Jetrudatabha
New Member
- Jul 18, 2021
- 3
- 3
#Hakika Jf ni mnyukano, Nami ni nani nisiunge mkono.
Kilicho bora milioni tano, kuwa balozi si kibano.
Nitashinda huu mtifuano, ukinipa hiyo yako tano.
Kwa maandishi Ambatano, na hoja changamano.
#Tulilisubili hili shindano, Kuleta hoja chanya.
Jf sio mvutano, nawe waweza jichanganya.
Kwa hoja zako tano, vingi waweza kusanya.
Hapa sio malumbano, hushinda mwingi wa chanya
# Hoja zenye kujenga, Na zenye Mabadiliko.
Jamii si kuitenga, Na huu ndio mwaliko.
Sera chanya kuchanga, Wana Jf kwao ndo heko.
Kizazi imara kujenga, kisicho na mihemko,
# Nidhamu ndio msingi, kuyapata mafanikio
Waambie hao warangi, Nidhamu ndio kioo
Kuna ubishani mwingi, Baba wa mafanikio
Nidhamu ndio kigingi, zingatia ule mafao
#Kaa chini fikilia, Eti siasa maji taka
Mpya katiba twaitaka, ya kake imechoka
Ina mambo yakusadikika, wachafu hufunika
huwabeba vibaka, wengi kama mapaka
# Katiba ni sheria mama, msojua niwajuze
Twapaswa kusimama, nchi tusiiuze
vijana akina mama, andiko tusilipuze
Msimamo kusimama, sheria tujifunze
# usawa kusimama, kila mtu oyaoya
sio kukicha kulalama, kila mtu kula soya
keki iwe salama, sote twimbe aleluya
Tanzania yangu mama, sintokuonea haya.
#Nitakupigania Daima, Misingi nitailinda
Sera zilizosimama, zituwezeshe kushinda
sheria zisizo lawama, zisizo zakupinda
zisizo bagua vyama, milima kupanda
# vijana kunufaika, sio kubweteka
mpya katiba kuiweka, kesho njema kufika
Ajira kujengeka, Imara msingi kusimika
Nawe dada na kaka, urithi kuuweka
#Tamati naifikia, Kura yako kunipigia
Mshindi kuwania, mimi ndo mtia nia
shairi kuwaimbia, tano kuchukua
Jf sana nasifia, imepigania demokrasia.
NAOMBA KURA YAKO YA HALI NA MALI
Kilicho bora milioni tano, kuwa balozi si kibano.
Nitashinda huu mtifuano, ukinipa hiyo yako tano.
Kwa maandishi Ambatano, na hoja changamano.
#Tulilisubili hili shindano, Kuleta hoja chanya.
Jf sio mvutano, nawe waweza jichanganya.
Kwa hoja zako tano, vingi waweza kusanya.
Hapa sio malumbano, hushinda mwingi wa chanya
# Hoja zenye kujenga, Na zenye Mabadiliko.
Jamii si kuitenga, Na huu ndio mwaliko.
Sera chanya kuchanga, Wana Jf kwao ndo heko.
Kizazi imara kujenga, kisicho na mihemko,
# Nidhamu ndio msingi, kuyapata mafanikio
Waambie hao warangi, Nidhamu ndio kioo
Kuna ubishani mwingi, Baba wa mafanikio
Nidhamu ndio kigingi, zingatia ule mafao
#Kaa chini fikilia, Eti siasa maji taka
Mpya katiba twaitaka, ya kake imechoka
Ina mambo yakusadikika, wachafu hufunika
huwabeba vibaka, wengi kama mapaka
# Katiba ni sheria mama, msojua niwajuze
Twapaswa kusimama, nchi tusiiuze
vijana akina mama, andiko tusilipuze
Msimamo kusimama, sheria tujifunze
# usawa kusimama, kila mtu oyaoya
sio kukicha kulalama, kila mtu kula soya
keki iwe salama, sote twimbe aleluya
Tanzania yangu mama, sintokuonea haya.
#Nitakupigania Daima, Misingi nitailinda
Sera zilizosimama, zituwezeshe kushinda
sheria zisizo lawama, zisizo zakupinda
zisizo bagua vyama, milima kupanda
# vijana kunufaika, sio kubweteka
mpya katiba kuiweka, kesho njema kufika
Ajira kujengeka, Imara msingi kusimika
Nawe dada na kaka, urithi kuuweka
#Tamati naifikia, Kura yako kunipigia
Mshindi kuwania, mimi ndo mtia nia
shairi kuwaimbia, tano kuchukua
Jf sana nasifia, imepigania demokrasia.
NAOMBA KURA YAKO YA HALI NA MALI