JF Exclusive: CAG Report on IPTL/Tegeta Escrow Account

Busara tupu.
 
CCM wanaipeleka nchi pabaya, soon tutaanza kuchinjana

Kwa lipi?

Nakushauri subiri ripoti kamii, sikioni cha maana katika hizi kurasa zilizobandikwa hapa. Bali naona TANESCO inadaiwa na inajaribu kupunguza deni kwa kukaa chini na wadai wake.
 

Msomw vizuri Invisible ameandika maneno ya busara wacha kukurupuka na kushutumu watu wakati hauna ushahidi.
Invisible ameandika "asionewe mtu wala asilindwe mtu".

Mpaka sasa naona makurupuka na kuonea watu kuwaita ni wezi ilhali hizi kurasa chache zzilizowekwa humu hakuna implication yoyote ya huo wizi? kulikoni?

Nilisema, ripoti ikitoka watu watabadili nyimbo na bado nnaendelea kusema hivyo hivyo.
 
Last edited by a moderator:
.... Wadau, Tunasubiri Nini. Tuwachape Mawe Hao Wezi
 
Tunataka pesa zirudishwe na adhabu za sheria za mahakama ya kijeshi dhidi ya wezi zichukuliwe. Si adhabu za kisheria ya mahakama ya jaji Chande No!....majaji wanahusika.....sina imani na mahakama zetu.....mahakama imehusika ktk wizi huuuuu...No sitaki kusikia kesi hiko mahakamani....watatuzuia kusikia, kuona na kujadili mwenendo wa kesi....

Nataka mahakama za kijeshi...kuanzia tar 27 pindi tu baada ya mjadara wa bunge na concl zake.

Tutafatilia pia mjadara wa bunge...nao ukiwa kama wa katiba pendekezwa tutawafuata hapo kabla ya kufunga bunge.
 
Kwa lipi?

Nakushauri subiri ripoti kamii, sikioni cha maana katika hizi kurasa zilizobandikwa hapa. Bali naona TANESCO inadaiwa na inajaribu kupunguza deni kwa kukaa chini na wadai wake.

Sasa kama mambo ni mepesi jinsi unavyoyaona wewe bibie,hizo sarakasi za kunyofoa hizo kurasa ni za nini? Hivi unadhani hao Magamba wenzio wangekuwa wanaona kama unavyoona wewe kungekuwa na sarakasi zote hizi?
 
Kwanini kurasa hizo zinyofolewe? Mbona sijaona ubaya wake kwa upande wowote?
Kuna viashiria kuwa watu walionywa au walikuwa na uhakika kuwa malipo sio sahihi ila yamefanyika!!!
Pia kuna wingu la kodi hapo, sijui maindocument imeainishaje hili.
 
Invisible nakushangaa unaposema "taarifa za kuanza kunyofolewa kurasa za ripoti hii", unajishusha hadhi yako. Ripoti za mitaani kuchomolewa kurasa wewe au mwingine yeyote wa karne hii zinamstuwa?

Ripoti kamili na rasmi zipo, na wala hizo za mitaani zisikufanye ukakurupuka. Ngoja Zitto aziwasilishe kwa mujibu wa kanuni na sheria za bunge, kama zitakuwa mbadala na zile za CAG na PCCB hapo ndipo utakuwa na la kusema, kwa sasa chunga hadhi yako usiingizwe mkenge ukawa biased.
 

Usiwe na wasiwasi,mkongo sio kama Tanesco wamemonopoly kila kitu,kuna mikongo mitatu hawawezi kukata yote at the same time,kuna mkongo wa taifa,ttcl,eassy,seacom.
~Invisible weka pages zenye majina tuzisave kabisa,maana Mwenyekti na makamu wake wapo kigoma wanaweza wasirudi maana yanaweza yakatokea ya kina Ntayamira na abelliymana.
 
Last edited by a moderator:
Kwanini kurasa hizo zinyofolewe? Mbona sijaona ubaya wake kwa upande wowote?

Utaona kuwa kuna watu humu huwa hawafikiri hata kidogo, hizo kurasa zilichomolewa kwenye kompyuta? wanataka ripoti iliyovuja mitaani zaidi ya iliyopo kihalali kwa PAC?

Hata mimi sikioni ni nini kikubwa kwenye hizi kurasa zilizowekwa hapa mpaka watu waongee hovyo.
 

Tuombe Mungu hawa Nguruwe waendelee kudhulumiana...Maana bila kudhulumiana wananchi tutaendelea kunyanyasika
 

Sasa hizo page zinazosemekana zimenyofolewa zimesha kuwa "hazisisimui", unafikiri hizo zilizopo mitaani ndio zitakusisimua?

Mmeshakuwa disappointed mapema hii? mmejazana uongo humu, sasa subirini Zitto awasilishe ripoti yake rasmi muone mlivyo danganywa.
 

Tuliza papa hilo, wajanja wa ccm wapo kwenye hiyo list.......wewe mtoka povu kazi yako ni kushabikia wenzio watengeneze neema zao.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…