JF Hip-hop frestyle battle

JF Hip-hop frestyle battle

kwa jina lako chungu mfano wa homa ya jiji/

uniwezi shahidi mungu mm ni bonge la ligi/

sijui unaitwa pella huna pa kupandwa zaidi ya jela/

unajifunza usela na huna pa kushika zaidi ya dela/

mm sipimw niogope kama zimw/

kuwa makin unipi mvuto hata upige min/

mtoto wa mama leo unajiita mtoto wa mjin/

kwangu utaungamana mm fasihi nawe ni dini/
 
Punch hazieleweki utadhan ticha wa math/

pia mistari michaf, let them get bath/

Kwa kuchana you are not my level,

Waite wenzako wanaoweza hizi level/
Yeeeha nipo Kwa mtaa,,,,,,,,/

nawachora madenti wanavyo chapika Kwa chips Na ofa za chupa za bar....../
Shida balaaah....../ Uswazi Hari ni ngumu kila day nguna Na fungu la dagaa..../
 
Nataka kuwanyamazisha wazee wa kujisifia//
Niko na line kadhaa ila kidogo ntawapatia//
Unapotaka kuanzisha battle mada zingatia//
Sio muda wote we ni best nani kakuambia//
Freestyle kuhusu demu, ngoma ama maisha//
Ukishindwa zaidi njoo kama dizasta na stori za kuelimisha//
jadili kuhusu kesho sio kujadili ubora wa kujilazimisha//
Niite kama nlivojiita na haya kwenu nayawasilisha//
 
Mwana, mistari yako una search kwenye google//

Bando likiisha, unadrop kwenye Battle//

Usiingie ulingoni nami nitakutoa magego//

Ninavochana mimi hadi Nay anakosa Mitego//

1, 2, 3 Naanza kutema flows

Zenye akili sio fyatu, haters zawavunja jaws,
dogo hujui yai unakimbilia kiswahili.
Jogoo hafi kwa utitiri
Mi ndio ngariba wako wacha nikutahiri
Kisu nimekichovya kwenye pilipili.
Maumivu utakayopata utatia akili

ninaposhika mic ma mc wanapagawa
wanadata na kipawa
Vile navyowapa dawa.
wanachachawa.
 
Cheki kwanza navyofroo bila xoo,natembea bila biti.
Haiwezi kuwa drop we bixhoo,end utawait.
Sikia hii michano we feki usile ngano,mixer amila kitaa ukavimba.
Bad normal feki bila promo,mi mkal zaid y ximba..........
 
Yeah!

Au sio, ....cheki

Tamathali za semi zinafika kama utani
Niacheni
Mkizingua nitaleta tafrani
Kato zitozibika kwa wingi wa hii mizani,
Tafadhal
Huu ujuzi ni kutoka kwa maanani

Focus kwenye mzuka, tayari kimeshanuka, haina noma bila hata ya biti mbishi napasuka
Kama moshi umeshafuka, border nimeivuka, thanks kwa aliye juu kwa vigingi nilivyovuka
 
Usikiapo mayowe" ujue street nawarusha"
Wanaitaji niwakomboe" japo washua ukausha"
Machizi,masera" wote wananipa peace"
Hata wanaobreizi huko jera" wananyaka sipandishii"
Check nipo hivi" na jukumu nimejivika"
Ni soo siku hiz" home kuadhirika"
Sitofanya hajizi" wanaamini nitafunika"
Japo upinzani aukosi" kwa mwanadamu"
Niwekapo mizani huwa mikosi" nadhani awafahamu"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sikamatiki kwenye fani, nipo real si utani,
bado nipo gado peace kote uraiani
Roho ya chuki sina si kama yule wa madarakani, uswazi mpaka ushuani nasomeka kwenye ramani ahh!

Fake MCs naona wanajigamba sina hofu nao mwisho wao ni kama mwisho mwampamba
Tangu kale nilianza,
Ubishi tangu utotoni, heshima kwa brother Sugu na Balozi wa mamtoni,
Sina haja ya kuuficha ujuzi wala sioni soni, Dude nimeliamsha Jf yote mfukoni..ahhh

Still na here, full aminia
Mashine yangu Mandingo, ya kwako ni kibamia

Mitindo huru
kwa kasi ya kizulu, hiki kina kirefu bwana wadogo mtajidhuru
 
Round two
Bado in da houze, sisomeki kwenye Google yeah change your browse
Na south
Beach tupo hatuna hata migogoro
Weed na Shisha hewani hatuna haja ya vigodoro

Flow haijalishi uwe cool ama Mbishi
Kichwa yai elimika na kwangu pata udadisi, si fananishwi na wapuuziii
Unapenda umbea..yeah!
Tembelea Blog ya Michuziii

Kwa wingi wa michano kichwa kimejaa utitiri
na sio siri
Baada ya tamu inayofuata ni shubiri
Kaa makini nikupe faida ya hii tafsiri
Sio ajabu kwangu tungo tata huwa nazibikiri

Kumekucha
Na makucha yake
Jemedari nipo imara yani full mwake mwake

Dunia kitendawili, hadaa ya tupu mamboye, Anti mpiga dili muache huru brother Mbowe
Masaa yanasogea, dakika nazikong'otea, Jua kali chini ndala ubinadamu unapotea, kazi na dawa ndo msemo ninaoutegemea, wanauliza naishije, we usikonde muulize Bodea
 
Sili chao, mdogo mdogo imara kwenye ngao, sina dharao, peke yangu ndo nakomaa nao, masafa ya mbali yamebaki ndo ubora wao

