Jicho lililopotea

Alafu nilipoona jicho nikashangaa hiiiii jicho lipi ? Kumbe lile na mama daaah hapo sawa.
 
Hii kitu ni ukweli mtupu mzee mlozi
Mimi wakati wa secondary nilishangaa tabia ya nikinunua chakula watu wananiomba ,wanakuja hata 5 afu wali sahani moja so mtu yupo tayari kupata hata kijiko kimoja
 
Mama Kijacho mtarajiwa mekuelewa kwa nguvu zoote!
 
Tushakuwa wa kubwa hatufanyi hayo makitu tena. No matter what mama yetu bado ni Mkali hata wajukuu zake anawanyoosha vile vile.

Na umri huu tulio nao mfano ukivaa nguo mama hajapenda basi atageuza jicho hasemi chochote anaongeza" hii ni ya kuvaa Mjini"😂😂😂

Watoto wa kike tunarithi kutoka kwa mama zetu, hakika.

Mdogo wangu ana mtoto Wa kike kama vile mm ndio namlea hadi sasa.ingawa anaishi kwa mama yake. yaani kanapenda wali balaa. Mara nyingi kananapenda kuja kwangu kutembea, kalikuwa na tabia ya kula kwa jirani, jirani uangu ana watoto umri wake.

Akitoka kucheza nikampa chakula anasema ameshiba, Siku moja nikamuita Chu.... Kimya nikamfata kweli yupo anakula na akina Joe. Na mama yao yupo siwezi kumtoa.
Si kusema ila nahisi nilimuona kwa jicho baya nikarudi kwangu, baada ya dk 10 nikamuita kwa sauti chu.... Njoo uvae sweta.akaja mpole kupitiliza akaanza kulia nikamuuliza kwa nini. Unalia " umeniona jicho baya ila ma mkubwa leo mm viatu nilikuwa nimevivaa" nikamwambia sio viatu, ukome kula kwa majirani mm sipendi.

Nikampigia mama yake, kumbe mama yake anamruhusuga kula kwa jirani yake huko kwao.nilimsema sana, hii Tabia sio nzuri.hilo likapita.

Kumbe Siku ilofata wakamuita kula aakasema ameshiba😂😂😂😂 muda ukafika akarudi kwa mama yake, Siku moja nikapika weekend nikamuita mtoto Huyo wa Jiran ale , Joe ananipenda sana, na anakulaga kwangu Mara nyingi, mweee Siku hiyo nimemuita ale akasema ameshiba nikaumia kwa nini kakataa? Au nae wamemzuia? Au chu..... Alisema? Nikakosa amani. Siku nyingine nikatoka kazini na zawad nikawaita wote na kaka yake yupo chekechea nikawapa zawadi wakapokea wakaenda wanakula kwao nikafatilia kama mama yao atawafokea, nikaona kimya. Nikawa na amani. Haya mambo bana😁
 
Umenikumbusha mbali sana mshana jr nilikuwa na bwana mdogo mmoja uyu nazani wa 90's na kalelewa ajui jicho hili tupo kwenye kikao sehemu akaanza lopoka nikamkazia jicho kuwa hiyo mada apotezee hakinielewa kabisa nikamkazia tena wala.hakunielewa nikakaza tena unajua kilichotokea mbele ya kadanasi akaniuliza kaka vipi mbona sikuelewi unaniangalia😀😀😀 dah nilikuwa mdogo galfa nikazuga tu hapana endelea

Baada ya ile meeting ndio nikamwambia eti sikuelewa ungenitumia meseji au kimemo nikasema matoto ya siku hizi bure kabisa
 
Siku hizi hayo macho yana kazi ya kushushulia majirani na kuwarembulia wanaume
 
Pole sana mama,next time umfundishe kama mwanao
 
Siku hizi hata kumtazama mtoto jicho la kukemea wanaona mtoto ataumia! Hivyo hawapendi kuwakwaza watoto wao.
Mtoto haonywi,hapigwi, hatumwi anafanya anavyotaka! Yaani shida tupu.

Malezi Ulaya yanatuponza. Toka ulaya waweke sheria kali za kutomwadhibu wala kumpiga mtoto hata akiwa wako, mashoga yakaanza kuongezeka! Mitoto ilikuwa bila maadili kabisa. Sasa naona ndiko tunakoelekea Africa.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…