanyika katika ulimwengu wa giza.
TUSOME AYUBU 2:4
Shetani akamjibu BWANA,na kusema ,Ngozi kwa Ngozi,naam, yote aliyonayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake.
Kwahiyo shetani anavyokupa mali anategemea au anakupa kiapo cha kujitoa uhai iwapo kama utashindwa kukitunza kiapo chako na makubaliano yenu.
Ndio maana nikasema ni kiapo cha nafsi na roho kama kafara kwa ajili ya utajiri na mali,viapo vyako vinavyokuwa vikubwa, ndivyo na maagano yako yanavyozidi kuwa makubwa zaidi.
Maagano yako yanavyokuwa makubwa zaidi ndivyo na sadaka zako za kafara zinavyozidi kuwa nyingi na kubwa zaidi. Mtu haapi kwa shetani pasipo hakikisho la jambo analotaka kulifanya. Lazima kuwepo na kusudi au lengo.
Watu hawaendi kwenye ibada au maombi pasipo kusudi ndani ya mioyo yao;lazima wawe na dhamira iliyo ndani ya mioyo yao ambayo inawapelekea kwenda ibadani na kutaka maombi.
Dhamira hiyo ndio kusudi.Sasa tunaposema mtu anajitoa nafsi na roho kwa ajili ya utajiri,mali,mvuto,umaarufu, cheo au hata uchawi na uganga mkuu, ndio huo uhai anausema AYUBU.
KWANINI NI UHAI KWA AJILI YA UTAJIRI?
Kwasababu,nafsi inatunza roho,na roho ndio uhai wenyewe.Na mahali nafsi ya mtu ilipo ndipo mali yake ipo hapo.
Kwahiyo hawa watu wanatunza viapo vyao vya mali kwa kuzitoa au kuziweka nafsi na roho zao rehani ili mali zao zisiweze kupotea. Ili pia mtu waliyemuibia asiweze kuzidai.
Na ikitokea akaanza kuzidai basi umauti umkute;maana yeye alitolewa kama kafara kwa ajili ya mali za yule aliyeapa viapo vya nafsi na roho kwa ajili ya mali.
Ikitokea huyu aliyetolewa akawazidi nguvu na kuzichukua mali zake; ndipo ule usemi wa shetani unajidhihirisha,kwamba Ngozi kwa Ngozi na yote uliyonayo utayatoa kwa ajili ya uhai wako.
Lazima ajitoe yeye uhai wake,kwasababu hana mali tena,hana mtu tena wa kumtoa kafara maana si kila mtu unaweza kumtoa kafara, wengine damu zao ni chafu shetani hazihitaji.
Kwahiyo hapa inabidi wewe ndiye ufe kama mbadala wake.Tena mbaya zaidi yule aliyezikomboa yuko ndani ya Kristo;wanakuwa wanaona hakuna uwezekano tena wa kuzipata, maana nguvu zake hawaziwezi.
Shetani anamwambia uliapa kwamba utalizilinda, kwamba huyu uliyemtoa kafara hataweza kukuzidi nguvu,na uliapa hautanipa mwingine maana hakuna aliyekuwa na damu ya utakatifu kama huyu.
Sasa si mali zangu,si sadaka yako ya kafara, vyote vimeondoka, sasa ninauhitaji uhai wako mikononi mwangu,maana uliapa na kusaini HATI YA KIFO.Hivyo huna ujanja tena wa kutoka katika kiapo hiki
Hapa mtu hawezi kuchomoka tena.Hana jinsi tena ya kukwepa. Ndipo hujikuta mtu amekauka hapo hapo pasipo mjadala. Watu wanaapa hivi viapo pasipo kujua madhara yake huko mbeleni.
......................................................................
OMBA NAMI KWA IMANI SALA HII:
Sasa ikiwa wewe ni mtoto wa Mungu uko ndani ya Yesu na unahitaji kujikomboa kutoka huko,ni vizuri na wewe kwenda na sheria,kanuni na utaratibu wao.
Wao wanafanyia gizani,wewe jiombee au fanyia nuruni.
Na wewe sema Ngozi kwa Ngozi katika kuchukua nyota yangu,mali zangu,utajiri wangu,pesa zangu,cheo changu kwa kubatilisha sadaka ya kafara ya mwili wangu kwa sadaka ya kafara ya mwili wa Yesu uliokufa msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kuchukua nafsi yangu, roho yangu na uhai wangu kudai mali zangu na vitu vyangu vyote vilivyokuwa vimetolewa kama sadaka ya uhai,kubatilisha viapo vyao vya uhai wangu kwa kutumia uhai wa Yesu Kristo uliotolewa kama kafara ya ulimwengu pale msalabani.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi,kudai mali zangu ambazo ni uhai wangu uliomo katika damu yangu uliotolewa sadaka ya uhai wa damu yangu kwa shetani ,nabatilisha viapo vya hao Watu kwa kutumia sadaka ya kafara ya uhai uliomo katika damu ya Yesu.
Hii itakusaidia kuua kila chembe chembe za mawasiliano ambazo shetani alizipandikiza katika damu yako ili aweze kujua baraka zako zinazoingia ndani yako ambazo Mungu amezirejesha kwako.
Sina muda wa kutosha kufafanua sana ila twende na mtiririko huu.