Kila idara
Uwe na akili timamu au uwe fala, unda tela mapinduzi milele ka che Guevara
Ujinga wanajivika,
ila ukija kwangu kwa tungo ntakazokupa lazima utastaarabika

Mistari imepangana mistari ndani ya process, tungo tata kichwa yai we ni hopeless

Haina kujuana full noma full ungwasu, Eminem wa jiji nime chill yani basi tu
 
Yeeah! Bado mimi nipo
Free style bure jipatie yani bila hata ya max malipo

Eti hammaz hamnazo
Wanani diss nikiwa mbali wananiona mi kama kikwazo
Kisa kipaji, wanadhani nimekuja kuwachukulia ulaji, na wanajua uwezo wao ni mdogo kama bajaji
Jioni najiachia yani full kuserebuka
Na totoz kibao za kike zilizorembuka

Yeah!
Fanya kama unajaribu
Mtiti nitakaokuanzia mbona wa kibiti ni wa kivivu



Sijakosea
Na mkija ki' gay na wa babu sea
 
Yajayo yanafurahisha
ndiyo kauli ya nowadays
Free smile naiachia kidume nisipagawe
Mbinu kibao za kimakanika ka electronics kwa Faraday
No hofu feelings na sexual heeling na dream za Marvin gey
Sms kwa wangu mpenzi anasema what's up bey
Na sikosei
nipo strictly kitaani kusaka pay
Yes man, mi ni wakishua japo ctokei
oyster bay
Shout out kwa miss mzigua mpenda mawigi na hakosei...

days zinakata swadakta bila ya matata
Kimbembe mashetani ya JF.. Mwana hayataki kunikacha
Fikra kibao zikanijia kumcheki brother kaka
Si mwengine ni Mshana Jr..bingwa wa ndumba na malimbwata
Au Kiranga na drama zake za alinacha
Au binti Hemedi na ibada za mababu wa kale nilizozikacha
Au labda kwa mada za Malcolm Lumumba ndo yatakacha
Ooh! God nisaidie mja wako nisije safa
 
The king iz here, the king z back
Gusa unase mi mpekuzi ulipuke kama fatak
N' niaje
Yo! Mwana expert una feel aje
Mzuka upo on fire hautulii hata usemaje
Lina ubani limenukia tulizo lake litaje
Hold on! Tuliza pupa we shemeji yake Mage

Nimeranduka
Kwa bhangi Kali za yule jamaa pusha
Kipindi kile nilipokuwa nasoma yeah yani Mkoani Arusha
Acha kuleta dharau kwa wale waliyo kuvusha
Pene mkizipata hamtaki hata kushtushwa
Mkifulia mnarudi kwa wana eti tumejuta
 
The king him self is back,
Siwataki tena mawack,
Siku zote mkali ka chatu,
Nawatemea mate ka kifutu,
Wale wenye walo na ukurutu,
Wenye roho zao za kutu,
Kama hakimu wa kisutu,
 
siku ilikuwa ndefu kweli nimechoka
Najipumzisha zangu kwenye kigoda
Hivi kila siku mbona nazidi kukonda
Nguvu zimeniisha afya imezorota
Nikiwa natembea nataka kudondoka
mfukoni sina kitu kila mahala nimekopa
Nimejaribu kila kitu mpaka niliokoka
Mambo magumu nazidi tu kuporomoka
sasa natamani dunia hii kuondoka
kujitoa roho ah !! tu ndio naogopa
Uzee umenifika kustaafu kumeniponza
Nikikumbuka ujana machozi yananitoka
Nashtuka!!! kumbe nilikuwa tu naota !!!
Hii kali alafu ni battle hip hop
free style
 
Mzuka ni ulele
Nitaendelea kuchana na nikichana bila ya hofu mi ndo wao mteule

Haina haja ya kuhofia kaa mbali bwana mdogo, unajiita legendary kuflow hauwezi nakupa kisogo, hammaz shamba boy a.k.a sina mikogo, unakula haunywi maji subiri wakati wa kukata gogo...ahh

Saa saba inakaribia,
Ni muda wa kusali, kipaji hakijifichi ka mkatoliki na rozali, mwana anafurahia ka vile kamuona mwali, najua imekubamba kwa flow zenye tamathali
 
Holla Holla na mistari, nipo juu na hii habari nisome kwa umakini speed yangu ni ya Ferrari
Kamata simu ndinga cheki time na ipo shwari,
vibe ipo cool acha niteme cheche za shari
Nashika cm naanza kuchora hii mistari, kwa hizi bars nnazoshusha fake MCs wapo chali...ahhh

Check! Round two sihitaji hizo kiki, ukweli mchungu nautema sina hofu ya wanafiki,
Jf kutoa Uzi
Wanaangalia mtu, hata akiandika mashudu wanamchukulia kuntu, Asiyejulikana akiandika anachukuliwa butu

Unastaajabu hii tabia... Yal men hii niaje.. Sitojali ukinidiss hata man uniitajee

Forum imehodhiwa na members vichwa mashudu,
Uzi uchwara nyomi kibao wanazihusudu,
Jf ni msiba now wengi wanakula vibudu
Ni time ya kusepa hatuna haja na madudu.....
 
Sipo fesibuku wala Instagram
Mambo yte huku Jamii forum
Washa data habar kem kem
Bila utata yaan kla sehemu
Kiu hukata hii ndo yangu stimu
Yaani konki master wadau nawasalimu
 
Back
Top Bottom