Jeshi la Polisi (Trafiki) lianze na vitu hivi ili kudhibiti ajali

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,673
22,264
Haya ndiyo mambo muhimu sana kwenye kudhibiti ajali za barabarani;

~ Iwekwe sheria ambayo itahakikisha kabla ya anayetaka leseni ya udereva pamoja na mafunzo anapimwa macho na dakitari wa polisi au wa hosipitali ya serikali, madereva wengi wana tatizo la mtoto wa jicho ambalo husababisha uono hafifu wakati wa usiku hasa macho yanapoangalia mwanga wa taa, tatizo hili ndilo chanzo cha magari kugongana yanapopishana.

~ Trafiki wapige marufuku matumizi ya diski za breki zinazochongwa mitaani na kubandikwa kwa gundi za viatu, hawa ajali ikitokea husingizia breki ilifeli kumbe gundi iliyeyuka na kusababisha breki isifanye kazi.

~ Mwisho matairi ya kuchongwa, matairi haya kwa hapo Dar yanachongwa karibu na kituo cha polisi Chang'ombe Temeke. Matairi haya huchongwa kurudishia mifereji (kashata) iliyokwisha, uchongaji huu husababisha tairi kulainika na gari kuyumba litembeapo pia kushindwa kusimama haraka breki ifungwapo.

Ninaamini endapo mambo haya niliyoyataja yatatekelezwa yataweza kusaidia sana kupunguza ajali kwani madereva wengi wanaona vizuri nyakati za mchana lakini wanauono hafifu sana usiku.

Sijui uhakiki wa leseni ni nini, leseni husika hupitia mikononi mwa trafiki na mtoaji ni TRA, sasa wanahakiki nini! Labda watueleze kama zipo leseni zinazotengenezwa mitaani.

Kuhusu vyuo, vingi havina walimu, mabasi na malori ya kufundishia madereva, wengi wao huanzia udeiwaka kwenye daladala kisha kwenye mabasi na utawakuta kwenye malori.
 
Sidhani kama ume wahi kusafiri mbali ukaona kati ya dereva na trafiki ni nani ana sabanisha ajali barabarani.
Trafiki wako kwa ajili ya hongo tuu. Mkishindwana ndipo ana kulima faini. Ina hitajika reform kubwa sana kikosi cha usalama barabarani.

Mfano mdogo, ukitoka Mtera kuelekea Iringa, baada ya kuvuka mizani mpya ya Iringa kuna gari la trafiki jeusi. Hukaa pale kazi yao ni kukusanya hongo tuu. Hii gari imelalamikiwa miaka mingi mno ila taasisi zote zimekaa kimya. Huu ni mradi wa wakubwa. Gari ikifika pale ina dondosha msokoto inaendelea.
 
Kweli mna shida sana. Kama uliyoandika ni kweli basi bora kutumia farasi na punda kwa usafiriq maana hamstahili kuwa na magari kwa umasikini huo

Mtu ananunua gari kwa mamilioni halafu anafunga break zilizopakwa Gundi
Matairi ya kuchonga
Sasa gari likaue wanaona sawa
Ubahili wa kishenzi kabisa huo
Poleni sana ila mtakufa sana
 
Haya ndiyo mambo muhimu sana kwenye kudhibiti ajali za barabarani;

~ Iwekwe sheria ambayo itahakikisha kabla ya anayetaka leseni ya udereva pamoja na mafunzo anapimwa macho na dakitari wa polisi au wa hosipitali ya serikali, madereva wengi wana tatizo la mtoto wa jicho ambalo husababisha uono hafifu wakati wa usiku hasa macho yanapoangalia mwanga wa taa, tatizo hili ndilo chanzo cha magari kugongana yanapopishana.

~ Trafiki wapige marufuku matumizi ya diski za breki zinazochongwa mitaani na kubandikwa kwa gundi za viatu, hawa ajali ikitokea husingizia breki ilifeli kumbe gundi iliyeyuka na kusababisha breki isifanye kazi.

~ Mwisho matairi ya kuchongwa, matairi haya kwa hapo Dar yanachongwa karibu na kituo cha polisi Chang'ombe Temeke. Matairi haya huchongwa kurudishia mifereji (kashata) iliyokwisha, uchongaji huu husababisha tairi kulainika na gari kuyumba litembeapo pia kushindwa kusimama haraka breki ifungwapo.

Ninaamini endapo mambo haya niliyoyataja yatatekelezwa yataweza kusaidia sana kupunguza ajali kwani madereva wengi wanaona vizuri nyakati za mchana lakini wanauono hafifu sana usiku.

