Jeshi la Polisi mjiangalie

Jeshi la Polisi mjiangalie

mmteule

JF-Expert Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
6,035
Reaction score
15,064
Katika nchi yetu Jeshi la Polisi ni Taasisi kubwa ambayo imefanyakazi nyingi kubwa zilizolenga kulinda Usalama wa Raia na Mali zao. Mmekomesha Ujambazi maarufu kwa MTAJI WA MASKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE.

Mmekomesha Uvamizi wa majambazi benki. Mmekomesha vitendo vya Uvamizi wa Vituo vya Polisi na dalili za Vitendo vya Ugaidi kule Kibiti na Amboni. Hongereni sana.

Lakini kuna matukio ambayo siku za hivi karibuni yameonekana kama fedhea kwa Jeshi.

1. RPC GEITA anatangazia Umma gari lake limeibwa matairi Usiku amelala! Unajiuliza RPC analindwa 24/7 anamiliki askari na silaha zote ndani ya Mkoa. Hao Vibaka wamefikaje kwenye makazi yake, wamepataje Upenyo, na intelejensia yake ilikuwa wapi?

Je, kulikuwa na hajja ya kututangazia huu uzembe? Unapotezea siku zinaenda unakuta na hii na. 2

2. RPC MULIRO wa Mwanza namuamini sana, yeye anakuja na tukio lingine la Uvamizi wa Benki ya NMB IGOMA wezi wamekata bati, wamevunja ceilling board wameingia ndani ya Benki wamevuruga Vijana wake wanakuja kustuka tooo late tukio liko mwishoni. Unajiuliza benki inalindwa na askari wasiopungua wawili 24/7 walikuwa wapiiii. Kuna dalili zote za Uzembe kwenye matukio ya aina hii.

Tumewaaacha Maaskari waingie kwenye Lindo na SIMU JANJA hakuna namna askari yuko bize na simu yake WhatsApp, Insta, JF amenogewa, Huyo siyo askari tena huyo ni Mtalii wa Mtandaoni macho yamepigwa mwanga wa simu haoniiii ni mwendo wa kunyang'anywa silaha kirahisi tu, wezi wataingia kirahisi tu.

Lakini unajiuliza hawa makamanda wanatangazia Umma haya matukio ili tujifunze nini? Kwamba askari ni wazembe, au hawana mbinu za kukabili Vibaka na wezi, ama Jeshi halichuji taarifa kabla ya kuweka wazi kwa Umma?

Mjitafakari kwa hayo haijakaa vizuri kabisa, ni Mtizamo tu lakini. Salute
 
Wewe pitapita mitaa yenye malindo utajionea uzembe wa aina hiyo kibao tu
 
Katika nchi yetu Jeshi la Polisi ni Taasisi kubwa ambayo imefanyakazi nyingi kubwa zilizolenga kulinda Usalama wa Raia na Mali zao. Mmekomesha Ujambazi maarufu kwa MTAJI WA MASKINI NI NGUVU ZAKE MWENYEWE.

Mmekomesha Uvamizi wa majambazi benki. Mmekomesha vitendo vya Uvamizi wa Vituo vya Polisi na dalili za Vitendo vya Ugaidi kule Kibiti na Amboni. Hongereni sana.

Lakini kuna matukio ambayo siku za hivi karibuni yameonekana kama fedhea kwa Jeshi.

1. RPC GEITA anatangazia Umma gari lake limeibwa matairi Usiku amelala! Unajiuliza RPC analindwa 24/7 anamiliki askari na silaha zote ndani ya Mkoa. Hao Vibaka wamefikaje kwenye makazi yake, wamepataje Upenyo, na intelejensia yake ilikuwa wapi?

Je, kulikuwa na hajja ya kututangazia huu uzembe? Unapotezea siku zinaenda unakuta na hii na. 2

2. RPC MULIRO wa Mwanza namuamini sana, yeye anakuja na tukio lingine la Uvamizi wa Benki ya NMB IGOMA wezi wamekata bati, wamevunja ceilling board wameingia ndani ya Benki wamevuruga Vijana wake wanakuja kustuka tooo late tukio liko mwishoni. Unajiuliza benki inalindwa na askari wasiopungua wawili 24/7 walikuwa wapiiii. Kuna dalili zote za Uzembe kwenye matukio ya aina hii.