Sema tena,Ngozi kwa Ngozi kwa ajili ya kubatilisha viapo vya nafsi vilivyoapwa juu yangu ili maji yaliyomo mwilini mwangu yatumike kama maji ya uzima kwa ajili ya shetani; sasa ninayabatilisha kwa kafara ya maji ya Yesu yaliyomwagika msalabani ili yanirejeshee uzima wangu maeneo yote.
Endelea kusema, Ngozi kwa Ngozi, wale wote waliodhani kwamba nitakufa siku ya kuzidai mali zangu kwa wao kujiapisha viapo vya nafsi,sasa sitakufa maana BwanaYesu alikishinda kifo kwa kafara ya msalabani,wao ndio watakufa na kuniachia baraka zangu zote.
Bwana Yesu alikishinda kifo kwa ajili yangu au yetu kwa kujitoa kafara pale msalabani, hivyo hamna mamlaka yoyote kuendelea kutushikilia katika viapo vya kafara za nafsi na roho kwa ajili ya mali na utajiri.
Ngozi kwa Ngozi: Viapo vyote vilivyoapwa kwa ajili yangu au yetu juu ya kuibiwa baraka za ku-renew au kurejesha mikataba ya kila mwisho wa mwaka ,sasa visiapwe tena kwasababu baraka zangu zinalindwa ndani ya kiapo cha damu ya Yesu iliyotolewa kafara pale msalabani.
Ngozi kwa Ngozi kwa wale wote walioapa viapo vya nafsi ili miungu izuilie baraka zetu zisiturudie, sasa miungu yote haina nguvu tena ,kwasababu kimiminika cha damu ya Yesu mara 12 iliyomwagika msalabani ninakimimina juu ya miungu 12 na miungu yote inayozuia baraka zetu iungue hadi iachie baraka zetu zote na ziturudie.
Ngozi kwa Ngozi, vile viapo vyote vilivyofanywa na wazazi ,ndugu ,jamaa na marafiki juu yetu wakaapa kwamba hata kama watakufa ,basi viapo vyao vife katika uhai wa kuendelea kutumika.
Ya kwamba hata siku moja tusikae tukazirejesha baraka zetu kama jinsi ile miili iliyofanya viapo hivyo haiwezi kurejewa na uhai tena.Ngozi kwa Ngozi kama ambavyo Yesu alirejewa na uhai katika mwili wake ,na sisi tunazirejesha baraka zetu ambazo ziko katika miili yote ambayo ni marehemu iliyokufa katika viapo vya nafsi na roho zao.
Ngozi kwa Ngozi. Vile viapo mlivyoviapa kwamba mwezi huu wa 12 hatutauvuka na kuuona mwaka mpya, tayari tumeshavuka kwa kafara ya matone 12 ya damu ya Yesu aliyekafarishwa pale msalabani.Amen.
.............................................................
Mpenzi msomaji mtoto wa Mungu hapo lazima uwe katika roho uombe haya maombi kwa imani ili uweze kutoka katika vifungo hivi vya nguvu za giza na makafara yaliyofanyika juu yako.
Ninawatahadharisha haya maombi siyo ya kitoto wala masihara yeyote aliyekuwa amememfanyia ndugu yake maagano ya namna hii, maombi haya ni upanga wa Mungu, sijui utakataje lakini habari mtaipata.
Kipindi hiki siyo cha mzaha na mimi huduma yangu ni ya kuvunja madhabahu na maagano, kwahiyo sina maombi ya rehema kwa waovu, upanga kwa upanga na jino kwa jino.
Naachiliaa moto wa Yesu kwa kila mchawi na mganga wa kienyeji na yeyote aliye na mpango wa kunitumia roho za mauti zimrudie yeye na wote waliojipanga kuwa kinyume nami.
Nawazingira wote wanisomao kwa nia ya kupata maarifa kutoka kwa Mungu uliye juu uwakinge na roho za visasi kutoka katika madhabahu za miungu yao ambazo kuanzia sasa wanaanza kuzipiga na kuzivunja katika Jina la Yesu Kristo aliye hai.
Mtoto wa Mungu ikiwa una sadaka itoe kwa imani na Mungu atakujibu katika maombi yako. Sindikiza maombi yako kwa njia ya kutoa sadaka.
Ahsante Bwana Yesu kwa ajili ya hizi roho ambazo nimezikomboa kwa mamlaka ya Jina lako,nazikukabidhi uzitunze na kuzilinda isipotee hata roho moja mpaka siku ile unarudi uikute iko kundini na uweze kuinyakua na kwenda nayo juu mbinguni kwa Baba,Amen.
MUNGU AWABARIKI SANA WATOTO WA MUNGU.
Amen! Atayeamini ndiye atakayepokea. Mambo yote ni katika imani, iwe nuruni au gizani,bado kote huko ni imani.Ubarikiwe sana mtumishi imenipasa kurudia somo hili na la mke hapo juu ili kufungua zaidi ubongo na kuelewa zaidi...
Mungu wa mbinguni akubariki pia nimebarikiwa sana na sala yako ya toba unayoweka kwenye maandiko yako mengi chini watu wanaweza kuona ni kawaida au kama utani tu ila kuna nguvu sana katika kumkiri Yesu kuwa mwokozi wa maisha yetu.