Sijui uhakiki wa leseni ni nini, leseni husika hupitia mikononi mwa trafiki na mtoaji ni TRA, sasa wanahakiki nini! Labda watueleze kama zipo leseni zinazotengenezwa mitaani.

Kuhusu vyuo, vingi havina walimu, mabasi na malori ya kufundishia madereva, wengi wao huanzia udeiwaka kwenye daladala kisha kwenye mabasi na utawakuta kwenye malori.
nikishakoswa na ajali kama mara 3 usiku mkubwa sababu ya kupigwa na taa full.

asilimia kubwa ya madereva hasa wa dar mida ya usiku huwa wanaendesha kwa uzoefu tu sababu wengi hugem ea kwa kufata chaki pale anaposhindwa kuona vzuri kutokana na wimbi la hii mitaa inauotumika na watu
 
Sidhani kama ume wahi kusafiri mbali ukaona kati ya dereva na trafiki ni nani ana sabanisha ajali barabarani.
Trafiki wako kwa ajili ya hongo tuu. Mkishindwana ndipo ana kulima faini. Ina hitajika reform kubwa sana kikosi cha usalama barabarani.
Mfano mdogo, ukitoka Mtera kuelekea Iringa, baada ya kuvuka mizani mpya ya Iringa kuna gari la trafiki jeusi. Hukaa pale kazi yao ni kukusanya hongo tuu. Hii gari imelalamikiwa miaka mingi mno ila taasisi zote zimekaa kimya. Huu ni mradi wa wakubwa. Gari ikifika pale ina dondosha msokoto inaendelea.
Ninazungumzia anayeendesha gari wakati wa usiku na gari lenyewe, mimi binafsi niliwahi kutatizwa na mtotowajicho ambapo changamoto ilikuwa kupishana na magari wakati wa usiku, ilinilazimu nifanyiwe oparesheni ndipo niliporudisha uono wa macho yangu. Unaposema trafiki sijui alikuwa ananihusu vipi ndani ya gari yangu! Trafiki unakutana naye dakika moja na mnaachana, hausafiri naye na ajali inaweza kutokea unapoaanza tu safari.
 
Changamoto ya ajali ina pande 3.

-Trafiki ni chanzo cha ajali sababu wako barabarani sio kutoa ushauri na ku enforce sheria pale inapobidi bali wako kwa ajili ya kuchukua rushwa kwa madereva. Ukimnyima rushwa basi atalazimisha kukuandikia kosa lolote tu atakaloona linafaa kwa muda huo. Kikubwa ataomba leseni kwanza ukimpa tu anakuchorea wala hakuwazi. Kwa kuwa wanakuwepo zaidi nyakati za mchana tusiopenda bugudha tunaamua kusafiri usiku which is more risky.

-Tanroads hawafanyi maboresho ya barabara za inter regions, wanatakiwa ku update vibao hilo hawafanyi na wakiona malalamiko yamezidi wanazidisha matuta tu. Ajali nyingi za mikoani ni head on collisions yani Gar A inagongana na gari B uso kwa uso. Suluhisho la kudumu ni kuongeza njia ziwe walau njia 4 na kuweka zege zito katikati ili kutenganisha njia za kushoto na za kulia ili kuondoa kabisa uwezekano wa ajali.

-Madereva wengi ni wazembe kwenye kuendesha at highway speeds, huwa wana overtake za kijinga mno especially kwenye vilima na kona kali. Matokeo yake hugongana uso kwa uso kila kukicha. Coaster ya msiba ni hivyo, Frester ni hivyo. Control ya hawa watu ni ngumu sababu wengine wamenunua njia kwa matrafiki, wengine wanaendesha usiku ambako hamna matrafiki ilimradi kusiwe na kero za faini na vibao.
 
Hakika, ila umesahau miundo mbinu ya barabara...
Mimi nilianza kusafiri na mabasi ya shirika la reli kati ya Itigi na Mbeya nyakati za usiku huku barabara ni ya vumbi, hatukuwahi kushuhudia ajali kwani madereva walikuwa wanapimwa macho na afya, pia nilisafiri kati ya Mbeya na Dar kwa mabasi hayohayo nako haikuwahi kutokea ajali, ajali zilikuwa za mabasi ya DMT(Kamata) na mengineyo, barabara ilikuwa ya vumbi; kivumbi ilikuwa barabara ya Dar kwenda Arusha kupitia Chalinze na Segera. Ajali nyingi zilikuwa zikitokea usiku na baadhi ni za kugongana na treni Korogwe! Bado sijaelewa uhusiano kati ya rushwa na uendeshaji wa gari barabarani usiku japo nimeshuhudia rushwa zikifanyika, kumbuka hausafiri na trafiki.
 