Tumewaaacha Maaskari waingie kwenye Lindo na SIMU JANJA hakuna namna askari yuko bize na simu yake WhatsApp, Insta, JF amenogewa, Huyo siyo askari tena huyo ni Mtalii wa Mtandaoni macho yamepigwa mwanga wa simu haoniiii ni mwendo wa kunyang'anywa silaha kirahisi tu, wezi wataingia kirahisi tu.

Lakini unajiuliza hawa makamanda wanatangazia Umma haya matukio ili tujifunze nini? Kwamba askari ni wazembe, au hawana mbinu za kukabili Vibaka na wezi, ama Jeshi halichuji taarifa kabla ya kuweka wazi kwa Umma?

Mjitafakari kwa hayo haijakaa vizuri kabisa, ni Mtizamo tu lakini. Salute
Mkuu RPC Geita gari yake iliibiwa matairi ikiwa Garage na sio Nyumbani kwake kumbuka hili na kuwa makini na utoaji wako taarifa, gari ilikuwa Garage ndpo vifaa hivyo vikaibiwa na si nyumban kwake

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
kero yangu tuu ni pale mwenye haki anapogeuzwa mtuhumiwa na mtuhumiwa kuwa mwenye haki
 
Lakini unajiuliza hawa makamanda wanatangazia Umma haya matukio ili tujifunze nini? Kwamba askari ni wazembe, au hawana mbinu za kukabili Vibaka na wezi, ama Jeshi halichuji taarifa kabla ya kuweka wazi kwa Umma?
Mkuu.una taaluma yoyote kuhusu ulinzi na usalama au unaongea kufuata moyo wako tu?
 
Hivi tunaelewa maana ya jeshi?

Wao hawalindi watu na mali wanalinda walivyoambiwa walinde

Jeshi au idara?

Jeshi lenye watendaji wabeba silaha
Nilitegemea hao polisi waachishwe kazi
 
We ndio umepotosha kuandika kuwa gari limeibiwa matairi wakati liko nyumbani kwa RPC wakati huo ni UONGO, gari lilikua garage
Kwani hiyo gereji anaimiliki yeye au hilo gari lilikuwa la Jeshi mpaka apoteze muda na attention kuutangazia Umma huo uzembe.
 
Kwani hiyo gereji anaimiliki yeye au hilo gari lilikuwa la Jeshi mpaka apoteze muda na attention kuutangazia Umma huo uzembe.
kuna uzembe polisi wanafanya,lakini huu wa gari haukupaswa kuwa sehemu ya mfano wako mkuu.gerage zinalala mpaka gari za jeshi,inategemea imeharibika kitu gani.

nyumbani kwa RPC kama unatafanikiwa kuiba huwezi ukaiba matairi ya gari,maana utakuwa umetumia nguvu kubwa matokeo kiduchu.
 
Kwani hiyo gereji anaimiliki yeye au hilo gari lilikuwa la Jeshi mpaka apoteze muda na attention kuutangazia Umma huo uzembe.
Kwan yeye ndiye alianza kutangaza ? Hyo mada iliingizwa tuu na waandishi alikuwa anaongelea swala lingine waandishi wakachomekea na hili la matairi ya gari ila haikuwa mada

Sent from my SM-A205F using JamiiForums mobile app
 
Hii ni kweli kabisa
Askari wakiwa Lindoni huna shida ya kumtafuta, simu aliyonayo ni kielelezo tosha kukupa location kutokana na mwanga wa simu hiyo, sasa unajiuliza huyo yuko Lindoni ama yuko Chart Room
 
kuna uzembe polisi wanafanya,lakini huu wa gari haukupaswa kuwa sehemu ya mfano wako mkuu.gerage zinalala mpaka gari za jeshi,inategemea imeharibika kitu gani.

nyumbani kwa RPC kama unatafanikiwa kuiba huwezi ukaiba matairi ya gari,maana utakuwa umetumia nguvu kubwa matokeo kiduchu.
Vipi hilo la IGOMA nalo wanasingiziwa Mkuu
 
Back
Top Bottom