Habari,
Nilizaliwa late 80’s ,Nimesoma mkoani na hakika watu wengi walinisifia kuwa nina uwezo mzuri darasani achilia mbali zawadi mbalimbali nlizokuwa nazipata shuleni enzi hizo,ilikuwa ni furaha sanaa kwangu na kwa familia yangu,Mimi ni mototo wa kwanza ktk familia ya watoto 5 na wengine niwa kike.
Nilimaliza msingi with flying colours nkapata nafasi mkoa mwingine shule ya boarding,nakumbuka tulifaulu 14 tu out of 288,nyumban watu hawakuisha kuja home niwafundishe masomo nakumbuka baba kuna siku alinyambia watu sio wazuri mambo mengine km unayajua husifundishe wapotezee jifanye hujui-kwa wakati huo nilikuwa sijui mshua anamaanisha nini?
Baba alikuwa na hali nzuri na biashara zake zilikuwa zinaenda poa sanaaa,pesa kedekede na miradi mingi hapa na pale in short mambo yalikuwa poa sanaa,madogo walikuwa wanasoma shule nzuri nzuri tu
Baada ya kumaliza form six na kupata nafasi udsm nakumbuka mtaan nlikuwa naokekana km msomi flani hivi na vijana wengi walitolewa mifano kwangu yaan nkawa role model wa mtaa mzima.
Baada ya kupata nafasi udsm ndio massive changes zilianza kuonekana ktk familia yangu,baba alifilisika kabisa kabisa kila kukicha ni habari za kuibiwa na wafanyakazi wanakimbia ata wale ndugu zake alioamua kuwapa nafasi kumsaidia kazi zake nao walikengeuka na kusepa na mali zake within 6 months mzee alikuwa taaban sana,madogo wote wakarudishwa shule za serikali na waliokuwa sekondari walipelekwa shule za gharama za kawaida mambo yalichange vibaya sanaaa.Huku kwangu mambo yalikuwa magumu sanaa nilikuwa naumwa kichwa kila siku yani kichwa icho hakielezeki maumivu yake muda wote nipo room hall 5(room no2670) nimelala kwa maumivu ya kichwa daaah.
Despite kuwa one of the best in class,nlipofika mwaka wa pili nilidisco masomo tena kwa GPA kitu ambacho mpk leo huwa sikubaliani nacho period,nakumbuka semester ya kwanza nlikuwa na GPA ya 3.2 ila semester ya pili eti nilipata F masomo yote 8-hii siku mama yangu alilia sana tena mbele yangu,Mkuu wa department alikuwa ananijua uwezo wangu aliniita na kuniuliza imekuwaje ,sikuwa na cha kumueleza zaid ya kumwambia ata mm sijui,aliniomba niandike barua ya appeal ataisimami,baada ya muda nkasikia eti ameteuliwa mkuu mwingine wa department na habar yangu ikashia hapo
Nlirudi kitaa kusikilizia appeal yangu mpk leo naisubiri tu,pesa ya kusoma tena familia yangu hawakuwa nayo nikatafuta kazi ya ulinzi nikaanza kufanya na nlivopata pesa kidogo nkaapply chuo kimoja hapa t own,nlisoma kwa shida ambazo hazielezeki ata kidogo.Huko nyumban mambo yalikuwa worse ile mbaya watu wakawa wanatucheka na kushangaaa nini kimetokea though watu wengi waliamini kuna mchezo mchafu unafanyika ktk familia yangu so wazazi wawe macho wasilale wala nini.
Wadogo zangu wote waliishia form 4 aseee,tena wameyumba kiasi kwamba wawili wamezalishwa na hawana msaada wamekaa home tu hawana pa kwenda wala kitu cha kufanya,baba hana kazi ata shilling mia hana ameyumba kupita kiasi,mama yangu anapika mama ntilie bubu pale mtaani,huwa naumia sanaaa nkiona maisha ya nyumban sasa hivi.
Hapa nilipo sina kazi yeyote nazulula tu mjini,nlishaomba kazi nadhan sehemu zinafika 500 ila hola mpk leo the worse thing ni kuwa wale washkaji zangu udsm wameshakuwa na life bomba sanaaa sa hv ila mm nasaga jiwe tu-hii huwa inaniuma kwelikweli
Simshutumu mtu yeyote kwa chochote pengine ndo maisha tunayotakiwa kuishi .Nina mengi ya kuandika kiasi kwamba zinaweza kufika ata page 100 ila kwa leo naishia hapo ujumbe wangu hapa ni ule ule usemi aloniambia baba “watu sio wazuri mambo mengine km unayajua husifundishe wapotezee jifanye hujui”
Mwisho,Napenda niwaombe msamaha wote waliokumbwa na mawimbi kwa kuwa karibu na mm starting from Daddy ,najua mko wengine wengi sanaa mmeumia kwa njia moja au nyingene kwakuwa mko karibu yangu may be one day tutajua ukweli halisi what went wrong?.