Haya ndiyo mambo muhimu sana kwenye kudhibiti ajali za barabarani;

~ Iwekwe sheria ambayo itahakikisha kabla ya anayetaka leseni ya udereva pamoja na mafunzo anapimwa macho na dakitari wa polisi au wa hosipitali ya serikali, madereva wengi wana tatizo la mtoto wa jicho ambalo husababisha uono hafifu wakati wa usiku hasa macho yanapoangalia mwanga wa taa, tatizo hili ndilo chanzo cha magari kugongana yanapopishana.

~ Trafiki wapige marufuku matumizi ya diski za breki zinazochongwa mitaani na kubandikwa kwa gundi za viatu, hawa ajali ikitokea husingizia breki ilifeli kumbe gundi iliyeyuka na kusababisha breki isifanye kazi.

~ Mwisho matairi ya kuchongwa, matairi haya kwa hapo Dar yanachongwa karibu na kituo cha polisi Chang'ombe Temeke. Matairi haya huchongwa kurudishia mifereji (kashata) iliyokwisha, uchongaji huu husababisha tairi kulainika na gari kuyumba litembeapo pia kushindwa kusimama haraka breki ifungwapo.

Ninaamini endapo mambo haya niliyoyataja yatatekelezwa yataweza kusaidia sana kupunguza ajali kwani madereva wengi wanaona vizuri nyakati za mchana lakini wanauono hafifu sana usiku.

Sijui uhakiki wa leseni ni nini, leseni husika hupitia mikononi mwa trafiki na mtoaji ni TRA, sasa wanahakiki nini! Labda watueleze kama zipo leseni zinazotengenezwa mitaani.

Kuhusu vyuo, vingi havina walimu, mabasi na malori ya kufundishia madereva, wengi wao huanzia udeiwaka kwenye daladala kisha kwenye mabasi na utawakuta kwenye malori.
Mbona kama mnaamisha goli kwa makusudi kila ajali inapotokea mnarudia maneno yaleyale na soln zenu zile zile, kwa nini hamtaki kwanza kujua nini hasa chanzo cha ajari. Sababu kubwa ya ajari nchini ni miundo mbinu ya barabara, barabara bado ni nyembamba na si salama tena kutokana na matumizi kuongezeka kila kukicha. Tatizo mnakwepesha kwenye chanzo kwa makusudi ili kutaka kuonyesha serikali haikosei na haijakosea.

Madereva wa nchi tena wanastahili pongezi kwa kusafirisha mamilioni ya watu na mizigo kwenye barabara za hatari namna hii, hiyo panda mbili kwa mfano ndio mahali ambapo marehemu Chacha wangwe ndio alipata ajari lakini hatua bado hazijachukuliwa na bado mnasingizia madereva. Hapa kabla ya kuongeza sheria barabara itanuliwe hasa yale maeneo hatarishi. Watunga sera na wafanya maamuzi wajifunze kutoka nchi nyingine kuliko kuachia kila alieshiba kande aje na suluhu kwa vitu vinavyoonekana dhahiri shairi.
haya magari nchi nyingine huko yanajiendesha, waotengeneza barabara wakati mwingine waone umuhimu wa kupunguza kona kona.
Mawasiliano kwa maana ya alama za barabarani hasa usiku ndio za kuongeza zaidi, kama serikali kweli mnayo akili anzeni kupunguza rushwa kwa askari wenu manake mpaka akili, utu na weledi hawana tena.

Kauli za mafunzo kwa madereva hatutaki tena kusikia mtu anaendesha basi miaka na miaka mnataka aje na cheti gani.
 
Hasa Hawa askari wa speed torch ni wala rushwa wakubwa. Ile torch ni mradi kwa traffic police. Na Kuna namna wanaset speed zao,ukiendesha speed 50 kwenye mark kwao inasoma 53. Walinikamata eneo la Ngulelo Arusha na tulishapeana ishara na magari yanayotoka Arusha mjini kwamba wapo Ngulelo,nikawa natembea speed 45. Kufika wakanisimamisha na kuniambia nilikuwa 53. Nilitamani kuwaachia gari Kwa hasira. Mwishowe nikawaambia waandike fine nikalipe.
 
Trafiki anauhusiano gani na niliyoyataja, yaani macho, breki na magurudumu ya kuchonga!

Hili la uoni hafifu lina ukweli wa dhahiri. Na kuna magari baadhi ambayo taa zake zimegeuka juu huumiza sana madereva wa magari mengine, hali hii hupelekea ajali nyingi sana.
 
Kimsingi barabara zote zinapaswa kuwa na taa mara Giza linapoingia.

Kutembea barabarani nyakati za usiku kwa kutegemea taa za gari pekee ni mambo ya kienyeji sana.

