thetallest
JF-Expert Member
- Oct 21, 2017
- 8,256
- 9,085
Katika kipindi cha bunge jioni hii ya leo, Mbunge Saed Kubenea alipata nafasi ya kuuliza swali la kisera kuhusu Tume ya Uchaguzi. Alihoji ni lini Serikali italeta hoja hiyo ijadiliwe ili ifanyiwe marekebisho Tume ya Uchaguzi kuzuia Wakurugenzi wa Halmashauri kuwa wasimamizi wa uchaguzi?
Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliombwa na Spika kutoa ufafanuzi akasema kuna kesi Mahakamani imefunguliwa kuhusu shauri hilo, hivyo Bunge haliwezi ingilia shauri lililoko mahakamani.
Je, ni jibu sahihi?
Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliombwa na Spika kutoa ufafanuzi akasema kuna kesi Mahakamani imefunguliwa kuhusu shauri hilo, hivyo Bunge haliwezi ingilia shauri lililoko mahakamani.
Je, ni jibu sahihi?