Mulama
JF-Expert Member
- Apr 16, 2011
- 3,047
- 1,823
Nimekuwa nikitafakari sana ujio wa jf, nikakumbuka miadhala inayofanyikaga hasa Dar. Nilichokumbuka ni kwamba kwenye miadhala hiyo huwa unakuta watu wanabishana huku wakiongea bila kupeana nafasi ya kusikilizana, yaani kila mtu anashindana na mwenzake kupitisha hoja yake kwa kupaza sauti kumzidi anayebishana naye! ( hapa namaanisha miadhara yote ya ndani au nje yenye kuhusisha majadiliano ya ana kwa ana)
Nikatamani kama wangekuwa wanapata nafasi kama ya jamvini jf ambapo kila mtu anaandika hoja zake na kujibiwa baada ya kusomwa na Kutafakariwa ingekuwa vizuri sana. Kwenye jf ni rahisi kujua uwezo wa mtu kuchangia hoja Fulani na pia kuelewa uwezo wa mchangiaji katika kuelewa mada anayoichangia.
I wish hata mikutano mingi ya kikazi hasa ya kiserikali ingekuwa inafanyika kupitia jf!
Hongera waasisi wa jf.
Nikatamani kama wangekuwa wanapata nafasi kama ya jamvini jf ambapo kila mtu anaandika hoja zake na kujibiwa baada ya kusomwa na Kutafakariwa ingekuwa vizuri sana. Kwenye jf ni rahisi kujua uwezo wa mtu kuchangia hoja Fulani na pia kuelewa uwezo wa mchangiaji katika kuelewa mada anayoichangia.
I wish hata mikutano mingi ya kikazi hasa ya kiserikali ingekuwa inafanyika kupitia jf!
Hongera waasisi wa jf.