Ni Sawa mtu kuwa na macho lakini ikifika usiku anahitaji mwanga wa taa ili aone vizuri
 
Haya ndiyo mambo muhimu sana kwenye kudhibiti ajali za barabarani;

~ Iwekwe sheria ambayo itahakikisha kabla ya anayetaka leseni ya udereva pamoja na mafunzo anapimwa macho na dakitari wa polisi au wa hosipitali ya serikali, madereva wengi wana tatizo la mtoto wa jicho ambalo husababisha uono hafifu wakati wa usiku hasa macho yanapoangalia mwanga wa taa, tatizo hili ndilo chanzo cha magari kugongana yanapopishana.

~ Trafiki wapige marufuku matumizi ya diski za breki zinazochongwa mitaani na kubandikwa kwa gundi za viatu, hawa ajali ikitokea husingizia breki ilifeli kumbe gundi iliyeyuka na kusababisha breki isifanye kazi.

~ Mwisho matairi ya kuchongwa, matairi haya kwa hapo Dar yanachongwa karibu na kituo cha polisi Chang'ombe Temeke. Matairi haya huchongwa kurudishia mifereji (kashata) iliyokwisha, uchongaji huu husababisha tairi kulainika na gari kuyumba litembeapo pia kushindwa kusimama haraka breki ifungwapo.

Ninaamini endapo mambo haya niliyoyataja yatatekelezwa yataweza kusaidia sana kupunguza ajali kwani madereva wengi wanaona vizuri nyakati za mchana lakini wanauono hafifu sana usiku.

Sijui uhakiki wa leseni ni nini, leseni husika hupitia mikononi mwa trafiki na mtoaji ni TRA, sasa wanahakiki nini! Labda watueleze kama zipo leseni zinazotengenezwa mitaani.

Kuhusu vyuo, vingi havina walimu, mabasi na malori ya kufundishia madereva, wengi wao huanzia udeiwaka kwenye daladala kisha kwenye mabasi na utawakuta kwenye malori.
Chanzo Cha Ajali ni kauli iliyotolewa Tunduma na Mzee Kinana ya Jeshi la polisi kupunguza Vituo vya ukaguzi barabarani. Ni matokeo ya ku politicize professions za watu.
 
Haya ndiyo mambo muhimu sana kwenye kudhibiti ajali za barabarani;

~ Iwekwe sheria ambayo itahakikisha kabla ya anayetaka leseni ya udereva pamoja na mafunzo anapimwa macho na dakitari wa polisi au wa hosipitali ya serikali, madereva wengi wana tatizo la mtoto wa jicho ambalo husababisha uono hafifu wakati wa usiku hasa macho yanapoangalia mwanga wa taa, tatizo hili ndilo chanzo cha magari kugongana yanapopishana.

~ Trafiki wapige marufuku matumizi ya diski za breki zinazochongwa mitaani na kubandikwa kwa gundi za viatu, hawa ajali ikitokea husingizia breki ilifeli kumbe gundi iliyeyuka na kusababisha breki isifanye kazi.

~ Mwisho matairi ya kuchongwa, matairi haya kwa hapo Dar yanachongwa karibu na kituo cha polisi Chang'ombe Temeke. Matairi haya huchongwa kurudishia mifereji (kashata) iliyokwisha, uchongaji huu husababisha tairi kulainika na gari kuyumba litembeapo pia kushindwa kusimama haraka breki ifungwapo.

Ninaamini endapo mambo haya niliyoyataja yatatekelezwa yataweza kusaidia sana kupunguza ajali kwani madereva wengi wanaona vizuri nyakati za mchana lakini wanauono hafifu sana usiku.

Sijui uhakiki wa leseni ni nini, leseni husika hupitia mikononi mwa trafiki na mtoaji ni TRA, sasa wanahakiki nini! Labda watueleze kama zipo leseni zinazotengenezwa mitaani.

Kuhusu vyuo, vingi havina walimu, mabasi na malori ya kufundishia madereva, wengi wao huanzia udeiwaka kwenye daladala kisha kwenye mabasi na utawakuta kwenye malori.
HUNA HOJA Sababu kubwa ya Ajali ni Mwendo kasi
Ubovu wa Magari
Barabara mbaya
Kutokujua Sheria
Kutokuwa na Leseni na ADHABU kuwa Ndogo
 
Hili la uoni hafifu lina ukweli wa dhahiri. Na kuna magari baadhi ambayo taa zake zimegeuka juu huumiza sana madereva wa magari mengine, hali hii hupelekea ajali nyingi sana.
Magari ya kisasa yana taa zinaumiza macho kama ujakalili mistari inakula kwako
 
Back
Top Bottom